Tuhuma za rushwa BAVICHA zipelekwe TAKUKURU - Zitto

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Na Tumaini Makene

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Kabwe Zitto ametoa pongezi kwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vijana (BAVICHA), huku akisema kuwa atamwandikia barua katibu mkuu wake, kushauri tuhuma za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa juzi, zipelekwe mbele kwa hatua zaidi.

Akizungumza na Majira jana, Bw. Zitto alisema kuwa leo atawasilisha barua hiyo kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa, kumwomba tuhuma za rushwa zifikishwe katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ili zifanyiwe uchunguzi, kisha hatua za kisheria zichukuliwe kwa watakaobainika.


"Nafikiri nitaiwasilisha kesho hiyo barua, nitamwomba katibu mkuu hizi tuhuma zifikishwe PCCB, nafikiri hiyo itakuwa ni hatua bora zaidi, PCCB wachunguze watakaobainika na makosa wachukuliwe hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa watu wengine wote wanaojihusisha na vitendo vya namna hiyo ndani ya chama.


"Nitatumia nafasi yangu ya Naibu Katibu Mkuu. Kwa sababu tusipofanya hivyo itaweza kujenga hisia za kuwa walioondolewa katika uchaguzi huo kwa tuhuma za rushwa wameonewa. Italeta hisia za upendeleo...kwa sababu mwenye haki ya ku-determine rushwa ni mahakama hivyo ni bora wachukuliwe hatua zaidi," alisema Bw. Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini.


Akizungumzia ushindi wa Mwenyekiti wa BAVICHA, Bw. John Heche, alisema kuwa changamoto kubwa aliyonayo ni kuwaunganisha vijana wote na kuwa kiongozi wao, wakiwemo wale waliokuwa washindani wake na watu waliokuwa nyuma yao wakiwasapoti.


"Nampongeza sana Heche, kwa ushindi wake alioupata. Sasa hivi ni wakati wa kukijenga chama, uchaguzi umeisha si wakati wa kulalama tena...vijana wanamtegemea atakuwa mwenyekiti wao, mimi nafikiri moja ya changamoto zake kubwa ni pamoja na kuwaunganisha vijana, wote hata walioenguliwa," alisema Bw. Zitto.


Juzi akizungumza na Majira juu ya uchaguzi wa BAVICHA uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Slaa alisema kuwa vitendo vyote vilivyo kinyume na maadili ya kampeni kwa mujibu wa kifungu cha 10 cha katiba ya chama hicho, pamoja na waliohusika, vitajadiliwa katika ngazi ya Kamati Kuu kwa maamuzi zaidi.


Alisema kuwa baadhi ya wagombea, hasa walioenguliwa, walibainika kwenda kinyume na maadili ya chama hicho, hasa katika kupiga vita ufisadi wa aina yoyote kama vile kufanya hila katika uchaguzi, kujenga makundi yenye kuhatarisha chama na kutaka kuvuruga uchaguzi.
 
ZT acha unafiki wewe!
Kwa mtu mwenye akili za kawaida kabisa hashindwi kuona undumilakuwili uliofichika ktk hoja yako kaka. Uchaguzi umekwisha na sasa wajenge chama. Mambo ya kuita PCCB eti waje kuchunguza ili kuondoa manung'uniko tusiyape nafasi bali mpeni support Heche aunganishe wote walioshindwa na walioshinda ili Chama kisonge mbele mtu wangu! Acha uchonganishi wa hila!
 
Panapokuwa na Uchaguzi, minyukano haikosekani. Lakini kuiendeleza minyukano baada ya uchaguzi ni kutaka kuvuruga Chama tu. Sifikiri kama Zitto anayosema yanalengo la kushitaki waliotoa rushwa au kuwasafisha watuhumiwa.

