Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,847
- 2,669
tunaambiwa kuwa GDP ni ile thamani ya pato la mwisho litokanalo na bidhaa au huduma fulani katika mwaka. pia ili kupata pato sahihi katika huduma na bidhaa zilizozalishwa, inachukuliwa thamani ya mwisho ya bidhaa husika ili kuepusha kuipa bidhaa thamani mara mbili au zaidi. mfano mmojawapo ni kitambaa cha nguo. huwezi kukipigia hiki kitambaa mahesabu katika pato la taifa kwani bado kipo katika mchakato wa kutengeneza bidhaa ya mwisho ambayo inaweza kuwa ni shati au gauni au suruali. pia ili kupata thamani ya hiyo bidhaa, ni mpaka mteja ainunue kwa matumizi binafsi. so kama mteja wa mwisho kanunua suruali kwa sh. 7000/- basi hicho kiasi ndio kinaingia kwenye pato la taifa. hapa tunazungumzia ile bidhaa iliyotengenezwa ndani ya nchi husika, na wala si mtumba au iliyotengenezwa nje ya nchi. bidhaa au huduma ambazo ni imported au exported zina mahesabu yake katika kukokotoa GDP. hayo macheche ni ya kuanzia tu. najua kuna wachumi wa kweli humu ambao haya mambo zaidi ya kuyasoma tu wanayafanyia kazi pia. katika hilo basi tubadilishane mawazo ili kuweza kujua mchakato halisi wa kujua pato sahihi la nchi yetu. hii pia itawasaidia wale wengine katika sekta tofauti kujua wanachangiaje katika pato la taifa lao (Tanzania).