Tuache Wivu kwa Nehemia Mchechu

Status
Not open for further replies.
Labour and professionalism ni commodity, bei yake hutegemea ubora wake na mahitaji ya soko. Watanzania wengi wanadhani mshahara huamuliwa na akili na kiwango cha elimu. Kitu ambacho ni kosa kubwa.

Mshahara huamuliwa na performance. Nini output yako. Unaweza kuwa na akili kama shetani, unaweza kuwa na PhD lakini mshahara wako ukazidiwa na mwenye diploma. Unapokuwa performer, unatafutwa, hutafuti kazi. Kwa sababu umetafutwa una-dictate terms. Kama hutaki terms zake unaachana nae, ataendelea na wengine.

Na nina hakika Msechu kutoka kwa mwajiri wake wa awali, na kwa kuijua serikali ilivyo kigeugeu atakuwa alijiwekea ulinzi wa kutosha wa kiajira. Na mkitaka kumtoa hapo, unaweza kulazimika kumlipa mshahara wake wa sasa kwa mwaka mzima au miaka miwili. Halafu unamlipa leo, kesho utamsikia ameajiriwa Ethiopia, Nigeria au SA. Kwa kuifanya NHC kuwa katika nafasi ya ubora katika Afrika, huyo mkurugenzi ni wa kutafutwa tu, hatalazimika kutafuta kazi. Ndivyo biashara za kisasa zinavyotaka.

Kuna wakati nilikuwa nalipwa mshahara wa $8,000, nilipofanikiwa kuongoza timu yangu na kupata mradi uliokuwa na thamani zaidi ya $4 billion, ndani ya wiki moja nilitafutwa na makampuni manne tofauti, kila mmoja na offer yake. Mimi niliweka terms za ajira, pamoja na mambo mengine, mshahara niliweka $16,000, mwajiri akaamua kunilipa $19,700. Tukazanie performane ili tuwe na nguvu katika kupanga mishahara.

Kwenye biashara za kisasa kinachoangaliwa unazalisha kiasi gani nawe unachukua kiasi gani. Mkurugenzi wa kwanza alikuwa anazalisha negative TZS 3 billion halafu analipwa TZS 5 million. Huyu alikuwa aghali zaidi kibiashara kuliko Msechu.
Asante ndugu kwa hili bandiko tatizo watanganyika tunakariri mambo
 
hicho sio kigezo,makosa yalianza pale serekali ilipomfuata na kumuangukia,kazi ingetangazwa then watu washindanishwe,ingekuwa ndo hivyo sasa kuna maana gani ya watu kusoma??
Ndugu TAI anatua kwenye MZOGA ukiona watu wanakutafuta wakupe kazi manake wanakubali uwezo wako....kwanini sikutafutwa mimi...ushauri wangu kwa vijana wote waliokwenye Nafasi yyt ya Ajira lazima afanyekazi at the maximum... mwisho wa siku kuna kufanikiwa zaidi lkn mtu unafanyakazi chini ya kiwango Nani anataka kuajiri LOOSER
 
Labour and professionalism ni commodity, bei yake hutegemea ubora wake na mahitaji ya soko. Watanzania wengi wanadhani mshahara huamuliwa na akili na kiwango cha elimu. Kitu ambacho ni kosa kubwa.

Mshahara huamuliwa na performance. Nini output yako. Unaweza kuwa na akili kama shetani, unaweza kuwa na PhD lakini mshahara wako ukazidiwa na mwenye diploma. Unapokuwa performer, unatafutwa, hutafuti kazi. Kwa sababu umetafutwa una-dictate terms. Kama hutaki terms zake unaachana nae, ataendelea na wengine.

