Wanajamii tufanye nini ili tuweze kupata taarifa za kila siku toka majimbo mbalimbali za uchaguzi.
Nakaribisha mapendekezo mbalimbali ili hili lifanikiwe.
Karibuni sana.
Ahsante mkuu,Inaonekana ujumbe haujaeleweka kwa baadhi yetu: Ujumbe wako una maana kwamba tufanye nini ili tupate taarifa za kila siku toka majimboni kwa muda uliobaki kuanzia leo hadi 30/10/2010.
Maoni
- Ni vema tukawa na coordinators wa taarifa kwa kila jimbo atakayetoa kwa ufupi yaliyojiri jimboni kwenda JF on daily basis.
- iNABIDI mANAGEMENT YA jf IWAPE CODE wale coordinators ili wa-route taarifa huko kabla ya kufika jamvini
- JF management ifanye summing up ya hizo taarifa na kuzipost to the general JF jamvi for daily consumption
- summary ya taarifa iwe fupi sana isijekutuchosha kusoma ila isibadilishwe it should reflect the actual situation occured in the field
Nilichomaanisha ni namna ya kupata habari za kampeni toka majimboni kila siku kuanzia sasa. Kama tunaweza kupata wawakilishi watakaotujulisha yanayojiri kila siku majimboni ni vizuri zaidi.NEC wameahidi kuwa matokeo yatakuwa yanatumwa kwenye mtandao wao mara wayapatapo na ndiyo maana wameahidi kumtangaza mshindi wa Uraisi katika siku tatu.
Kwa hiyo tukienda huko tutajionea kama ahadi hizi wamezitekeleza wenyewe NEC au ni braa-braa zao tu...........................
CHADEMA (Na vyama vingine) waweke Monitors (watu) katika ngazi ya kila Jimbo la uchaguzi. Hao Monitors wawe na orodha ya vituo vyote vya kupigia kura halafu wawe na watu ambao watavizungukia vituo na kuchukua matokeo na kutoa taarifa kwa Monitor wa Jimbo. Alternatively, mawakala wawezeshwe kwa kupewa simu (kama hawana) na muda wa maongezi ili wawe wanatoa taarifa kwa Monitor, hata kwa sms, kadiri upigaji kura unavyoendelea. Matokeo ya jimbo yakiishatangazwa Monitor anatuma mara moja makao makuu ya chama. Na chama kinatundika matokeo kwenye website yake instantly. Ni kiasi cha kujipanga na kujitolea. WanaJF wenye ujuzi wa IT mnaonaje mkijitolea kufanya kazi hiyo siku ya siku?