Naamini atakuwa upande mmoja wapo hapo juu. Yeye kama kiongozi alitakiwa kuwashauri wagombea walioshindwa kuunganisaha nguvu kujenga chama na wala siyo kuleta utengano wa kutafuta nani katoa rushwa au vipi. Nakuomba mh. Zitto uridhike na matokeo na hao wanaonung'unika washawishi wakumbali matokeo ingawa kila iliyeingia kwenye kinyang'iro aliamini atashinda, lakini anatakiwa mmoja tu.

Naomba waeleshwe hao vijana hayo na kutumikia chama siyo lazima uwe mwenyekiti unless otherwise awe anatafuta kazi ya umwenyekiti na wala siyo cheo cha umwenyekiti.
 
Ili kukomesha hiyo Tabia na iwapo ushahidi unajitosheleza Chama moja kwa moja kupitia wanasheria wake kiwafikishe Mahakamani ila hilo lakupitia Takukuru siliafiki kwanza hii Taasisi imeoza na haiaminiki pia hawana Historia yakushinda Kesi yoyote ya Rushwa ya Mwakalebela juzi tu hapa wamechemsha sasa wa nini hawa.
 
Mvutana wa makundi mawili ndani ya chama ndio huu, kundi la akina mbowe linadaiwa kutumia rafu kumpitisha mtu wao bache ili hali kundi la akina zitto mtu wao akipigwa chini kimizengwe.

Zitto na kundi lake hawajakubali matokeo mioyoni na ndio maana anataka baraka ili liwasilishwe takukuru, lakini katibu mkuu wake amesha sema wazi matatizo yote ya uchaguzi yatajadiliwa na kamati kuu.
kazi kweli kweli
 
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Kabwe Zitto ametoa pongezi kwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vijana (BAVICHA), huku akisema kuwa atamwandikia barua katibu mkuu wake, kushauri tuhuma za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa juzi, zipelekwe mbele kwa hatua zaidi.

Akizungumza na Majira jana, Bw. Zitto alisema kuwa leo atawasilisha barua hiyo kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa, kumwomba tuhuma za rushwa zifikishwe katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ili zifanyiwe uchunguzi, kisha hatua za kisheria zichukuliwe kwa watakaobainika.

"Nampongeza sana Heche, kwa ushindi wake alioupata. Sasa hivi ni wakati wa kukijenga chama, uchaguzi umeisha si wakati wa kulalama tena...vijana wanamtegemea atakuwa mwenyekiti wao, mimi nafikiri moja ya changamoto zake kubwa ni pamoja na kuwaunganisha vijana, wote hata walioenguliwa," alisema Bw. Zitto.

Alisema kuwa baadhi ya wagombea, hasa walioenguliwa, walibainika kwenda kinyume na maadili ya chama hicho, hasa katika kupiga vita ufisadi wa aina yoyote kama vile kufanya hila katika uchaguzi, kujenga makundi yenye kuhatarisha chama na kutaka kuvuruga uchaguzi.

Acha unafiki zitto, tunaomba na wewe uangalie kwenye simu yako tarehe 3 mwezi may 2011, hii kumbukumbu namba ya MPESA uliyomtumia mmoja wa wagombea aliyeenguliwa ilikuwa ni ya nini??? Kumb namba ni hii hapa - B66FE724.

Ukiendelea nitaweka mpaka kiasi cha pesa ulichotuma. Najua ulikuwa humuungi mkono heche tangu uchaguzi wa mwaka 2009 ulioharibika. Tafadhali sana iache BAVICHA hii ya kwanza ya kitaifa ifanye kazi.
 
Mvutana wa makundi mawili ndani ya chama ndio huu, kundi la akina mbowe linadaiwa kutumia rafu kumpitisha mtu wao bache ili hali kundi la akina zitto mtu wao akipigwa chini kimizengwe.
Zitto na kundi lake hawajakubali matokeo mioyoni na ndio maana anataka baraka ili liwasilishwe takukuru, lakini katibu mkuu wake amesha sema wazi matatizo yote ya uchaguzi yatajadiliwa na kamati kuu.
kazi kweli kweli

Hakuna mtu aneyeitwa bache, nahisi wewe ni mwana ccm na unafananisha heche na hussein bashe wa uvccm.
 
