Tuitizame hii hotuba - Part One

OMG nitaitafuta hiyo CD nitaisambaza jimbo lote la mtera, anatukana kiasi hiki kura ya babu inadharika kiasi hiki? ila mwulizeni kilichomtoa cdm 2005 ni yeye ndiye aliyenufaika na EPA alinunuliwa akaacha kugombea. akaenda tarime aaaah the history of this bajaj inakera
 
Mkuu sana,kwa matusi aliyoporomosha huyo anaye itwa mhe. Sikubaliani na ruhusa ya kuanika kwenye mtandao huu ambao ni wa age zote{refer jf rule,zimeainisha sababu ya porn pics kutoruhsiwa ikiwemo sababu ya watoto kuwemo humu}Naamin huyo Lusinde ana akili mbovu,ya kuweza hata kurusha hzo picha hadharan!
Hilo likitokea,zitaruhusiwa hum,eti sababu aliye rusha ni public figure?
Mwongozo wako mkuu.

umetumwa na nani?

moja ya sifa ya great thinker ni kujua namna ya kuhandle issues kulingana na zilivyo, nasikitika kwamba silioni hili kwako, mfano wako wa picha za porn hauendani hata kidogo na issue iliyo mezani, kama angekua kasambaza mipicha ya hovyo hadhari ningejua namna ya kuhandle kama ningehitaji kureport issue hiyo.
 
OMG nitaitafuta hiyo CD nitaisambaza jimbo lote la mtera, anatukana kiasi hiki kura ya babu inadharika kiasi hiki? ila mwulizeni kilichomtoa cdm 2005 ni yeye ndiye aliyenufaika na EPA alinunuliwa akaacha kugombea. akaenda tarime aaaah the history of this bajaj inakera

sidhani kama ccm watampitisha kupeperusha bendera yao
 
kwa matusi haya lusinde atuombe radhi watanzania kwa lazima...haiwezekani heshima ya taifa ipotezwe na watu wachache wasio na adabu kama lusinde
 
Kwanza nilisikitika sana kwa mtu mzima kama LL kutoa matusi kama hayo mbele ya watu. Halafu sijui wana harakati wa jinsia wapo wapi, ametumia neno mimba kama ni laana au mchezo unaoweza kuufanyia mzaha huku mamia ya akina mama wanapoteza maisha hospitalini wakati wa kujifungua. Kwa hiyo anaona mimba kama ni jambo la mzaha sio? Halafu ina maana mahabusi zetu ni sehemu ya kudhalilisha watu na watawala wetu wanatumia hilo! Jeshi la polisi liko wapi hapa? Msajili wa vyama ameliona hilo au mpaka wawe ni wa kutoka upinzani? Nimebaki na maswali mengi kuliko majibu.
 
jamani kama watu walimfungulia Lema kesi ya uchaguzi wakati hawakuwa wagombea, kwa nini KIBAJAJ nae asifunguliwe kesi kwa upumbavu huu?

Mama Bisimba, na tanganyika Law society hebu tusaidieni
 
Mbunge huyo ni takataka kabisaaaa na wala hafai hata kungoza jamii, yaelekea famiali yake inaishi kwa matumaini ya matusi yake...... Ehhh mungu mjaalie Luinde ili afike 2015 aone navyong'olewa kwa CD yake ya matusi kusambazwa jimboni kwake. Aminnnnnnnnnnnnnn
 
Hiyo ni dalili ya kufilisika,kudhan kutofautiana na wewe ni kutumwa!
Anyway,na appreciate kazi ngumu uloifanya kuandika hotuba hii,shida yangu ilikuwa ni contradiction na jf rules.
Otherwise,tupo pamoja mkuu!
umetumwa na nani?

moja ya sifa ya great thinker ni kujua namna ya kuhandle issues kulingana na zilivyo, nasikitika kwamba silioni hili kwako, mfano wako wa picha za porn hauendani hata kidogo na issue iliyo mezani, kama angekua kasambaza mipicha ya hovyo hadhari ningejua namna ya kuhandle kama ningehitaji kureport issue hiyo.
 
jaman nani mwenye cv ya mh lusinde?naiomba tafadhali
HII HAPA MKUU, just a primary school leaver!

lusinde.png
 
Ninajua na nina hakika Watanzania sisi ni WAOGA mbaya kabisa ... LAKINI ... With this Noooh! We must do something for our nation Jamani!! Lazima hicho KITU kifanyike SASA ... !!!
mkuu tangu useme haya umeshafanya nini kuhusu huyu mlevi anayewawakilisha mtera??
 
