RGforever
JF-Expert Member
- Apr 3, 2011
- 6,878
- 5,424
Tunamshukuru Mungu kwa kutuweka hai. Wiki iliyopita swali langu limeleta gumzo na maneno ya jaziba na matusi dhidi yangu kwa baadhi ya watu waliodhani kuwa Mimi ni mpinzani wa dini ya kiislamu.
Niwashukuru wote miliotoa maoni yenu kwenye ukurasa huu, mazuri na mabaya, kutoka wa marafiki na maadui, kwani wote mmetoa. Lakini jambo moja ndugu zangu wantazania naomba tujifunze kujadili hoja sio jaziba na chuki.
Naomba tujifunze kuangalia mambo katika usahihi sio jaziba udini na itikadi, tujaribu kufanya observation iliyo sahihi kisha tufanye
interpretation sahihi inayotokana na observation kisha unajua kipi cha kufanya ambayo ni application itakayokuongoza kwenye
implementation.
Dini isitufanye Tusiwe na uwezo wa kufikiri, kuhoji au kudadisi, kwa wale wanoweza futilia historia someni reason age, philosophers wangi pamoja na wa kiislamu ambao walipinga kanisa lilipokuwa linalzimisha watu kutii bila kuhoji hiyo likuwa karne ya 18'ni ajabu tunataka turudi nyuma.
Ni uvivu wa kufikiri na Kuniita mdini eti kwa sababu imehoji mamlaka ya katiba na kuwa katiba imevunjwa kule Zanzibar na waziri
mkuu ameunga mkono uvunjaji wa katiba ambayo wote pamoja na yeye tuliapa kuilinda.
Siwezi ogopa kusema ukweli eti kwa sababu nitawaudhi watu Flani au dini Flani, swala la nguo sio ajenda hapa, hiyo ni zile tunaita cheap politics.
Ndugu zangu waislamu kawasomeni wale wanaoitwa Muslim modern philosophers, ambao walitoa mchango mkubwa sana katika
kipindi hiki kinachoitwa enlighment age au reason age
SOURCE: MH. PETER MSIGWA BLOG