Tuanzie na mtanzania huyu halisi nadhani tukimbana vilivyo atatuambia nani kala nini na lini

so who

Member
Oct 28, 2011
73
7
SAM_2434.JPG
 
duh!
Ni wajibu wetu kubadili hizi sheria zetu ziwe na meno makali zaidi. hii inatisha! kwa sheria zilizopo huyu huwezi kumshitaki, na ukithubutu hasara kwa taifa itakuwa kubwa mno.
 
Kuna jamaa amechukua jukumu la kufuatilia kwa karibu kujua ni mhasibu gani pale Hazina anaweza kuwa na kiasi kikubwa cha pesa kiasi kile.

(1)
Habari zilizopo ni kwamba inasemekana mhusika ni Mhasibu Mkuu wa Serikali (ACGEN) anadaiwa amekuwa akichota pesa nyingi kwa njia zaudanganyifu ikiwemo kuwalazimisha watu waliochini yake kumfanyia malipo ya posho kwa kila shughuli inayofanyika pale ofisi yamhasibu mkuu wa serikali na amekuwa akilipwa kwa kila shughuli kama msimamizi mkuu wa shughuli bila kujali yupo ofisini, yupo nje ya nchi au yupo likizo.

(2) Inasemekana posho mbalimbali anazolipwa kwa mwezi kutokana na shughuli za pale ofisini kwake zimekuwa zinamuingizia zaidi ya Tshs 80,000,000.00 (milioni80) kwa mwezi ambayo ni sawa na Tshs 2,666,666.70 kwa siku inadaiwa kwamba proposal yeyote ya kazi isiyo onyesha posho yake itakuwa bei gani haiwezi kupitisha. Na amekuwa akiwafanyia roho mbaya mbaya zisizo na mbele wala nyuma.
Imefikia mara utasikia Mhasibu mkuu wa Serikali (ACGEN) ana mgogoro na mtu mdogo kama secretary au dereva fulani na kamhamisha kituo cha kazi na kufuatilia aliko mhamishia ahakikishe unapata taabu kama alivyokusudia au lah, shughuli ambayo kimsingi hatakiwi kuisimamia mtu wa hadhi yake aliyeapishwa na Rais kwa kushika na kuahidi kuilinda KATIBA YA NCHI".:spider:

(3) Taarifa zinaendelea zaidi kwamba kutokana na kwamba mkataba wake wa kazi karibia utaisha ameongeza ukali(orally) kwa watu wanaomuwekea kiwango kidogo vya posho kwa kisingizio cha ufinyu wa bajeti kwa kila shughuli.

(4) Habari kutoka idara nyeti za TISS na PCCB zimethibitisha kuwa ana mabilioni ya Shiringi katika akaunti yake ambayo watu waliofanyiwa ubaya kwanza ni idara hizo mbili kuna miezi fulani hawakulipwa mshahara hata OC hawakupelekewa na wanaweza wakawa wametoa hii chokochoko ili Serikali iwape kibali kumchunguza na wameangalia vyanzo vyake vya mapato bado hajakidhi kumiliki kiasi hicho na mara ya kwanza walivyoitupa habari hii hewani watu walimfuata GAVANA wa BOT B NDULLU wakihisi ndio mmiliki wa akaunti hizo lakini vijana wakajitahidi kuirekebisha ukweli ukawa nje.

(5)
Vijana wameweza kubaini posho anazo saini hata akiwa likizo, na vishughuli mbalimbali anazozianzisha ilimradi tuu yeye apate pesa. Kuna taarifa pia kwamba kwamba kaanzisha viproject vingi sana vya ujenzi lakini vina maslahi yake kama vile ukarabati wa kisehemu kidogo cha kukaa wastaafu na madreva wakisubiri huduma na kazi, inadaiwa kibanda hicho kimeghalimu (Milioni58) Tshs 58,000,000.00 na hiyo kazi aimefanya yeye akishirikiana na mtu wake wa karibu sana (Afsa utumishi) bila kuwa shirikisha watu wa ugavi.

(6) kuna mtu anaifanyia finishing hii kashfa ataileta hapa JF naomba tuone hawa watuwanaovunja katiba hii waziwazi wakidhani ni mbovu kama tunavyoilalamikia nadhani hapa ubovu wa katiba ya nchi hii upo kwa mhalifu kama huyu kumsubiri aliyemteuwa afanye maamuzi.