Sikuwa nikielewa kwamba kuwa kiongozi ndani ya CCM kunahusishwa na utaahira kama wa kijana huyu. sasa naamini CHADEMA ni chama makini kwelikweli kwani kijana huyu huyu mwaka 2005 alijipenyeza kugombea ubunge wa jimbo hilo hilo la Mtera kwa tiketi ya CHADEMA na alitoswa kiaina. Alitoka akijiapiza siku mojauwafanyia "Kweli" CHADEMA. Alitangaza kurudi CCM na naona sasa ndiyo amepata fursa ya kutema sumu zake na kuuthibitishia umma utaahira wake. CHADEMA wasisononeke sana kwani wao si wa kwanza kuvurumishiwa matusi ya nguoni, hata katika uchaguzi uliopita uliomweka nafasi ya sasa alifanya hivyo kwa Baba yake mdogo Mzee Malecela! Yaelekea ana laana na iko siku atafanya hivyo kwa Mwenyekiti wake wa CCM. tatizo la nchi hii hatuna mfumo wa kuwa "vet" wanaowania uongozi kama wana akili timamu au la ndiyo maana hata machizi wanajipenyeza kufikia hatua za ngazi kubwa kama ubunge, ukuu wa wilaya n.k.
Hii yote ni kutokana na "kufa" kwa asasi za Usalama wa Taifa ambapo sasa wamegeuka kuwa mashabiki wa siasa zaidi ya kuwa watendaji. Nasema dhambi hii itamsakama kijana huyu katika maisha yake yote na pengine huu kuwa mwisho wake wa kisiasa.
Mungu ibariki Tanzania.
 
jamani kama watu walimfungulia Lema kesi ya uchaguzi wakati hawakuwa wagombea, kwa nini KIBAJAJ nae asifunguliwe kesi kwa upumbavu huu?

Mama Bisimba, na tanganyika Law society hebu tusaidieni

mtu mwenye contact za huyu mama au za yule eli... nkya naomba tafadhali
 
Hiyo ni dalili ya kufilisika,kudhan kutofautiana na wewe ni kutumwa!
Anyway,na appreciate kazi ngumu uloifanya kuandika hotuba hii,shida yangu ilikuwa ni contradiction na jf rules.
Otherwise,tupo pamoja mkuu!

nashukuru kwamba tuko pamoja.

kuhisi umetumwa hakukutokana na wewe kutofautiana na mimi, ukiangalia post zangu zaidi ya 900 sasa sijawahi kumuuliza mtu kama katumwa au lah na mara zote wapo watu wamekua wakitofautiana na wengine wakiunga mkono.

kwa hili sikutegemea kwa sababu lipo wazi sana, ukisoma humu ndani watu wanasema, sijui kama kweli, aliwahi ku,poromoshea matusi Mh Malecela, kama ni kweli basi kuna udhaifu mahali, mo ninafatilia siasa sana lakini hii ndio kwanza naisikia.

labda kweli ilitokea na kwa sababu za kisiasa labda ilibanwa, matokeo yake ni nini? leo kasimama hadharani mbele ya watoto, katumia dk 15 kutukana tu.

kama tukifichaficha, kama tukijaribu kulainisha maneno kwa sababu yale aliyotumia lusinde, kitu ambacho hata mie naamini, yana ukakasi sana, tutakua hatusaidii. . . wacha tuyaweke wazi, jamii ione, ningependa mwenyekiti wa chama cha kijani aone, ningependa watu wa mtera waone kisha wao wataamua kama anawafaa au lah.

ninataka kuamini mwenyekiti atanishukuru kwa kumsaidia kuweka wazi tabia ya kijana wake!
 
