Tuhuma za kuuawa Dr Mwakyembe na Mawaziri wenzake vp?

Mafie PM

JF-Expert Member
Mar 19, 2011
1,317
207
Baadhi yetu tulisoma na kuisikia ripoti ya Dr Mwakyembe kuwa kundi la Al-shabab toka Somalia likishirikiana na Wahalifu sugu wa hapa kwetu Tanzania, limekodiwa na baadhi ya wanasiasa kwa ajili ya kuwaua baadhi ya viongozi hapa nchini kama Dr Slaa, Prof Mwandosya, Anne Kilango, Bernad Membe na Mfanyabiashara maarufu Reginald Mengi pamoja na yeye mwenyewe Dr Harison Mwakyembe، zile ni tuhuma nzito sana maana ziligusa Serikali, Uhamiaji, Polisi, Usalama wa Taifa,viongozi wa serikali, watu binafsi na rasilimali za Taifa,

Je? Serikali inayotawala na vyombo vyake waliamua kumpigia magoti baada ya kuona mpango wao umevujishwa?
Walifanya nini wakati watuhumiwa wanajulikana majina yao na walipokuwapo hapa nchini pamoja na wenyeji wao? Je kwa
hali hii haitaonekana serikali iko likizo na haina Mtawala?

Serikali isingepaswa itoe tamko kama ni kweli au ni uzushi ili aliyetoa uzushi akamatwe kwa kuhatarisha usalama wa Taifa? Hii inadhihirisha ndani ya serikali kila mtu ana jeshi lake na usalama wake wa Taifa! Hili halina ubishi. Ufalme umegawanyika tayari:
Nataka mchango wenu Great thinkers maana najua mnajua mambo mengi pia:
 
binafsi nakubaliana na wewe kabisa, serikali yetu kusema ukweli imeenda likizo, ingawa ukiuuliza sasa watasema intelegensia haijamaliza kazi yake. majina yalitajwa yaani ule ulikuwa ni uchunguzi kamili kabisa ambao ulitakiwa kufanyiwa kazi moja kwa moja. lakini kwa kuwa serikali imeguswa wanasema waacha bora liende. Tuzidi kuomba Mungu hawa ibilisi wasitimize adhma yao hiyo.
 
Hasa shemeji nae jeshi la polisi limemshinda anabakia kula mwisho mwisho maana sidhani kama atadumu zaidi ataijuaa na wake anaoa kila kukicha
 
ndugu zangu mnataka vyombo vya usalama viwe vinatoa taarifa kuwa leo tunaenda kupeleleza vingunguti, na kesho tunaenda kupeleleza kyela kwa mwakyembe, tusubili tuwe na subila selikali yetu itafanya vile inavyotakiwa ifanye. kama ni ulinzi inawezekana wameongezewa kuliko kawaida ila kwakuwa hawajatangaza ndiyo maana hatujui. tusubiri tuone serikali itakavyo fanya. ukiona mmojawao kauwawa ndiyo tusema nyie mlipewa taarifa hamkuzifanyia kazi.
tuwe na subira! nawapenda sana viongozi hao, naipenda serikali ya Tanzania bila kujali inaongozwa na nani kwakuwa hata nikiichukia nitakuwa najiumiza mwenyewe yenyewe ipo tu!.
 
Nyie mnachekesha kweli yani serikali yetu inashidwa kunifikishia ka barua tuu toka kilomita 10 bila kupotea mara kadhaa unazani wanaweza kupanga na hao magaidi na wawalipe! Wakati magereza yetu yamejaa majambazi sugu wauwa watu ambao wanaweza watumia bure tuuu, kama wangetaka Slaa afe ange kufa siku nyingi. Siasa ni mchezo sisi watazamaji mwishowe wanasema timu bora hushinda waonge, watumia maarifa na ujuzi. Matokeo ndo yanasema mshindi. Nyie hamjiulizi Mrema aliishia wapi alibwabwaja wee halafu akaja lipumba na yeye akabwabwaja na kupayuka payuka wakati akila na wana magamba na siye tukiishiwa kupigwa na polisi kwa vivurugu hewa hatuna hata kadi ya unachama. Sasa leo yupo Slaa naye anabwabwaja tuu bure bure ala hotelini siye mlo mmoja juani wee acha tu.
 
Back
Top Bottom