(7) Amekuwa akipokea fedha za hongo na cha juu anachoweka kwa ujenzi wa ofisi za hazina ndogo huko mikoani. Kwa mfano ile ya dodoma ujenzi wake bado kabisa lakini mabilioni ya pesa amekwapua huku akiwaambia wakandarasi walete madai upya za kazi za ziada pori na anazipitisha wakati hakuna kazi iliyoongezeka.

(8) Ana roho mbaya sana, kwani amekuwa akipitishia kwa wakurugenzi wa baadhiya halmashauri fedha za miradi kama kilimo ambazo baadaye huchotwa na maofisa wa halmashauri na kumpelekea yeye tena.
 
Duh yaaani billion 150! Zote hizo za nini? Yaani anaweza kuanzisha benki zake kumi! Twende mbele turudi nyuma hizo pesa ziko benki gani manake kama ziko hata benki mbili ama tatu tofauti siku akiamua kuzitoa kutatokea mtikisiko wa uchumi!
 
Mkuu so who inaonekana wewe u miongoni mwa wanaofanyiwa mtimanyongo na huyo mama.
 
Last edited by a moderator:
This has to be done in different way,

Find the account and query to know the owner,

Let the owner in an open language explain how he has that much money,

If he fails, suck the owner, return the money to Higher learning Institution Student Loans Board

If he says he is doing business then check every company, tax payment, income amaount and every operational details to reveal the money in the account.

Au mwisho tumnyonge tumuweke makumbusho ili awe fundisho
 
Kama ni kweli, basi VIONGOZI wakuu serikali ni Mbona mnampa kazi sana Mkuu SA NCHI? Sasa amaamini nani Jamani? Tuwe NA uchungu NA hii NCHI, hasa KWA kuwa kumbuka, wAlio vijijini, ambao ndiyo wengi NA Wenye kuteseka NA Maisha
 
Mtajeni kwa majina kama wengine wanavyotajwa... Mbona Mama Nyoni aliwekwa hadharani? Muwekeni tu na huyu WanaJF. Tunaomba wenye data za muhusika ziwekeni hapa live!
 
This has to be done in different way,

Find the account and query to know the owner,

Let the owner in an open language explain how he has that much money,

If he fails, suck the owner, return the money to Higher learning Institution Student Loans Board

If he says he is doing business then check every company, tax payment, income amaount and every operational details to reveal the money in the account.

Au mwisho tumnyonge tumuweke makumbusho ili awe fundisho

Wenye mamlaka ya kufanya hayo yote hawajaona umuhimu wa kufanya hivyo. Hupaswi kusahau kwamba hii inaitwa Tanzania, nchi ya yasiyowezekana!
 

Mkuu
so who inaonekana wewe u miongoni mwa wanaofanyiwa mtimanyongo na huyo mama.

KIMBUNGA!
MIE SIE MMOJAWAPO HAPO HAZINA NILIYEFANYIWA HUO MTIMA NYONGO NA HAJAWAHI NIFANYIA MTIMA NYONGO MAHALA POPOTE NA BAHATI NZURI HUWA TUNASALI MSIKITI MMOJA NA DINI YETU HII HAITAKI UNAFIKI NA FITNA KWETU NI DHAMBI ISIYOSAMEHEKA.
ILA INA UMA SANA KUONA FEDHA ZA WANANCHI ZIKICHOTWA NA HUKU TUKIELEZWA KWAMBA HALI  YA UCHUMI NI MBAYA LABDA AKIRUDI ILULA IRINGA ANAWEZA KUNIFANYIA HUO MTIMA NYONGO NA AKIJA LABDA KUFUNGUA BENKI HALAFU NIKAJIGONGA KWENDA KUKOPA LAKINI MPAKA SAA HIZI NAONA HURUMA KWA WANANCHI WENZANGU TUNAVYOPEWA TAARIFA ZA UCHUMI ZISIZO NA UHALISIA
 
Dawa ya watu Kama hawa akipatikana na hatia baada ya upelelezi kukamilika ni kunyongwa hadharani pale mnazi mmoja na maiti inazikwa na Halmashauri ya Jiji usiku wa manane kwenye dampo la tabata.....itakuwa mfano kwa wafuatao.
 
Dawa ya watu Kama hawa, baada ya uchunguzi na kupatikana na hatia...ni kunyongwa hadharani pale mnazi mmoja na maiti kuzikwa na Halmashauri ya Jiji usiku wa manane kwenye dampo la Tabata. Ili iwe mfano kwa watumishi wa umma na walafi wengine.
 
Back
Top Bottom