Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mmeishiwa? hamnatena sera
Huyu jamaa sijui kama atafika tunakoelekea....mmhuuu yangu macho nuksi inakuja.
Tanzania, kila mtu ni daktariHii kali
Naomba kuelimishwa juu ya hili,hivi kuna utaratibu/sheria ya mgombea Urais kupeleka ripoti ya afya yake katika tume ya Uchaguzi ili kujua kama mgombea yuko fit?kama haipo,hii si ni hatari kwa taifa kiuchumi na kiusalama wa taifa!
Kwa maoni yangu kiongozi wa ngazi ya juu kama rais,ni muhimu akawa na afya nzuri japo kuna maradhi mengine madogo madogo ambayo hata kama akiwa nayo hayato muathiri sana katika utendaji kazi.Hii ni kwa sababu Rais akiwa mgonjwa kila wakati,rasilimali nyingi itatumika kumtibu kutokana na nafasi yake.Pili Rais aliyechaguliwa na wananchi ananguvu zaidi ya kuwaunganisha wananchi na mara nyingi huwa na anakuwa na ushawishi kwa viongozi katika serikali ,watumishi wa uma na binafsi na wananchi kwa ujumla.Ikitokea kwa sababu ya maradhi raisi akaondolewa katika nafasi yake au kwa maradhi yale tukampoteza na nafasi hiyo kuchukuliwa na makamu wake,kuna uwezekano mkubwa wa serikali kuyumba,kutokana na nguvu ndogo ya ushawishi kulinganishwa na Rais wa kwanza,ni hatari kwa usalama wa taifa.Ingawa yawezekana rais mpya akawa na ushawishi mkubwa na kukubalika kwa wananchi pia.
Why taking risk?
Vile vile kuwe na sheria ya kumpima mgombea yeyote wa nafasi ya urais kama ana afya ya akili!!