POMPO
JF-Expert Member
- Mar 12, 2011
- 6,690
- 2,400
WanaJF,
Ni miaka 13 toka Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere atutoke, Alizaliwa tarehe 13 Aprili, 1922. Alifariki dunia 14 Oktoba, 1999, daima atakumbukwa kuwa:
Ndiye rais wa kwanza wa Tanzania aliiongoza Tanzania toka mwaka 1961 hadi mwaka 1985.
Anakumbukwa na watanzania kuwa ndiye mwasisi wa itikadi ya ujamaa na kujitegemea.
Anakumbukwa na watanzania hasa kwa kujenga umoja na amani kwa Taifa na utamaduni wa Kiafrika pamoja na lugha ya Kiswahili, kushinda ubaguzi wa rangi, kutetea usalama wa taifa katika vitani dhidi Idi Amin.
Anakumbukwa na watanzania hasa wa hali ya chini kutokana na sera zake za kujali utu na ubinadamu.Pia ataendelea kukumbukwa na waafrika kote barani hasa kwa mchango wake mkubwa wakati wa harakati za kupigania uhuru katika nchi mbali mbali barani Afrika.
Mwalimu Nyerere ni kati ya viongozi wachache wa Afrika ambao wameacha madaraka kwa hiyari baada ya kutawala kwa muda mrefu. Alipostaafu urais mwaka 1985 alirudi kijijini kwake Butiama ambako aliendesha shughuli za kilimo.
WanaJF,najua kukutana ilishakuwa ni story,
Alikuwa na mapungufu alikuwa na mafanikio: JE TUIEZI VIPI SIKU YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA MWL. NYERERE?
Na miaka 13 Taifa bila Mwalimu Nyerere?
Ni miaka 13 toka Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere atutoke, Alizaliwa tarehe 13 Aprili, 1922. Alifariki dunia 14 Oktoba, 1999, daima atakumbukwa kuwa:
Ndiye rais wa kwanza wa Tanzania aliiongoza Tanzania toka mwaka 1961 hadi mwaka 1985.
Anakumbukwa na watanzania kuwa ndiye mwasisi wa itikadi ya ujamaa na kujitegemea.
Anakumbukwa na watanzania hasa kwa kujenga umoja na amani kwa Taifa na utamaduni wa Kiafrika pamoja na lugha ya Kiswahili, kushinda ubaguzi wa rangi, kutetea usalama wa taifa katika vitani dhidi Idi Amin.
Anakumbukwa na watanzania hasa wa hali ya chini kutokana na sera zake za kujali utu na ubinadamu.Pia ataendelea kukumbukwa na waafrika kote barani hasa kwa mchango wake mkubwa wakati wa harakati za kupigania uhuru katika nchi mbali mbali barani Afrika.
Mwalimu Nyerere ni kati ya viongozi wachache wa Afrika ambao wameacha madaraka kwa hiyari baada ya kutawala kwa muda mrefu. Alipostaafu urais mwaka 1985 alirudi kijijini kwake Butiama ambako aliendesha shughuli za kilimo.
WanaJF,najua kukutana ilishakuwa ni story,
Alikuwa na mapungufu alikuwa na mafanikio: JE TUIEZI VIPI SIKU YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA MWL. NYERERE?
Na miaka 13 Taifa bila Mwalimu Nyerere?