akilimtindi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2008
- 421
- 83
Kwa haya yote yaliyotokea tangu jana sidhani kama kuna mwenye furaha ya kweli moyoni mwake leo, labda watu kama Maige, Nundu, Maige, Ngeleja na wengineo ambao waliponea tundu la simba siku ya jana. Kwa wengine wote wenye uchungu na Taifa hili naamini leo hawana raha kabisa na kwa vyovyote watataka kujua nini cha kufanya ili sasa tuone mabadiliko ambayo tumekuwa tukiyasubiri kwa siku zote.
Nashauri tukubaliane kwa nia njema kabisa kugoma kwa kukaa majumbani mwetu siku ya Ijumaa tarehe 28/04/2012 ili kuishinikiza serikali kufanya mabadiliko ya kweli. Hii haitotupa shida kubwa maana hatutakuwa na wasiwasi wa kupata virungu vya polisi ambavyo najua wengi wetu tunaviogopa ingawa kweli hasira tunazo za kiwangi fulani. Tununue vyakula na mahitaji mengine ya muhimu kuanzia leo na hii tutaitumia kama akiba wakati tunaishinikiza serikali kufanya tunachotaka. Wiki ijayo nadhani wataanza mchakato wa kukusanya maoni kuhusu katiba na hii wataipa publicity kubwa kujaribu kufunika hii hali iliyopo, let's igore the Katiba thing kwa sasa maana haina maana kwetu kwa hali.
Mwisho nimeshauri tugome au tuandamane kwa maana ya kwamba kama Hasira zinatosha basi tuandamane, tuna uwezo huo na tunaweza kabisa kuandamana. Lengo liko pale pale kwamba tunataka serikali ifanye mabadiliko ya kweli sio kuipindua serikali. Hiyo ni kazi ndogo sana kama tukiamua na ukweli ni kwamba serikali yetu ni dhaifu sana kuanzia juu hadi chini, hata hao polisi wanaoringa nao hawapo wa kutosha kabisa kwahiyo tuache woga kabisa kama tupo tayari tuandamane. Tukiona ngumu tugome kwa kunyamaza kimya maana hata sisi tunaweza kunyamaza kwa kuacha kila kitu kwa kusema huu ni upepo tu...!
Nashauri tukubaliane kwa nia njema kabisa kugoma kwa kukaa majumbani mwetu siku ya Ijumaa tarehe 28/04/2012 ili kuishinikiza serikali kufanya mabadiliko ya kweli. Hii haitotupa shida kubwa maana hatutakuwa na wasiwasi wa kupata virungu vya polisi ambavyo najua wengi wetu tunaviogopa ingawa kweli hasira tunazo za kiwangi fulani. Tununue vyakula na mahitaji mengine ya muhimu kuanzia leo na hii tutaitumia kama akiba wakati tunaishinikiza serikali kufanya tunachotaka. Wiki ijayo nadhani wataanza mchakato wa kukusanya maoni kuhusu katiba na hii wataipa publicity kubwa kujaribu kufunika hii hali iliyopo, let's igore the Katiba thing kwa sasa maana haina maana kwetu kwa hali.
Mwisho nimeshauri tugome au tuandamane kwa maana ya kwamba kama Hasira zinatosha basi tuandamane, tuna uwezo huo na tunaweza kabisa kuandamana. Lengo liko pale pale kwamba tunataka serikali ifanye mabadiliko ya kweli sio kuipindua serikali. Hiyo ni kazi ndogo sana kama tukiamua na ukweli ni kwamba serikali yetu ni dhaifu sana kuanzia juu hadi chini, hata hao polisi wanaoringa nao hawapo wa kutosha kabisa kwahiyo tuache woga kabisa kama tupo tayari tuandamane. Tukiona ngumu tugome kwa kunyamaza kimya maana hata sisi tunaweza kunyamaza kwa kuacha kila kitu kwa kusema huu ni upepo tu...!