fikirini
Senior Member
- May 24, 2011
- 114
- 22
Nikiwa mgeni kabisa katika safu hii ya jamii forum yenye kutoa fursa ya fikra pevu na zisizo za woga. leo naomba tufikirie pamoja nanyi katika hili! mapema wiki hii vyombo vya habari viliripoti na kuonesha hali ya hatari ya majengo na mitaro inayozunguka kampasi ya chuo kikuu cha Dodoma. uwepo wa nyufa katika majengo wanapolala watanzania na wasomi wenzetu ni hali hatarishi kwa rasilimali ya taifa. kuna vyuo kama udsm, sokoine ambavyo vimejengwa miongo mingi iliyopita lakini hadi sasa hakuna nyufa za ajabu kulinganisha na umri wa majengo hayo. kuna nini udom? kuanzishwa kwa udom kwa mbwembwe na majigambo ya viongozi wetu wa kitaifa ilikuwa ni jambo la dharula? Hatuna wakandarasi weledi ambao wangeweza kufanya kazi yenye tija? au ujenzi huu wa chuo kikubwa kama hicho ni mradi wa kumnufaisha mtu mmoja? na je si fedha za walipakodi wa nchi hii?. Hebu ndugu zangu naombeni mawazo yenu katika hili.
Ni mimi Fikirini
Ni mimi Fikirini