Kijiji Chetu
Member
- Jul 29, 2009
- 7
- 0
Mimi inanisikitisha sana kuona baadhi ya watu wakipata nafasi za kazi serikalini tena hadi kufikia ngazi ya uwaziri wakati vyeti vyao ni vya kuchonga? hawa mawaziri wawili wenye vyeti feki ni baadhi tu, naamini kabisa kama mamlaka zinazohusika zikiamua kuchunguza ajira za watu serikalini na ktk mashirika nyeti, amini usiamini Ofisi nyingi zitabaki nyeupe, wapo wengi tu wanaofanya kazi tena kwa mishahara minono huku wakitumia vyeti bandia au vya babu zao waliofariki, sasa kama mtu unaajiriwa na cheti bandia hata kazi zako nazo zitakuwa ni bandia tu... tuwe makini jamani, Taifa haliwezi kuendelea kwa kuwa na vihiyo wanaotoa maamuzi kana kwamba wako usingizini au wamekunywa mnazi au ile pombe ya kufunga kamba suruali...., mimi naziomba mamlaka husika zianzishe utaratibu wa kukagua vyeti vya watumishi serikalini na kuhakiki kweli ni vyao? hatuwezi kuvumilia kuona watu wenye sifa wakisota mitaani. tena ikiwezekana hata wamiliki wa vyuo nao washirikishwe ktk zoezi kama hilo la kuhakiki uhalali wa vyeti .. nina mengi ya kusema naomba niishie hapa. Naipenda Tanzania, naipenda Afrika, na Mungu anatupenda