Huku akijiamini na kuamini kuwa aliyokuwa akiyasema ni kweli na ukweli tupu, Mh. Tundu Lissu alitoa tuhuma nzito dhidi ya Mh. RAIS, WAHESHIMIWA MAJAJI, na MAAFISA WA SERIKALI.
Nimefanikiwa kusoma taarifa ya Mh. Lissu (MB): MAONI YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA KATIBA NA SHERIA, MH. TUNDU A.M. LISSU (MB.) KUHUSU MPANGO NA MI YA FEDHA YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KWA MWAKA 2012/2013.
Katika ukurasa wa 9, Mh. Lissu anasema:
Kwa mujibu wa taarifa tulizonazo, sasa watu wanateuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ambao hawajawahi kupendekeza na Tume Tume ya Utumishi wa Mahakama na- kwa sababu hiyo- hawajafanyiwa vetting yoyote na mamlaka hiyo ya kikatiba juu ya uwezo na ukjuzi wao kama wanafaa kwa kila hali kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu. Inaelekea watu hao- wengi wao wakiwa wamekaribia muda wao wa kustaafu kwingineko katika utumishi wa umma- wanapewa ZAWADI YA UJAJI ili kuwawezesha kupata mafao ya Majaji wastaafu ambayo yameboreshwa sana katika miaka ya karibuni.
Tuhuma za Mh. Lissu zinaibua maswali kadhaa kuhusu mustakabali wa taifa letu:
Kwa bahati mbaya, watu wengi wanaamini kuwa Mh. Lissu ni Mwanasheria bora kuliko wanasheria wote katika Jamhuri ya Muungano. WAtanxzania wengi wanaamini chochote kinachosemwa na viongozi kama Mh. Lissu ni sahihi na kweli tupu.
Kwa bahati mbaya, hata Magazeti yalimnukuu huyu Mbunge bila kunukuu yaliyosemwa na wabunge wengine kuhusu tuhuma alizotoa Mh. Lissu.
Je ni kitu gani kimeyazuia Magazeti kufanya uchunguzi wa kina na kubaini ukwel ;i kuhusu uteuzi wa Majaji ? Je uwezo wa magazeti na waandishi wa habari kufanya uchunguzi wao wa kina umepotea hapa Tanzania ?
MHESHIMIWA SPIKA. Tuhuma dhidi ya Rais, Mahakama na maafisa kadhaa wa Umma zilitolewa ndani ya Bunge lako. Mh. Lissu anajua kuwa kama angetoa hizo tuhuma nje ya Bunge walioguswa na tuhuma hizo wangefuata utaratibu wa Kisheria kurudisha heshima yao mbele ya jamii.
Ili kulinda utawala wa sheria na heshima ya Bunge, ili kulinda heshima ya Mahakama na pia heshima ya Rais na ili kulinda heshima ya watumishi wa umma waliotuhumiwa bila ya wao kujitetea: ninakuomba Mh. Spika uamuru uchunguzi wa kina ufanywe ili kujua ukweli wa mambo.
KWA KUWA MH. ALITOA TUHUM ZAKE MBELE Y WATU WOTE WALIOKUWA WAKIANGALIA RUNINGA, NINAOMBA KUWA WAKATI WA UCHUNGUZI HUO SISI WANANCHI TURUHUSIWE KUHUDHURIA ILI HUO USHAHIDI WA MH. LISSU TUUONE BILA KUSUBIRI KUAMBIWA.
Nimefanikiwa kusoma taarifa ya Mh. Lissu (MB): MAONI YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA KATIBA NA SHERIA, MH. TUNDU A.M. LISSU (MB.) KUHUSU MPANGO NA MI YA FEDHA YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KWA MWAKA 2012/2013.
