Tufanye jee kurudisha hadhi ya kiume?

Hahaha. . Hygea sio nyie wanaume ndo mnapenda kulalia nyama choma na bia alafu wali wa samaki nyumbani mnaona sio kitu? Binafsi nasikitika sana kuona watu wanakimbia vyakula vizuri na fresh vyote tulivyobahatika kuwa navyo alafu wanajaza vitu visivyo vizuri sana kwa afya ya mwili. Yani mimi ningeweza ningekua nakula mboga za majani asubuhi, mchana na jioni. Kitu ambacho wengi hawataki, wao ni nyama, nyama, nyama tuu basi.

Nyie wanaume nanyi kuweni responsible. . .
Kama tatizo ni chakula cha nyumbani hakinogi basi ongea na mkeo aboreshe mapishi yake, omba upikiwe vyakula (vya maana) upendavyo na ujitahidi kuwa hata unatembea kidogo mida ya jioni. Unaweza ukafanya iwe family activity, mama na watoto wote mnaungana. Kama mna kauwanja kenu chezeni hata mpira na watoto wenu.

Sema hayo hapo juu yanahusu yu iwapo wewe ni mtu wa familia, kama hupendi kutumia muda na familia yako endelea tu kujaza nyama/ndizi kavu na ngumu pia machips yaliyojaa mafuta tumboni day in day out. Matokeo yake utayaona soon enough.

Hehehe ndio na somo linahusu, yale nayo ni mazoezi!!

Kimsingi nakubaliana na uliyoongea. Ila na haya mafriji yenu ya siku hizi watu wanalishwa viporo kwa kwenda mbele tu hata majumbani. Wali, maharage, mboga zinapikwa zinakaa wiki nzima kinachofanyika ni kupasha moto tu. Mimi binafsi sioni ubaya wa nyama choma ikiliwa responsibly. Nimekulia kijijini ambapo nyama choma ilikuwa ikiliwa na haikuwahi kuwa sababu ya haya matatizo ya wanaume wa kisasa.

Hilo la kuwaambia kina mama waboreshe mapishi ni "easier said than done". Sio kinamama wote mkiambiwa mboreshe mapishi mnaweza kuelewa kiurahisi. Nakuhakikishia hilo linaweza kuwa chanzo cha mgogoro na unaweza kuambatana na vikwazo vingine kama kununa na usitishwaji wa huduma kuu ya ndoa.
 
Jamani hata mambo ya kitambi yanahitaji hekima ya mke, ina maana wewe mwanaume hujui baya na zuri lipi?!

Btw, nimesema hapo juu bwanyenye hataweza kukaa kwenye mji wetu mana atakula zoezi/gym na kuzingatia diet yanguvu home.
Sijampata huyo mume ila hawezi kuwa bonge bonge hivyo..




Nimekosa cha kusema mana umenichekesha. Uwepo wa vitendea kazi siyo issue, magonjwa na usanii umejaa siku hizi. Ni vyema kuwa mwangalifu hata kama ina raha yake vipi. Kwa awamu hii ya Jakaya mzigo umeshafunguliwa:)) ha ha

Hili la ama mume kuwa bonge au la subiri muda ukifika utapata majibu. Na wakijua unataka wanaume vipotable wataingia gym mapema kwa lengo la kukupata. Akikupata tu anakumbuka "my dear bottle" na remote kama kawaida. Hivi ulishawahi kujiuliza mme wako akishakuoa kisha akagoma kufanya mazoezi na akaanza kuwa bonge utamfanyaje? Je utamshurutisha afanye mazoezi? akikataa? ......
 
Hili la ama mume kuwa bonge au la subiri muda ukifika utapata majibu. Na wakijua unataka wanaume vipotable wataingia gym mapema kwa lengo la kukupata. Akikupata tu anakumbuka "my dear bottle" na remote kama kawaida. Hivi ulishawahi kujiuliza mme wako akishakuoa kisha akagoma kufanya mazoezi na akaanza kuwa bonge utamfanyaje? Je utamshurutisha afanye mazoezi? akikataa? ......

Ni kweli mambo mengine majaliwa. Ila nitamhimiza kuhusu afya bora halafu najua kitu kingine watu hatufuatilii afya zetu sana, ndyo mana magonjwa mengine yanajulikana too late..huo unene ukiacha kazi tunayoingelea hapa una madhara mengine makubwa, kama mtu unaweza kuuzuia ni vyema..Kweli mimi na mwanaume bonge hatuwezani, atawork out body lake!
 
Ni kweli mambo mengine majaliwa. Ila nitamhimiza kuhusu afya bora halafu najua kitu kingine watu hatufuatilii afya zetu sana, ndyo mana magonjwa mengine yanajulikana too late..huo unene ukiacha kazi tunayoingelea hapa una madhara mengine makubwa, kama mtu unaweza kuuzuia ni vyema..Kweli mimi na mwanaume bonge hatuwezani, atawork out body lake!

Wakati mwingine naufananisha unene na uvutaji wa sigara au ulevi wa pombe. Siyo kwamba wavuta sigara au walevi wa pombe hawajui madhara ya sigara au pombe tena ukiwauliza watakueleza vyema tu madhara yake. Tatizo kwa watu wengi ni jinsi gani ya kuacha sigara au pombe. Watu wanene hivyo hivyo. Siyo kwamba hawajui madhara ya unene na matatizo yanayotokana na unene kwani wengi wao ni wasomi na wengine ni madaktari wa kutibu binadamu kabisa. Suala ni maamuzi magumu ya kuamka alfajiri au kutoka ofisini jioni kwenda kufanya mazoezi na kupunguza/kuachana kabisa na vyakula/vinywaji wanavyovipenda. Wengi mpaka waambiwe na daktari kuwa wana matatizo ya kiafya na ili wapone inabidi waanze mazoezi na kuacha vyakula/vinyaji filani ndio wanasikia.
 
Back
Top Bottom