Namkubali lusinde kwa matusi na mipasho. Halafu wameru wanamsikiliza tu na kumshangilia. Hakika wameru wametiwa mimba kudadadeeki! Na ccm ikishinda nitaamini kweli ni vishababi. Nitaamini kuwa wameru ni wachumba tu. Na ole cdm washindwe uchaguzi kwa hoja za kipumbavu kama hizi toka timu ya kampeni ya ccm. Nitafikiria kurudisha kadi ya uanachama
 
:thinking:huyo mtoa hiyo hotuba nafikiri alikuwa ameshatupia viroba uwezi ukatamka maneno kama hayo mbele ya jamii, hata walevi wanakuwaga na staa ila huyu amepitiliza, anayo bahati baada ya mkutano angekuwa anatembea mtaani aangejutia aliyoyatamka, ila ndo mwanzo wa "CHAMA CHA MAFISADI" ccm kuingia kaburini, kwani kiama chao ni 2015 kwani kunao nguvu ya umma ambayo imefikisha umri wa kupiga kura kwaiyo watakuwa wamejiandikisha, ila tungeomba sheria ibadilishwe ukiwa nje ya jimbo lako uruhusiwe kupiga kura ya rais.
 
CCM oyeee Oyeeee!

Mh mwenyekiti wa chama, waheshimiwa viongozi wenzangu na wanachama wenzangu, nataka nianze kutofautiana hapahapa jukwaani na wenzangu, habari ya sisi kutukanwa halafu tunasema sisi hatutukani hatufanyi kazi ya kanisa hapa, kudadadeeeki matusi yakija nitatukana hoja zikija nitasema, potelea mbali

CCM oyeeeee.......oyeeee!

Niseme nisiseme.....semaaaaaa!

Unajua kuna wabunge wa chadema maji marefu unawalea sana, wewe ndio uliowachanja chale mpaka matakoni leo wanakutukana, nataka niwaambieni wenzetu wanajifanya wanajua kutukana hapa mwisho! ndio maana nimekuja kuwapasha kwamba hoja nyingine za kipuuzi wanazozisema chadema wanajitukana mpaka wao wenyewe, kuja kusema hapa kwamba mgombea wa ccm katoboa sikio kwa hiyo ni shoga maana yake na baba yake slaa nae ni shoga maana nae katoboa sikio kudadadeeeki CCM oyeeee....oyeeeee


Nataka niwaambie ndugu zangu msindanywe, msidanganywe na rangi utamu wa chai sukari, wale waliojazana katika chadema wote karibu nusu baba zao wametoboa masikio kwa hiyo na wao mashoga? Niwaambie nisiwaambie. . . .waambie! mbunge wa arusha mjini juzi alikua mahabusu na si tunajua kule mahabusu alifanywa nini, lakini hatutaki kusema

tuwalambe tusiwalambe.....walambeee!

Ndungu zangu nataka niwaambieni kwa habari ya lugha chafu wote sisi tunazo wala msifikiri hatujui sisi hatuna, tunajua Lema alikua mahabusu amepata bwana kule tunajua, na kuna wanaume wengine wameolewa sisi tunawafahamu, nataka kuwasihi sana, kwenye uchaguzi, kwenye uchaguzi tunajenga hoja za msingi lakini wakileta maneno ya honyo na hapa yapo, kudadadeeeki

nataka niwasihi sana, hakuna mtu asiye na makosa duniani, leo dr slaa anapita kuwasema wenzake wakati yeye upadri ulimshinda kanisa likamfukuza kwa kutia mimba wanakwaya

Sioi oyeeee! Oyeeee!