Kabla ya kujadili hoja ya Zitto, tujiulize. Mwaka jana wakati Fedrick Mwakalebela anatafuta kura za maoni za kugombea Ubunge wa Iringa Mjini na alipopatwa na tuhuma za kutoa rushwa katika minyukano ya kusaka kura za maoni, Je ni CCM iliyompeleka TAKUKURU au ni TAKUKURU ndiyo iliyomdaka?

TAKUKURU kama taasisi ya kupambana na rushwa imesoma na kusikia kupita kwenye vyombo vya habari juu ya tuhuma za rushwa dhidi ya wagombea wa CDM. Wao ndio wanapaswa wawakamate wote wanaotuhumiwa na kuanza kufanyia kazi tuhuama dhidi yao. Au watuhumiwa wenyewe wajisalimishe TAKUKURU ili wakafanyiwe uchunguzi hatimae wasafishwe kama wanataka.

Si kazi ya CDM kufanya kazi ya TAKUKURU unless tukubaliane kwamba TAKUKURU yetu ni SIKIO la kufa. Haisomi magazeti wala haisikilizi Radio na TV.

Tuendelee kujadiliana!

By TUMBIRI mtoto wa NYANI.
 
ZT acha unafiki wewe!
Kwa mtu mwenye akili za kawaida kabisa hashindwi kuona undumilakuwili uliofichika ktk hoja yako kaka. Uchaguzi umekwisha na sasa wajenge chama. Mambo ya kuita PCCB eti waje kuchunguza ili kuondoa manung'uniko tusiyape nafasi bali mpeni support Heche aunganishe wote walioshindwa na walioshinda ili Chama kisonge mbele mtu wangu! Acha uchonganishi wa hila!
ni kweli kabisa kuwa ZITO anayo hiden agenda ya kutaka kuleta malumbano ndani ya chama. Haihitaji mtu kufika form four kuliona hili.
 
Ni vizuri lakini je, hao PCCB wanaaminika kwa lipi kaka Zitto? Tusije mpa mbu kazi ya kutibu maleria kaka yangu
 
Na Tumaini Makene

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Kabwe Zitto ametoa pongezi kwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vijana (BAVICHA), huku akisema kuwa atamwandikia barua katibu mkuu wake, kushauri tuhuma za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa juzi, zipelekwe mbele kwa hatua zaidi.


"Nafikiri nitaiwasilisha kesho hiyo barua, nitamwomba katibu mkuu hizi tuhuma zifikishwe PCCB, nafikiri hiyo itakuwa ni hatua bora zaidi, PCCB wachunguze watakaobainika na makosa wachukuliwe hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa watu wengine wote wanaojihusisha na vitendo vya namna hiyo ndani ya chama.

"Nitatumia nafasi yangu ya Naibu Katibu Mkuu.

I dont understand kwa nini Zitto anaongea as if hakuwepo kwenye uchaguzi. Huyu mtoto amekuwa na kasumba ya kuongea na vyombo vya habari mambo ambayo kimsingi ni Internal communications! Kama anataka kumuandikia barua kiongozi ndani ya chama chake kwa nini akasemee majira? Zitto is bad news kwa CHADEMA through & through!
 
Sounds good, mature and credits for advocacy for the rule of law. But bearing in mind this TAKUKURU that I know,the level of democracy in this country and the credibility of our judicial systems; and amid the political mitafutano going on between the ruling party (practical the owner of PCCB and the judiciary) and our dear CDM.....BIG NO!! BIG NO!!!
Kesi ya mbuzi unampelekea simba?
 
Ni hoja nzuri, lakini ukizingatia na historia ya PCCB katika miaka ya karibuni, sidhani kama hatua muafaka zitachukuliwa...
 
