TUHUMA za nyumba ya Gavana wa BOT na majibu yake

Wanajamii wa JF,

Mimi huwa napenda sana kusikiliza mashairi ya huyu jamaa anayejiita 'Mjomba' au Mpoto. Kuna shairi huwa analighani kwa kusema,namnukuu,"This country Bwana is very poor", mwisho wa kunukuu. Kwamba haya maneno huwa yanasemwa na viongozi wetu tuliowapa dhamana ya kuongoza na kusimamia Taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo BOT.

Mpoto anamaanisha kwamba viongozi hawa wanawadanganya Wa-bongo kuwa nchi hii ni maskini na fukara ya kutupwa. Lakini wakti huo huo hawa viongozi wanazitumbua fedha mabilioni kwa mabilioni kwa kununulia magari ya bei mbaya na kukarabati majengo ambayo hayana thamani hata ya hayo mabilioni ya ukarabati!!

Mnashangaa ukarabati wa nyumba ya Gavana Ndulu kugharimu Tshs. Bilioni 1??? Mbona Ikulu ya JK huwa inatengewa BILIONI 5 za ukarabati kila mwaka????Nenda pale TANESCO uone kile ambacho Idrisa Rashid amefanya! TANESCO wamekarabati nyumba kwa mabilioni halafu wanataka kujiuzia kwa vimilioni kiduchu!!

Wachunguzi wa mambo na wathaminishaji wa majengo wanadai kwamba hii Bilioni 1 Tshs sawa na Pound sterling kama 500,000 ukiingia nayo katika jiji la Malkia Elizabeth pale Londoni utapata nyumba mbili za nguvu za kununua siyo kupangisha!

Hii ndiyo Tz bwana. Kila mtu akipewa nafasi ni kutafuna fedha kama mchwa kwa kwenda mbele. Nani atakuuliza bwana wewe maana huu ni ulaji unaohusisha mtandao mzima wa mafisadi wale wale wa Chama Twawala-CCM.

Hao mnaosema eti tuna Gavana Makini nawasikitikia sana. Nchi hii haina kiongozi makini hata mmoja katika eneo liwalo lote la kiuongozi. Tutaendelea kushuhudia uoza huohuo ulifanyika wakti wa marehemu Balali na kina Liumba!

Ni wizi mtupu!!!!!

Narudia tena kauli yangu kuwa nchi hii imelaaniwa!
 
Tatizo lenu ni umasikini mlio nao wa kutokujua na kutokufahamu. Hiyo nyumba siyo ya Beno Ndulu binafsi. Ni nyumba ya Gavana wa BOT ambaye kwa sasa ni Beno Ndulu. Akija mwingine ataingia. Ukarabati huo umefanyika kufuatana na bajeti iliyopitishwa sasa mnalalamika na kushangaa nini. Hiyo Bilioni 1? Kama iko ndani ya bajeti iliyopitishwa so be it. A billion figure is just a relative figure. Kama huna waiona nyingi na kama unazo kama vile BOT it is just an expendable item.

Of course ukilinganisha na nyumba yako binafsi ndiyo unahisi kuna ufisadi. Lakini haya majumba yote ya serikali ya mashirika ya umma yanajengwa through tendering process na wanapewa contaractors. Hapo ndipo gharama zinakuwa kubwa. Kwa sababu kuna Main Contractor, Consulting Engineer, Electrical Consultant, Quantity Surveyor na kadhalika. Wote hawa wanatakiwa kulipwa professional fees kufuatana na sheria ya nchi. Sasa ukayajumlisha haya pamoja na gharama za vifaa vya ujenzi utakuta hiyo bilioni moja na kajisenti tu.

Kwa hiyo acheni ushabiki wa watu wasioenda shule.
 
Khaaa! yaani hiyo ndio nyumba iliyogharimu bilioni 1 kukarabati? Stupid


ningependa kujua hasa kilichokarabatiwa ni nini na kabla ya hapo nyumba ilikuwaje? usije kukuta wamebadilisha vitasa vya Tanzania na kuweka vya Uarabuni, madirisha ya misonobari na kuweka ya mivunge; huku wakibadilisha mapazia na mazuria.. ..
 
attachment.php
 

Attachments

  • NYUMBA- UPANDE WA MBELE[1].JPG
    NYUMBA- UPANDE WA MBELE[1].JPG
    44.7 KB · Views: 206
Lakini haya majumba yote ya serikali ya mashirika ya umma yanajengwa through tendering process na wanapewa contaractors. Hapo ndipo gharama zinakuwa kubwa. Kwa sababu kuna Main Contractor, Consulting Engineer, Electrical Consultant, Quantity Surveyor na kadhalika. Wote hawa wanatakiwa kulipwa professional fees kufuatana na sheria ya nchi. Sasa ukayajumlisha haya pamoja na gharama za vifaa vya ujenzi utakuta hiyo bilioni moja na kajisenti tu.

Kwa hiyo acheni ushabiki wa watu wasioenda shule.

We Marigwe wewe!

Hivi Gavana Benno Ndulu ni mjomba wako au na wewe ni mfanyakazi wa BOT? Mbona unaanza kutetea ufisadi ulio wazi kabisa?Unataka kutuambia kuwa wale wote wanaopinga ufisadi nchi hii hawajaenda shule kweli??? Hebu uwe mpole usitake kutuchefua kwenye forum hii!