Katika ukurasa wa 9, Mh. Lissu anasema:
Kwa mujibu wa taarifa tulizonazo, sasa watu wanateuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ambao hawajawahi kupendekeza na Tume Tume ya Utumishi wa Mahakama na- kwa sababu hiyo- hawajafanyiwa vetting yoyote na mamlaka hiyo ya kikatiba juu ya uwezo na ukjuzi wao kama wanafaa kwa kila hali kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu. Inaelekea watu hao- wengi wao wakiwa wamekaribia muda wao wa kustaafu kwingineko katika utumishi wa umma- wanapewa ZAWADI YA UJAJI ili kuwawezesha kupata mafao ya Majaji wastaafu ambayo yameboreshwa sana katika miaka ya karibuni.
Tuhuma za Mh. Lissu zinaibua maswali kadhaa kuhusu mustakabali wa taifa letu:
- Ni kweli MAJAJI WETU wanateuliwa na Mh. RAIS bila kupata mapendekezo ya Tume ya Utumishi wa Mahakama?
- Ujaji nchini Tanzania ni zawadi?
- Je Mbunge anajiridhisha kwanza na usahihi wa taarifa anazopokea kabla ya kuzitamka BUNGENI KAMA UKWELI?
- Hatua gani zichukuliwe dhidi ya Mbunge anayetumia uhuru wa mbunge kuongea bungeni kwa kutoa TUHUMA ZA UONGO NA ZINAZOPOTOSHA dhidi ya Mihimili mingine ya Dola ?
- JE Chama Rasmi cha Upinzani Bungeni kilipata nafasi ya kuijadili hotuba ya Mh. Lissu na kuibariki isomwe Bungeni PAMOJA NA TUHUMA? Au ILIKUWA ni hotuba Binafsi ya Mh. Lissu ambayo haikupitia katika mfumo wa kimajadiliano na kimaamuzi (shadow cabinet) ndani ya kambi ya upinzani?
- Je wanachama binafsi ndani vya vyama ni bora kuliko uamuzi wa chama?
- Je Chama Rasmi cha Upinzani kina uwezo wa kuwadhibiti baadhi ya wanachama wao ambao ni « el-maarufu »?
Kwa bahati mbaya, watu wengi wanaamini kuwa Mh. Lissu ni Mwanasheria bora kuliko wanasheria wote katika Jamhuri ya Muungano. WAtanxzania wengi wanaamini chochote kinachosemwa na viongozi kama Mh. Lissu ni sahihi na kweli tupu.
Kwa bahati mbaya, hata Magazeti yalimnukuu huyu Mbunge bila kunukuu yaliyosemwa na wabunge wengine kuhusu tuhuma alizotoa Mh. Lissu.
Je ni kitu gani kimeyazuia Magazeti kufanya uchunguzi wa kina na kubaini ukwel ;i kuhusu uteuzi wa Majaji ? Je uwezo wa magazeti na waandishi wa habari kufanya uchunguzi wao wa kina umepotea hapa Tanzania ?
MHESHIMIWA SPIKA. Tuhuma dhidi ya Rais, Mahakama na maafisa kadhaa wa Umma zilitolewa ndani ya Bunge lako. Mh. Lissu anajua kuwa kama angetoa hizo tuhuma nje ya Bunge walioguswa na tuhuma hizo wangefuata utaratibu wa Kisheria kurudisha heshima yao mbele ya jamii.
Ili kulinda utawala wa sheria na heshima ya Bunge, ili kulinda heshima ya Mahakama na pia heshima ya Rais na ili kulinda heshima ya watumishi wa umma waliotuhumiwa bila ya wao kujitetea: ninakuomba Mh. Spika uamuru uchunguzi wa kina ufanywe ili kujua ukweli wa mambo.
KWA KUWA MH. ALITOA TUHUM ZAKE MBELE Y WATU WOTE WALIOKUWA WAKIANGALIA RUNINGA, NINAOMBA KUWA WAKATI WA UCHUNGUZI HUO SISI WANANCHI TURUHUSIWE KUHUDHURIA ILI HUO USHAHIDI WA MH. LISSU TUUONE BILA KUSUBIRI KUAMBIWA.