Dena Amsi
R I P
- Aug 17, 2010
- 13,082
- 4,260
Salut!!
Nimesikia hiki kisa kimenisikitisha sana.
Mwanaume alikuwa na mpenzi wake wakakorofishana mwanaume kamweleza msichana kuwa kuanzia sasa mimi na wewe basi kwa njia ya simu.
Msichana kusikia hivyo kapanic kweli kamwambia Mwanaume kuwa "We need to talk" jamaa kakubali kamwambia njoo tuzungumze. Msichana kafika kabla ya mwanaume na kwa kuwa alikuwa na ufunguo wa nyumba kaingia kumsubiri.
Jamaa alipofika kamweleza kuwa kutokana na tabia yako ya kuwa na wanaume wengine mimi nimeamua sikuhitaji tena endelea na maisha yako na mimi na maisha yangu msichana kusikia hivyo kaja juu na hasira na kachukua laptop ya mwanaume katupa nje (gorofa ya pili).
Mwanaume kabaki na msimamo ule ule kuwa sikuhitaji tena fanya chochote unachotaka lakini sitabadili msimamo wangu. Cha kushangaza zaidi msichana kaondoka na hasira na kurudi baadae kachukua nguo, vyeti na vitu vingine vya mwanaume kachoma moto na kuondoka.
Najiuliza kwanini huyu msichana hakubali kuwa kaachwa??? Ni lazima uendelee kuishi na mtu ambaye hakuhitaji????. Kwanini asikubali kuwa hahitajiki tena???
Hapa ndipo pale lile swala la wanawake hupenda toka moyoni na wanaume hupenda kwa macho linapokuja na kuwa gumu.
Tujifunze kukubali ukweli na upendo wetu usizidi kipimo, maana hata ukiambiwa mimi na wewe basi usiumie sana kiasi hiki.
Hiki ni kisa kimetokea huku nilipo na huyu msichana anapelekwa mahakamani leo kwa kosa la uharibifu wa mali za huyu mwanaume.
Nawasilisha
Nimesikia hiki kisa kimenisikitisha sana.
Mwanaume alikuwa na mpenzi wake wakakorofishana mwanaume kamweleza msichana kuwa kuanzia sasa mimi na wewe basi kwa njia ya simu.
Msichana kusikia hivyo kapanic kweli kamwambia Mwanaume kuwa "We need to talk" jamaa kakubali kamwambia njoo tuzungumze. Msichana kafika kabla ya mwanaume na kwa kuwa alikuwa na ufunguo wa nyumba kaingia kumsubiri.
Jamaa alipofika kamweleza kuwa kutokana na tabia yako ya kuwa na wanaume wengine mimi nimeamua sikuhitaji tena endelea na maisha yako na mimi na maisha yangu msichana kusikia hivyo kaja juu na hasira na kachukua laptop ya mwanaume katupa nje (gorofa ya pili).
Mwanaume kabaki na msimamo ule ule kuwa sikuhitaji tena fanya chochote unachotaka lakini sitabadili msimamo wangu. Cha kushangaza zaidi msichana kaondoka na hasira na kurudi baadae kachukua nguo, vyeti na vitu vingine vya mwanaume kachoma moto na kuondoka.
Najiuliza kwanini huyu msichana hakubali kuwa kaachwa??? Ni lazima uendelee kuishi na mtu ambaye hakuhitaji????. Kwanini asikubali kuwa hahitajiki tena???
Hapa ndipo pale lile swala la wanawake hupenda toka moyoni na wanaume hupenda kwa macho linapokuja na kuwa gumu.
Tujifunze kukubali ukweli na upendo wetu usizidi kipimo, maana hata ukiambiwa mimi na wewe basi usiumie sana kiasi hiki.
Hiki ni kisa kimetokea huku nilipo na huyu msichana anapelekwa mahakamani leo kwa kosa la uharibifu wa mali za huyu mwanaume.
Nawasilisha