Je, sheria zetu za kupambana na rushwa haziwaruhusu PCCB kufanya haya ambayo Taasisi ya Kuzuia Rushwa nchini Malawi (ACB) wamejaribu kuyafanya?
Bila hatua kama hizi ambazo zitasaidia kuweka precedent kwa watu watakaopewa madaraka na kujua nini kinaweza kuwatokea pindi wakifanya madudu yao na kugunduliwa tutafika kweli?
============
TAASISI ya Kuzuia Rushwa nchini Malawi (ACB) imekamata mali za rais wa zamani wa nchi hiyo, Bakili Muluzi, kama dhamana katika kesi ya rushwa inayomkabili.
Hatua hiyo ya ACB imechukuliwa wakati bado inaendelea na uchunguzi katika kesi hiyo ambayo Muluzi anadaiwa kuingiza kwenye akaunti yake fedha za wafadhili zinazofikia dola za Marekani milioni 11.
Taasisi hiyo imesema kwamba imekamata jumba analoishi lenye thamani ya mamilioni ya fedha lililoko katika mji wa biashara wa Blantyre. Imesema pia ya kuwa imekamata magari 44 kati ya magari 149 ambayo rais huyo wa zamani wa Malawi anamiliki.
Vingine vilivyokamatwa ni jumba lake la biashara la Keza Office Park ambalo lilizinduliwa kwa mbwembwe, mgeni mwalikwa wakati huo Rais wa Tanzania, Benjamin Mkapa, na akaunti zake zote za benki.
Habari zinasema wakati hayo yakiendelea, Muluzi mwenyewe yuko Uingereza kwa matibabu. Ofisa Uhusiano wa ACB, Egrita Ndala, amekaririwa na gazeti la kila siku la Malawi- The Daily Times, akisema taasisi hiyo bado inaendelea na uchunguzi wake.
"Kikosi cha Kupambana na Rushwa (ACB) bado kinaendelea na uchunguzi wa mali nyingine ili kujiridhisha na umiliki wake. Ni vigumu kwa sasa kusema mali nyingine ambazo zimepangwa kuchukuliwa, " alisema Ndala.
Katika hatua nyingine, kabla ya tukio hili la wiki hii, hivi karibuni rais huyo wa zamani wa Malawi alizuiwa kusafiri kwenda Uingereza na pasi yake ya kusafiria ikanyang'anywa baada ya kuzuka uvumi kwamba angetorokea Uingereza. Hata hivyo, aliruhusiwa kuondoka kabla ya ACB kuvamia mali zake kama dhamana endapo atashindwa kesi hiyo na hatarejea nchini humo.
Habari kutoka nchini humo zinasema ya kuwa mwanasheria wa Muluzi, Jai Banda, ameomba zoezi la kukamata mali za Rais huyo lisitishwe. Muluzi aliwahi kukamatwa huko nyuma kwa kwa kesi hiyo hiyo.
CHANZO: Raia Mwema
Bila hatua kama hizi ambazo zitasaidia kuweka precedent kwa watu watakaopewa madaraka na kujua nini kinaweza kuwatokea pindi wakifanya madudu yao na kugunduliwa tutafika kweli?
============
Mali za Muluzi zakamatwa Malawi
TAASISI ya Kuzuia Rushwa nchini Malawi (ACB) imekamata mali za rais wa zamani wa nchi hiyo, Bakili Muluzi, kama dhamana katika kesi ya rushwa inayomkabili.
Hatua hiyo ya ACB imechukuliwa wakati bado inaendelea na uchunguzi katika kesi hiyo ambayo Muluzi anadaiwa kuingiza kwenye akaunti yake fedha za wafadhili zinazofikia dola za Marekani milioni 11.
Taasisi hiyo imesema kwamba imekamata jumba analoishi lenye thamani ya mamilioni ya fedha lililoko katika mji wa biashara wa Blantyre. Imesema pia ya kuwa imekamata magari 44 kati ya magari 149 ambayo rais huyo wa zamani wa Malawi anamiliki.
Vingine vilivyokamatwa ni jumba lake la biashara la Keza Office Park ambalo lilizinduliwa kwa mbwembwe, mgeni mwalikwa wakati huo Rais wa Tanzania, Benjamin Mkapa, na akaunti zake zote za benki.
Habari zinasema wakati hayo yakiendelea, Muluzi mwenyewe yuko Uingereza kwa matibabu. Ofisa Uhusiano wa ACB, Egrita Ndala, amekaririwa na gazeti la kila siku la Malawi- The Daily Times, akisema taasisi hiyo bado inaendelea na uchunguzi wake.
"Kikosi cha Kupambana na Rushwa (ACB) bado kinaendelea na uchunguzi wa mali nyingine ili kujiridhisha na umiliki wake. Ni vigumu kwa sasa kusema mali nyingine ambazo zimepangwa kuchukuliwa, " alisema Ndala.
Katika hatua nyingine, kabla ya tukio hili la wiki hii, hivi karibuni rais huyo wa zamani wa Malawi alizuiwa kusafiri kwenda Uingereza na pasi yake ya kusafiria ikanyang'anywa baada ya kuzuka uvumi kwamba angetorokea Uingereza. Hata hivyo, aliruhusiwa kuondoka kabla ya ACB kuvamia mali zake kama dhamana endapo atashindwa kesi hiyo na hatarejea nchini humo.
Habari kutoka nchini humo zinasema ya kuwa mwanasheria wa Muluzi, Jai Banda, ameomba zoezi la kukamata mali za Rais huyo lisitishwe. Muluzi aliwahi kukamatwa huko nyuma kwa kwa kesi hiyo hiyo.
CHANZO: Raia Mwema