Tuepuke sumu hizi: Brigedia Jenerali mstaafu Francis Mbena

Mzee Said Mohammed

Nakuomba mzee wangu uendelee kuwa mvumilivu wakati unatoa darasa humu. Kwa sababu Sifa kubwa ya watu humu ni ubishi na kutotaka kusoma au kujifunza hata unapowapa reference wakasome, huo ni ugonjwa wa waTanzania wengi.

Kwa hiyo unajadiliana na mtu ambaye ameshaamua kuwa mbishi tu hapo kunakuwa na changamoto nyingi sana. Ndio maana wengine wanasema "mdini" wengine "mchochezi" etc.

Lakini Mungu akupe uvumilivu mzee wangu.

Mungu hawezi kumpa uvumilivu Mdini kama huyu,Huyu anastahili kulaaniwa tu kutokana na Uchochezi wake wa kidini.
 
Bado upo na story zako za udini? kazi kweeli! utabaki huko huko hadi kiama chako!
Pilipili,
Kitabu changu kinakwenda toleo la tatu Kiingereza na toleo la nne Kiswahili.

Aliyekuwepo na hicho unachoita stori za dini si mie bali ni wasomaji wa kitabu hiki ambacho kimependwa kwa kuandika historia ya kweli.

Ni bahati mbaya kuwa wewe unaghadhibishwa na kitabu hiki.

Sasa tumlaumu nani?
Chuo Cha Kivukoni kwa kupotosha historia ya TANU au Mohamed Said kwa kuirekebisha historia?
 
Gangongine,
Huijui historia ya Waislam na Nyerere.

Soma kwanza historia yetu uwajue wazee wangu na nini walifanya
hadi kumfikisha Nyerere pale alipofika na nini Nyerere aliwalipa.

Kwani wewe ulimjua Abdul Sykes kabla ya mimi kueleza habari zake?

Au ulipata kumsikia Sheikh Hassan bin Amir popote pale au Sheikh
Suleiman Takadiri
?

Unachofanya wewe ni sawa walichokuwa wakifanyiwa Wayahudi na
Wajerumani.

Wamewarundika ghetto Poland hawana vyoo wala maji kisha wanasema
kuwa Wayahudi ni wachafu.

Waislam wamevunjiwa taasisi iliyokuwa inataka kujenga Chuo Kikuu 1968
na wananyimwa kila fursa katika elimu kisha wanalaumiwa ati mbona
hawajajenga vyuo kama wenzao.

Msome Njozi (2002) kaeleza kila kitu.
Sivalon (1992) yeye kasema wazi Uislam ni adui yetu.

Bergen (1981) kaeleza Nyerere alikuwa anapendelea kanisa lake.
Takwimu si hizo ndugu yangu nakuwekea hapo juu?

Au unataka nikupe miradi ya elimu ambayo illihujumiwa toka tupate uhuru?
Mimi nakubaliana na kauli yako.

Hakika mimi si wakajadiliana na wewe.
Wewe huna unachojua.

Mimi niehadhiri vyuo kadhaa Ulaya na Marekani na nina paper kadhaa
nimewasilisha na nina kitabu cha historia kimo ndani ya Cambridge Journal
of African Histrory.

Mimi nimeshiriki mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York
kuandika Dictionary of African Biography (DAB).

Wewe umeandika kipi kaka?

Mawazo Mfrisi kabisa kutaka waislamu waonekane walinyanyaswa na nyerere,hivi ukiwa meislamu ni lazima uwe mlalamishi!!!!!na kusingizia wengine kuwa walikuonea au unaonewa!!!!! Au ninyi mnataka kuufanya uislamu maana yake ni kulalama?????
 
Wewe Udini utakuja kukuua au utakuja kuua watu kwa sababu ya Udini wako,Hivi wewe huwezi kuandika makala zenye amani bila kuweka Uislamu wako na kuponda imani zingine????
Echolima,
Kitabu kimechapwa 1998 na matoleo kadhaa yamechapwa.

Hajafinywa hata kuku kwa kusomwa kitabu hiki.

Lililopo ni labda watu mfano wako kuchomwa na ukweli ulioandikwa katika kitabu hiki.

Kitabu kimefanyiwa review na mabingwa wa
historia ya Afrika hakuna aliyekishutumu kwa udini.

Hiki ni kitabu cha historia lakini wasomi wanakiita corrective.

Naamini unajua wana maana gani.
 
Mawazo Mfrisi kabisa kutaka waislamu waonekane walinyanyaswa na nyerere,hivi ukiwa meislamu ni lazima uwe mlalamishi!!!!!na kusingizia wengine kuwa walikuonea au unaonewa!!!!! Au ninyi mnataka kuufanya uislamu maana yake ni kulalama?????
Echolima,
Jifunze kuandika vyema.
Kisha jitulize usome historia ya uhuru wa Tanganyika.

Hivi unavyoandika huwezi kufanya mjadala wa maana na mimi.

Labda na watu wengine lakini si mimi.
Mimi nimetafiti na nimeandika kitabu ambacho ndicho kilichoziba mapengo mengi katika historia ya TANU.
 
Huwa najisikia kuchoreka sana ninapomuona mwafrika anashabikia uislamu au ukristo. Ukristo una miaka elfu mbili. uislamu una miaka elfu moja na mia tano. Lakini dini za kiafrika zimekuwepo kwa zaidi ya miaka billioni mbili. Its only a fool who will exchange 2 billions with 2000 or 1500...

Hapo ndipo elimu inahitajika kabla ya kukurupuka, kwanza unatakiwa uelewe maana ya Uislam ni nini kabla hujakurupuka na kuupangia miaka 1,500.
 
Mnataka tujadili udini kwa manufaa ya nani?

Waafrica ni kama tunalaana vile. Badala ya kujadili maendeleo ya watu wetu mnataka tujadili udini Ili tulete vita tuuane wenyewe kwa wenyewe.

Tuache upuuzi huu wa udini.
Kwako ndio upuuzi ila kwa wahanga wa udini wanajua madhara yake
 
EcholimOTE="Echolima, post: 17007293, member: 7509"]Vitu vyenye viashiria vya uchochezi wa kidini havina nafasi kwangu,Pamoja na hayo mnapalilia udini kwa faida ya nani hasa???[/QUOTE]
Echolima,
Hakuna uchochezi katika historia hii.
Ili taifa lijue leo yake ni muhimu ijue kwanza jana yake.

Ikiwa haya yakielezwa yanakuudhi huna lazima ya kuchangia.
Jikalie pembeni kwani aliye kando haangukiwi na mti.
 
Tejateja,
Kuwa Nyerere hakuwa mbaguzi si wewe kusema na kuhukumu.

Hakuna afundishae wanae ubaya na historia imeandikwa na dunia itaamua kuhusu hili la
ubaguzi wa Nyerere.

Wala hili si jambo la hamaki na kutaka kutujana watu.
Hii ni historia ya kweli ya yaliyotokea na ni muhimu kujulikana ili tusirudie tena makosa.

Wewe Mohamed Said unajivunjia heshima bure,kuchokonoa aliyoyafanya mke wako alipokuwa Bint,maana hata ukiyachokonoa hayo huwezi rudisha bikira yake!!Mmeng'ang'ania chuki zisizo na msingi hata hazijengi umoja wetu bali zimelenga waislamu kuwaona wakristo ndiyo waliodumaza fikra na maendeleo yao,hayo ni mawazo ya watu waliofilisika kimawazo wanawaza kuwachochea wengine waonekane kwa jamii furani ni wema.
 
Wewe Mohamed Said unajivunjia heshima bure,kuchokonoa aliyoyafanya mke wako alipokuwa Bint,maana hata ukiyachokonoa hayo huwezi rudisha bikira yake!!Mmeng'ang'ania chuki zisizo na msingi hata hazijengi umoja wetu bali zimelenga waislamu kuwaona wakristo ndiyo waliodumaza fikra na maendeleo yako,hayo ni mawazo ya watu waliofilisika kimawazo wanawaza kuwachochea wengine waonekane kwa jamii furani ni wema.
Furani?
Fulani.
 
Unastahili kuchomwa moto tena wa gesi kwa tabia zako za kichochezi,raha yako ni kutaka kuona watanzania wanapigana kwa udini? narudia tena Unastahili kuchomwa tena moto wa gesi....!!