Hizi Professional au Consultation Fees za Contractors ni kiasi gani kwa kila mmoja? Remember this is just a RENNOVATION NOT A NEW CONSTRUCTION! Hii bilioni moja inatosha kujenga nyumba nyingine mbili mpya za Gavana!

Hapa bwana hakuna cha Consultation Fees isipokuwa ni 10% za wazee wanaoingia kwenye mchakato wa Tendering Board. Watu tu mashahidi tumeona Contractor anaanza kujenga jengo la Serikali na by the time anamaliza hiyo project na yeye anamaliza nyumba yake au yake inaisha na jengo la serikali linasimama!!!.

Hata hivo kauli zako zinaonyesha harufu ya ufisadi. Unaposema eti Bilioni 1 ni kama kajisenti tu kwa BOT nakumbuka ile kauli ya Mhe. Chenge aliyodai kuwa bilioni 2 alizokutwa nazo kwenye offshore accounts huko nje ilikuwa ni vijisenti tu!!!

Kwa hiyo Marigwe acha hizo.
 
Nyumba hiyo tu ndo imegharimu Bilioni 1? Je manunuzi si tutaambiwa imegharimu .... kweli sisi wehu
 
Na akistaafu atajiuzia ili iwe mali yake, enhe si ndio!! Poa Kuleni tu bwana!!
 
Wewe nyumba unayoishi imekugharimu kiasi gani? Chukua hicho kiasi hakafu ugawe kwa milioni 1000! ndo ujue kama ni gharama au la!!
one billion kwa rennovation ni pesa ndogo tu!HIVI NINYI HAMJUI KWAMBA NYUMBA HII NI FULL-FURNISHED?tatizo lenu sio prefessionals!

kuna nyumba hapo usalama-wa-taifa ya mfanya biashara maarufu hapa mjini nikiwaambia gharama zake si mtachanganyikiwa?tena sio full-furnished.....!

ongeeni kitaalamu jamani
 
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]
brentst664.jpg
[/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Hendon[/FONT]

Price: [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]£299,500 Freehold [/FONT][FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]3 Bedrooms[/FONT][FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]2 Reception[/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]We are pleased to offer for sale this well presented refurbished extended 3 bedroom terraced house, The property has to offer two reception rooms, three bedrooms, family bathroom, en-suite shower room, guest WC, kitchen, utility room, front and rear garden. It lies close to Hendon Mainline station (Thames link) and is offered with the benefit of immediate vacant possession.[/FONT]


Haya hii nyumba tena yenye ghorofa moja iko mtaa wa Hendon kule Uingereza inauzwa Pounds 299,500 sawa na Tshs. 600 million.

Linganisha nyumba hii yenye ghorofa iliyoko London na hii nyumba yenye kighorofa uchwara ya Gavana Benno Ndulu na tofauti ya bei ya kununulia nyumba London na bei ya ukarabati Dsm halafu ujiulize kama kweli hapa kuna uhalali wa pesa inavotumika ndani ya nchi hii. Pambaf!
 
Hiyo nyumba ni mbovu, nimechoka mwenyewe sijui walikarabati nini maana hiyo lawn yenyewe imekaa kiupande upande tuu.


Hakuna standards TZ kila mtu anajiwekea stds zake. Nilishangaa kuona nyumba ya ghorofa mbili inauzwa USD 2 million Kigamboni wakati viwanja vya jirani vinauzwa million 14.

Hata wewe kajumba kako ka Tshs million 20 unaweza kukauza 100 million na watu wasistuke.
 
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]
brentst664.jpg
[/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Hendon[/FONT]

Price: [FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]£299,500 Freehold [/FONT][FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]3 Bedrooms[/FONT][FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]2 Reception[/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]We are pleased to offer for sale this well presented refurbished extended 3 bedroom terraced house, The property has to offer two reception rooms, three bedrooms, family bathroom, en-suite shower room, guest WC, kitchen, utility room, front and rear garden. It lies close to Hendon Mainline station (Thames link) and is offered with the benefit of immediate vacant possession.[/FONT]


Haya hii nyumba tena yenye ghorofa moja iko mtaa wa Hendon kule Uingereza inauzwa Pounds 299,500 sawa na Tshs. 6 million.

Linganisha nyumba hii yenye ghorofa iliyoko London na hii nyumba isiyo hata na ghorofa ya Gavana Benno Ndulu na tofauti ya bei halafu ujiulize kama kweli hapa kuna uhalali wa pesa inavotumika ndani ya nchi hii. Pambaf!
SASA wewe unalinganisha na nyumba za marine plywoods?
 
Masahihisho hiyo bilioni moja imetumika kufanyia ukarabati, nyumba ilinunuliwa kwa dollar 400,000. Walichokarabati ni nini hasa?
gharama ya ile nyumba nia FINISHING!
unajua bei za tiles,marbles na kuifurnish nyumba kwa vitu ambavyo wamevioutsource america?
 
kwa nini wamevioutsource America?
mkuu,
ninavyoielewa mimi serikali!LAZIMA WAMEIMPORT MATERIALS KIBAO kutoka ulaya na amerika

kulijibu swali lako mkuu wangu ni labda wamezingatia ubora!

au ulitaka waweke PORCELAIN FLOOR TILES ZA UCHINA AMBAZO NI KAMA 30,000/= KWA SQUARE METRE?

ai mini kuna vitu vingi sana vya finishing ndivyo vilivyokula hela,kuanzia floor,wall ceiling roofing,external works pia naona kama imekula sana hela,

sasa ukija kwenye kui-furnish,hapo lazima mil 150-200 ilidondoka
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom