TUCTA ivunjwe, hakuna sababu kuwepo

MPadmire

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,928
3,225
TUCTA ina faida gani kwa sasa?

Jamani hawa TUCTA wameshindwa kulaani hata huu ufisadi mkubwa uliofanywa na Mawaziri.

Sasa kama hela nyingi hivi zimeliwa, je wafanyakazi si wanaweza kulipwa hata 500,000 kwa Mwezi?

Pia TUCTA imeshindwa kuzibana KAMPUNI binafsi ili zilipe wafanya kazi wa Sekta binafsi vizuri. Vyama vya sekta binafsi viko hoi na viongozi wake ni wanafiki. Viongozi wakuu wa TUCTA mmepewa Nini?

TUCTA imeshindwa kuwabana Mashirika ya Hifadhi kama NSSF, NPF, LAPF n.k ili zikopeshe wanachama wake

Sasa TUCTA inasimama au inatakiwa iwepo kwa ajili ya nini?

kama TUCTA inashindwa hata kuwaunganisha wafanyakazi wa Sekta binafsi na serikali ili kuandamana kulaani ufisadi watanzania tumeisha.

jamani Watanzania tumegawanyika kwa misingi gani?
 
Kila siku natafakari juu ya TUCTA sipati jibu kweli bora vyama vyote vifutwe havina faida yoyote kwa wafanyakazi. hao viongozi wa hivyo vyama wanaishi maisha mazuri wanatembelea magari ya kifahari na kufuja pesa ya chama.
 
Rais wa TUCTA walikuwa na JK Mkwe.re pale Tanga shule wanajuana na usitegemee jipya, katibu mkuu naye alipoona hapewi pesa akaita vyombo vya habari naye akalipwa na hapo Mkwee.re akatukana mbayuwayu-TUCTA kwisha hawamuwezi. Ukibadili uongozi TUCTA bado ni muhimu
 
Mgaya kashatulizwa na system anakula kwa ulaini. Amekuwa sehemu ya serikali kukandamiza wafanyakazi. Hta comments zke wkt wa mgomo wa madaktari zilikuwa pro govt. Cha maana ni kuwang،oa.
 
Vyama vya wafanyakazi vilikua na nguvu wakati wa kutafuta uhuru wa Tanganyika,baada ya hapo sijui walikua nini hawana cha ziada walichofanya kuiwajibisha serikali wakati wafanyakazi ni moja ya walipa kodi kubwa kawa serikali hii. yani kama kufutwa vifutwe vyama vyote vya wafanyakazi tujue hamna kabisaa
 
hii thread nilikuwa naiota, hakuna chochote ambacho chama hiki kinafanya ili kuwasaidia wafanyakazi nchini! Mimi binafsi nashauri wafanyakazi wote wasusie sherehe za mei mosi mwaka huu, pili kila mfanyakazi ajitoe kwenye chama cha wafanyakazi ambacho yeye ni mwanachama, tatu nashauri tarehe moja mwezi ujao tuandamane kwenda kwenye jengo la bunge tukalitie moto ili kushinikiza marekebisho ya sheria ya kodi ambayo ni dhurumishi! vingenevyo wafanyakazi tutakuwa maskini na corrupt milele!
 
Asante wachangiaji. Natumaini TUCTA watasoma huku na pia kama kuna mtu ana namba ya Mgaya au Rais wa TUCTA amwambie asome maoni huku JF.

Pia Naunga mkono maoni ya SoNotorius - MWanajf hapo juu.

Wafanyakazi wajitoe TUCTA na vyama vyake
 
Kila siku natafakari juu ya TUCTA sipati jibu kweli bora vyama vyote vifutwe havina faida yoyote kwa wafanyakazi. hao viongozi wa hivyo vyama wanaishi maisha mazuri wanatembelea magari ya kifahari na kufuja pesa ya chama.

QK
Ukiangalia kwa undani , hawa viongozi wa hivi vyama ni kama hawa wabunge waliopiga kelele juzi bungeni kwa jazaba, halafu wakashindwa kuchukua hatua kwa kuweka sahihi kwenye listi. Ukiwaangalia maisha yao na wanao watetea waweza lia... unafiki unafiki unafiki kwa kwenda mbele, wanapewa vizawadi na ahadi kidogo wanawauza wanao watetea.

hakuna maana ya kuwa na hivi vyama vya wanafiki tu...
 
hii thread nilikuwa naiota, hakuna chochote ambacho chama hiki kinafanya ili kuwasaidia wafanyakazi nchini! Mimi binafsi nashauri wafanyakazi wote wasusie sherehe za mei mosi mwaka huu, pili kila mfanyakazi ajitoe kwenye chama cha wafanyakazi ambacho yeye ni mwanachama, tatu nashauri tarehe moja mwezi ujao tuandamane kwenda kwenye jengo la bunge tukalitie moto ili kushinikiza marekebisho ya sheria ya kodi ambayo ni dhurumishi! vingenevyo wafanyakazi tutakuwa maskini na corrupt milele!

Hii sheria ya kodi ndi balaa kuliko zote..... na mbaya zaidi ni hizi kodi hawa wahuni wanakwenda kukwiba na kustarehe ....inauma sana...
 
Inawezekana kabisa kima cha chini mshahara kuwa laki 3 kama ilivyopendekezwa na TUCTA.

Angalia ni mabilion mangapi yamepotea katika ufisadi wa serikali.

Kile kisingizio eti serikali haina hela ni uongo, wanatafuna wenyewe mawaziri.

Hata madokta wanaweza kulipa stahili safi na watanzania kupata huduma bora za afya.

Ila TUCTA yetu imelala
 
Back
Top Bottom