Haya haya huko mashariki ya kati yalishaondoa amani maana kila kukicha mwarabu anamwambie mwanae habari mbaya za wayahudi na wayahudi vivyo hivyo mwishowe imekuwa watu uridhishana na woto tabia ya kuchukia upande mwingine.Hii si tabia njema hata kidogo,Mohamed Said utafaidika na nini na huu uchochezi wako???
 
Msambichaka,
Unauliza ushahidi?

Kwani hukuona rejea iliyowekwa?
Kitabu kilipigwa marufuku kwa kuwa kilitoa ushahidi wa yote.


Msambichaka,
Nimeandika kitabu hiki kwa kutumia staili ya, ''biographical approach.''
Ndiyo sababu unaona jina la Abdul Sykes.

Hii ni sababu ya kwanza.

Sababu ya pili nilitaka kuwahakikishia Chuo Cha Kivukoni (1981) walioandika
historia ya TANU bila kutaja jina la Abdul Sykes kuwa walifanya dhulma na
udanganyifu mkubwa.

JDYsmmgBx5zoLD50cqis1EXTTLtY92JkrAwwN7tBKOR7-AfpaD8FDT-sAw3PjpCP-JTDz5ggJq8jlQtN0oyqkr-OXjnBGZDAQLjjd75ADIXwvUlQ-U57up02nqi9il977v0_HTEpN-zO2IKRp95MDGeWzc2P7LX5XIxrg161oatw6VDqS7Pqn2eF1pkpQFpnO-olWKzghj_9fyvj5GAVTB54kT5jg8lQ2laD9tRRAjvu5GCT1DpVn0W0-GmnZ1YtbbD7bG6SGfOtuNYa3a-FEpCaBb4bS4oH5I0EhKZN5vO43AkXkF6xTQg4VyPsBVEJovxJ7MYmQwUba-F27uLda-NNQ7yWoaPJsDysR_6UokbOxI-6GGmmikX1umN3EgT2P3JuiuY7OCb7hETD1r8fOKW5ncJ7sb3mFjZ1mRrBTFzKVtbJPl5XhOPwSqWKco25iC0MKSBQ5wRftvd7ba8I40sZfcCUmxbUKJTnpIA6TFf50md1CGtpdhLM9O-Ffd2L3RNI457UXeK_ioY4xe6HDIAWhMSWqyJKB9g3JoZ2OYgyVHFPn_fumoMJLkgXcrXjKQj-Gnf6eVdfoudnIpHekhD2Ghww3FM=w890-h657-no

Kitabu hicho kilipigwa marufuku kwa kuwa kilikuwa kinachochea uvunjifu wa amani.
 
Mbona huelezi ni nani chanzo cha taarifa juu uya mazungumzo ya watu watatu,Nyerere,FDR Rweyemamu na mwakilishi wa Papa?unasisitiza mtu akasome kitabu kilichopigwa marufuku
 
Kitabu hicho kilipigwa marufuku kwa kuwa kilikuwa kinachochea uvunjifu wa amani.
Echolima,
Hujui historia ya kitabu cha Mwembechai na ndiyo maana unasema hivyo.
Serikali haikutoa sababu za kukifungia.

Wewe umetoa sababu.
Nakupa kazi moja.

Hebu jiulize kwa nini serikali haikutoa sababu.
Hii mosi.

Pili ikiwa hujakisoma kitabu kisome na ufanye uamuzi.

Kitabu hiki kiliandikwa baada ya Waislamu kumsomea risala Rais Mkapa
kuhusu madhila ya ubaguzi dhidi yao.

Risala hii ilisomwa na Ramadhani Madabida katika Ukumbi wa Diamond.

Katika majibu Mkapa akawaambia Waislam wampe ushahidi na ndipo kitabu
hicho kikaandikwa.

Ingependeza sana kama kabla ya kuandika angalau ukafanya utafiti mdogo.
 
Mbona huelezi ni nani chanzo cha taarifa juu uya mazungumzo ya watu watatu,Nyerere,FDR Rweyemamu na mwakilishi wa Papa?unasisitiza mtu akasome kitabu kilichopigwa marufuku
Magangwala,
Tatizo kubwa ninalokutana nalo hapa Majlis ni kuwa wengi wenu
hamchukui tabu ya kusoma kwa utulivu.

Rejea ya hiyo taarifa nimeitoa hapa mara nyingi sana.
Chanzo ni Bergen (1981).
 
Back
Top Bottom