Mi nawafahamu wale, unajua tukiendelea kuwachekea hivi tukiendelea kuwambeleza hivi itafika mahali watatuchokoa machoni bora tule nao sahani moja, kuna bwe.ge mwingine yuko mle, kuna bweg.e mwingine yuko mle anajiita campain manager wa chadema, ukoo wa nyerere, baba yake mzazi wa nyerere akiitwa buhito alikua akitoboa masikio, alikua shoga? anajitukana mpaka mwenyewe kwa sababu ya akili mbovu, kutoboa masikio sio ushoga, masai wanatoboa, wagogo wanatoboa, wameru zamani walikua wanatoboa, wa-wakurya wanatoboa, wakamba wanatoboa, ye hajui historia anakuja hapa (huku kabana pua) ng'wee ng'wee ng'weeee, mbona ye ameliwa si hatusemi

ccm oyeee, oyeeeee
wanaokipenda chama mikono juuu!

(sauti ya kike kwa mbaali inasikika – wamekwisha!)

subiri niwaambie, hoja zinazojengwa hapa ni hoja za kipumbavu, kuna watu wanakuja kujenga hoja ya kitoto, kwamba msimchague sioi kwa sababu alizaliwa kenya, sio raia wa tanzania, mtu akizaliwa kwenye ndege anakua raia wa nchi gani? Acheni ushamba nyie, Suala la mtu kuzaliwa na suala na uraia ni vitu viwili tofauti, uchungu unapompata mwanamke anazalia hapohapo hawezi kusubiri, kuna wengine wamezaliwa kwenye mabasi mbona hatuwaiti raia wa basi, washamba wakubwa nyie, hiyo mnaona ni hoja ya kupita mnazungumza, halafu nyingine wanapita wamebana pua, msimchague sioi kwa sababu baba yake alikua mbunge, baba yake atarudi lini? Baba yake anarudi?

Ngojeni niwaeleze, na bahati nzuri najua walipo ntakua napiga hapa afu napiga palepale, kudadadeeeki . . .

PART TWO COMING SOON!

Muendelezo huu hapa

CCM oyeee .....oyeeeee!
Msikubali kudanganywa ndugu zangu maswala ya mtoto kufata kazi ya baba yake, katika tanzania ni kitu cha kawaida, tunao wanajeshi na watoto zao wanajeshi uongo kweli?....kweliiiiii! tunao madereva na watoto wao madereva uongo kweli?.....kweliiii, tunao wapiga debe na watoto zao wapiga debe uongo kweli . . . kweliiii! kuna ajabu gani kwa sioi piga makofi kwake.


Niwaulize nisiwaulize.....ulizaaaaaaa! Marehemu sumari angekua daktari na mtoto wake daktari CHADEMA wangegoma kunywa dawa (sauti ya kimbea kwa mbali inajibu . . . . wathubutu!), washamba nyie!


ccm oyee. . . oyeeee! Niwalambe nisiwalambe. . . . walambeee!


Ndio maana tunataka tuwaambie chama cha mapinduzi ndiyo chenye makamanda wa ukweli sio nyie makamanda feki, Jakaya Kikwete mwenyekiti wa ccm kazi yake zamani alikua mwanajeshi uongo kweli?..... kweliiii, kapteni komba alikua mwanajeshi uongo kweli? .......kweliiii! lakini wanavaa nguo za kijani halafu washamba ambao hata mgambo hawajapita wanavaa makombati.


ccm oyeee.....oyeeee!
Halafu katika washamba hakuna mshamba kama dokta slaa, anavaa kombati kuuubwa akitembea kama kajinyea vile (anapata shangwe kutoka kwa wanaomsikiliza, sorry to say this hapa hata mke wangu alicheka, nikamtazama kwa hasira hadi akaogopa!)


Nipige Nisipigeee?.........Pigaaaaaaaaaaaa
Bendera ya CCM ina rangi ganiiiiiiiiiiiiii?...................Kijaniiiiiiiiiiiiii.
Ukipanda mahindi yanaota na rangi ganiiiiiiiiiiiii?............Kijaniiiiiiiiiiiiii.
Ukipanda mpunga unaota na rangi ganiiiiiiiiiiiiii?.............Kijaniiiiiiiiiiiiiiii
Migomba yote ina rangi ganiiiiiiiiiii?...........................Kijaniiiiiiiii.
Piga makofi na vigelegele kwa chama cha mapinduzi.



