Mtanzania, Jumamosi Novemba 14, 2009
Aliyewakashifu Mkapa, Mwinyi adhaminiwa
Na Evaline Shayo, TSJ
MKAZI wa Arusha, Anney Anney, anayetuhumiwa kuwakashifu marais Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, amepata dhamana.
Anney, ambaye ni mlemavu wa miguu, alifikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Ilala Julai 23, mwaka huu, kwa tuhuma za kuwakashifu marais hao. Dhamana ilikuwa wazi, lakini hakupata wadhamini.
Mwendesha Mashataka, Daniel Juma, mbele ya Hakimu Samwel Maweda, alidai kwamba mtuhumiwa huyo aliwakashifu Mwinyi na Mkapa, huku akimsifia Mwalimu Julius Nyerere.
"Mwinyi aliua Azimio la Arusha, Mkapa aliuza mashirika yetu na nyumba za umma. Wewe unauza ardhi yetu kwa Wazungu na Waarabu pamoja na utu na utaifa wetu. Nyerere alilinda ardhi yetu, utaifa na uzalendo, udumu ujamaa na kujitegemea, lidumu Azimio la Arusha, zidumu fikra za Mwalimu Nyerere." anadaiwa alisema mtuhumiwa huyo.
Mtuhumiwa huyo yuko nje kwa dhamana hadi Novemba 19, mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa tena.
Aliyewakashifu Mkapa, Mwinyi adhaminiwa
Na Evaline Shayo, TSJ
MKAZI wa Arusha, Anney Anney, anayetuhumiwa kuwakashifu marais Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, amepata dhamana.
Anney, ambaye ni mlemavu wa miguu, alifikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Ilala Julai 23, mwaka huu, kwa tuhuma za kuwakashifu marais hao. Dhamana ilikuwa wazi, lakini hakupata wadhamini.
Mwendesha Mashataka, Daniel Juma, mbele ya Hakimu Samwel Maweda, alidai kwamba mtuhumiwa huyo aliwakashifu Mwinyi na Mkapa, huku akimsifia Mwalimu Julius Nyerere.
"Mwinyi aliua Azimio la Arusha, Mkapa aliuza mashirika yetu na nyumba za umma. Wewe unauza ardhi yetu kwa Wazungu na Waarabu pamoja na utu na utaifa wetu. Nyerere alilinda ardhi yetu, utaifa na uzalendo, udumu ujamaa na kujitegemea, lidumu Azimio la Arusha, zidumu fikra za Mwalimu Nyerere." anadaiwa alisema mtuhumiwa huyo.
Mtuhumiwa huyo yuko nje kwa dhamana hadi Novemba 19, mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa tena.