Msiwe na wasi wasi kuhusu TAKUKURU, ikihudumia kesi za ccm inaangalia maslahi ya aliyowateua, lakini kwa cdm hawana maslahi yoyote hivyo watatenda haki
 
Kupeleka tuhuma TAKUKURU ni kupeleka kwenye Chama Cha Magamba....Takukuru ni sehemu ya vitengo vya CCM. Zitto fikiri kwa usahihi...usirukie umaarufu ukasahau kuwa sensible. Kama kulikuwa na rushwa...CDM wachunguzane wachukuliane hatua...TUKUKURU wakitaka waingie kivyao sio kuwapelekea....kijichama kichanga hiki hata GAMBA hakina....kitakula mweleka hicho...oooh!
 
Zitto acha unafiki wewe ulisusia uchaguzi sasa baada ya uchaguzi kinakuhusu nini kwa nini usiseme walioandaa uchaguzi watayashughulikia, katibu mkuu ameshasema matatizo yote yatashughulikiwa na kamati kuu sasa wewe kama hukuridhika tangulia mahakamani au Takukuru mwenyewe au wape hela tena za mahakama kama ulivyowapa za kampeni.

Mambo ya chama kwa nini unayapeleka kwenye magazeti kwanini hiyo barua usiipeleke kwenye chama hadi utangaze magazetini, Zitto my friend tumekuvumilia sana na siasa zako za makundi karibu tutafika mwisho, uchaguzi wa Bavicha uliopita ni wewe ulisababisha kuvunjika leo wenzako wamefanikisha wakati wewe umesusa unataka tena kutuletea makundi jiangalie unakokwenda.
 
Zitto acha unafiki wewe ulisusia uchaguzi sasa baada ya uchaguzi kinakuhusu nini kwa nini usiseme walioandaa uchaguzi watayashughulikia, katibu mkuu ameshasema matatizo yote yatashughulikiwa na kamati kuu sasa wewe kama hukuridhika tangulia mahakamani au Takukuru mwenyewe au wape hela tena za mahakama kama ulivyowapa za kampeni.

Mambo ya chama kwa nini unayapeleka kwenye magazeti kwanini hiyo barua usiipeleke kwenye chama hadi utangaze magazetini, Zitto my friend tumekuvumilia sana na siasa zako za makundi karibu tutafika mwisho, uchaguzi wa Bavicha uliopita ni wewe ulisababisha kuvunjika leo wenzako wamefanikisha wakati wewe umesusa unataka tena kutuletea makundi jiangalie unakokwenda.

Zitto kama analeta uozo wa kimagamba nadhani hataweza, intelijensia ya CDM kwa sasa ni zaidi ya ile ya magamba, ZT yuko kwenye darubini tunamcheck vizuri, akithubutu tuuuuu atashughulikiwa kama alivyoshughulikiwa yule jamaa wa FIFA.CDM ni kama FIFA ya SEpp Blater.
 
Zitto kama analeta uozo wa kimagamba nadhani hataweza, intelijensia ya CDM kwa sasa ni zaidi ya ile ya magamba, ZT yuko kwenye darubini tunamcheck vizuri, akithubutu tuuuuu atashughulikiwa kama alivyoshughulikiwa yule jamaa wa FIFA.CDM ni kama FIFA ya SEpp Blater.

CDM msiwe wanafiki mwaka jana mlikuwa mnashupalia CCM walipoalila TAKUKURU katika uchaguzi wao wa ndani. Kama mpo safi kwa nini mwaogopa kuialika TAKUKURU au kwa sababu rushwa ilitolewa kama njugu kwa uwezeshaji wa mwenyekiti wa Chama HIVYO mwaona so. Kuweni na UJASIRI pelekeni maombi kwa TAKUKURU ili ukweli ujulikane, ZK mpeni pongezi kwa wazo zuri!
 
Back
Top Bottom