Nataka niwaambie kama CHADEMA, kama viongozi wa CHADEMA ni vichaa wa kurogwa, mie ni kichaa wa kuzaliwa, kudadadeeeki! tarehe moja, dk slaa juzi, (anaguna) yaani katika watu washamba nimewashangaa dk slaa, anakakaa kwenye tv anasema eti ''ooooh hapa isipochaguliwa chadema patachimbika'' kama ni fujo itaanzia arumeru, kwa nini isingeanzia kwa mke wake? Ngoja niwaambie ndugu zangu, alichokua anakisema slaa, alichokua anatutishia vita slaa mimi namwambia anatishia kujamba wakati anaharisha.


ccm oyeee....oyeeee!. wangapi mtampa kura kura sioi, mikono juu....(watu wananyanyua mikono), hatufanyi kazi ya kanisa hapa! hapa tumekuja kuwaambia kwa suala la kutishana hakuna mtu anayeogopa, wote si tumeaga na nataka niwaambie slaa yule anavimba macho ya watu, lakini kama slaa ana ubavu nipeni mi tuweke ulingo hapa, ngumi moja naua yule, nikikusanya yule nipige mkono mmoja mnakuja kuokota yule, akiona watu wamejaa (anabana pua) ng'weng'weng'wee ng'weng'weng'wee upadri umemshinda ataweza serikali? thubutuu!

Nataka niwaambie, ndugu zangu wa arumeru, suala la uchaguzi mdogo sio suala la kudanganywa, wanakuja CDM hapa wanakudanganyeni, kwamba watapora mashamba ya wazungu wawagawieni, muasisi wa chama cha CDM ndugu mtei ana shamba hapa heka 700 mbona hawampori wawagawie? wangeanza kwanza la mtei, sio kuwadanganya wananchi, kama wanawapenda kweli wa meru wamwambie mzee mtei chukua shamba lako rudisha kwa watu wa meru(sauti ile ya kike. . . hatudanganyiki)

ccm oyeee.....oyeeee!
Niwachane nisiwachane?......wachaneee!

Vijana wenzangu, CDM inawapa pesa za kunywa viroba, mnalewa viroba na bangi mnazomea wazee wenu, halafu wenzenu wanapita na helikopta wanawaona machizi

niseme nisiseme.....semaaa!

Kokote duniani askari wanaoteka nchi ni askari wa miguu wacha wao waruke juu si tunateka nchi, wao wanaruka na helicopter si tunachukua jimbo asubuhi, kudadadeeki, mnakuja mnadanganywa hapa eti ooh chadema, sijui ooh nasari ataleta ajira na soko, ajira atazitoa wapi? Watu hawana shukrani anasimama hapa dk slaa anatukana ccm, hawajafanya kitu, hawajafanya kitu, shule alizosoma yeye zimejengwa na baba yake? shule zimejengwa na serikali ya chama cha mapinduzi, watu wanajiita wamesoma chuo kikuu (chuo hicho) kimejengwa na serikali ya chama cha mapinduzi, nionesheni hapa chuo walichojenga CDM. . . hakunaaa!

ccm oyeee....oyeeee!

Wanatuletea sera ya jogoo, nataka mkatae sera ya CDM ni sera ya jogoo, Jogoo katika makuku maongo hakuna kama jogoo, Jogoo linapokua linamtaka kuku mwenzake linadanganya linamwambia nitakushonea gauni reeefu mpaka huku (anainama huku akizunguka kuonyesha mfano wa jogoo, watu wanalipuka kwa kicheko)

Niseme nisiseme. . . .semaaaa!

Kataeni uongo wa jogoo, linaahidi kushona gauni refu wakati lenyewe likiinama hata chupi halina, waongo wakubwa tunawajua, na hivyo viroba mnavyokunywa vijana, viroba mnavyokunywa vijana mwisho tarehe moja, wataondoka watakuacheni mmetukana wazee wenu, mmewapiga mawe wazee wenu, na mimi nataka niwaambie vijana wa CDM utaonekana kichaa ukionekana unazomea rangi ya kijani maana utakuta mti una rangi gani....kijani! unaanza uhuuuu watu wanasema huyu chizi, mchezaji aliyeumia ni mchezaji wa timu ya ccm tunaweka mchezaji wa ccm, suruali yangu nyeusi imetoboka siwezi kuweka kiraka cheupe kama nina akili nzuri, inabidi niweke cha rangi gani? Kijaniii! Hata hilo mnataka mtu atoke dodoma kuja kuwaambia? Kama huoni kwa macho papasa kwa mkono utapa majibu.


Ccm oyeeeee.....oyeeeee!
Niwaambie nisiwaambie hawa.....waambie!...ngoja niwaambie watu wa CDM nyie


nikakutana na kijana mmoja akanichekesha sana, ananiambia mwanaume mzima, basi kati ya watu ambao hawajui kiswahili mbowe hajui kiswahili, mbowe anasimama anasema nina uchungu mkubwa, bibilia inasema hivi wanawake mtazaa kwa uchungu, wanaume watakula kwa jasho uongo kweli...kweliiii! kama mbowe anauchungu ana mimba?....vicheko


ccm oyeeee.....oyeeee!


Nataka niwaambie, kipindi hiki ni kipindi cha lala salama, ukiona mtu anasikia kichefufu, ukiona mtu anatema mate, ukimuona mtu anaichukia ccm ujue tayari tumeshamtia mimba, ndio maana unawaona saa hizi wanapiga kelele, unaona kina slaa wanapiga kilele, wameshapigwa mimba, mbowe pigwa mimba, nasari pigwa mimba....mayoweee

Tarehe moja wanaenda kujifungua mtoto anaitwa sioi, piga makofii. Kichefuchefu chote kitawaisha utawaona ooh tulikua pamoja tulikua pamoja kudadadeeki.


Niwachane nisiwachane?.....wachane!

we ukiona unapita mwanaccm humsemeshi mtu anakufanyia hivi (anaonesha V, ishara ya CDM) ujue ana mimba ya mapacha, mnunulie udongo, mnunulie maembe mabovu, mnunulie vitu vya uchachu tarehe moja anajifungua sioi anakwenda bungeni na wao mimba wanazaa hapohapo.

Tuwapime wenye mimba tusiwapime....tuwapimeeee
Tuwapime wenye mimba tusiwapime....tuwapimeeee

nitakuuliza swali, nitakuuliza swali, atakaempigia kura sioi anyoshe mkono kama hakunyosha jua ana mimba

ccm oyeeee....oyeeee!

Hotuba inaisha, zinaisha wanaonyeshwa watoto wengi wa shule za msingi, wamevaa uniform za shule nao walikua kati ya watu waliohudhuria huu mkutano ambao bwana Livingstone alihudhuria.


My take:

  1. Ukisoma hapa mwisho kuna udhalilishaji mkubwa kwa wanawake, inasikitisha sana!
  2. Kuna watoto wengi wa shule ya msingi ambao kwa kuwatizama tu, hawajafika hata miaka 15, sijui wanajifunza nini, Jamaa hakuzingatia hili kabisa wakati anatema u.pupu wake
  3. Jamaa amedhalilisha sana chama, kuna maeneo mengi ameongea vitu vyenye ukakasi na amejaribu kutuaminisha kwamba CCM (hata wale ninaowaheshimu sana) ndio wapo hivo
  4. Naomba hii clip apewe mwenyekiti wa chama aitizame mwanzo hadi mwisho, naamini yeye yuko na busara ya kutosha, atajua kitu cha kufanya

My take:
at least CCM is trying to reveal its true colour and what it represents!
 
My take:
at least CCM is trying to reveal its true colour and what it represents!

M,agamba wasirahie haya matusi hicho kichwa kimevunda ipo siku kitapasukia kwao kianze kutoa harufu. Shauri yao
 
Naomba uthibitisho wa madaktari kama huyu jamaaa alikaa miezi 9 kwenye tumbo la mama yake,,,:lock1::crazy:
 
Back
Top Bottom