Na nina hakika Msechu kutoka kwa mwajiri wake wa awali, na kwa kuijua serikali ilivyo kigeugeu atakuwa alijiwekea ulinzi wa kutosha wa kiajira. Na mkitaka kumtoa hapo, unaweza kulazimika kumlipa mshahara wake wa sasa kwa mwaka mzima au miaka miwili. Halafu unamlipa leo, kesho utamsikia ameajiriwa Ethiopia, Nigeria au SA. Kwa kuifanya NHC kuwa katika nafasi ya ubora katika Afrika, huyo mkurugenzi ni wa kutafutwa tu, hatalazimika kutafuta kazi. Ndivyo biashara za kisasa zinavyotaka.

Kuna wakati nilikuwa nalipwa mshahara wa $8,000, nilipofanikiwa kuongoza timu yangu na kupata mradi uliokuwa na thamani zaidi ya $4 billion, ndani ya wiki moja nilitafutwa na makampuni manne tofauti, kila mmoja na offer yake. Mimi niliweka terms za ajira, pamoja na mambo mengine, mshahara niliweka $16,000, mwajiri akaamua kunilipa $19,700. Tukazanie performane ili tuwe na nguvu katika kupanga mishahara.

Kwenye biashara za kisasa kinachoangaliwa unazalisha kiasi gani nawe unachukua kiasi gani. Mkurugenzi wa kwanza alikuwa anazalisha negative TZS 3 billion halafu analipwa TZS 5 million. Huyu alikuwa aghali zaidi kibiashara kuliko Msechu.
Msambichika, nisaidie majibu katika haya;

1. Kuna ukweli kiasi gani unaposema mshahara haupangwi au kutolewa kutokana na kiwango cha elimu cha mtu?.Hivyo si sahihi kumlipa Prof. anayefundisha chuo kikuu mshahara sawa na Tutorial Assistance ambaye "anaakili" sana.!

2. Huyo mkurugenzi kabla ya Nehemia aliyekuwa anazalisha bilioni tatu tu, unadhani hakuwa na akili za kuzalisha zaidi au kwa kuwa serikali ilikiwa haijaamua kuwekeza intensively katika shirika hilo la umma?

3. Maswala ya uendeshaji wa biashara binafsi kama kuendesha timu yako ya mpira, hayaendani na biashara zinazofanywa na mashirika ya umma. tambua kuwa lengo kuu la serikali kupitia taasisi hizo ni kuhalalisha inatoa huduma kwa wananchi wake. Kama Nehemia anajenga na kuuza nyumba hasa kwa wageni, Sera hiyo anayoifanya haiendani na Sera ya serikali ya kuhakikisha watu wake wanapata makazi bora. Basing on your argument ni kweli Msechu "anaakili" kubwa kuliko ma DG wote hapa nchini?
 
Asante ndugu kwa hili bandiko tatizo watanganyika tunakariri mambo
Mkuu watanzania hawakariri mambo, siku hizi wanauelewa mpana wa mambo!

Ukiona wanahoji Pesa anayolipwa jamaa huyo jua hawakajua awali kama kodi zao zinatumika kulipa watu wa namna hiyo!

Si dhambi kuhoji, ni wajibu wa wanaohojiwa kutolea ufafanuzi na sio kuwabeza kuwa hakuna mtanzania .wenye akili kama msechu na kustahili malipo hayo!
 
hata akina maswi walifuatwa kuombwa hivyo hivyo yuko wapi leo hii,ukipewa kazi unapewa na job descriptions zako zikikushinda unaachia ngazi,ndio maana ya ajira,ukiona hivyo ujue kuna mahali mambo hayapo sawa??

Ndugu TAI anatua kwenye MZOGA ukiona watu wanakutafuta wakupe kazi manake wanakubali uwezo wako....kwanini sikutafutwa mimi...ushauri wangu kwa vijana wote waliokwenye Nafasi yyt ya Ajira lazima afanyekazi at the maximum... mwisho wa siku kuna kufanikiwa zaidi lkn mtu unafanyakazi chini ya kiwango Nani anataka kuajiri LOOSER
 
Wakati watu wako busy kumsifia ana miakili huyo CEO mwenyewe interview yake aliyoiweka juu ya website yao anajivunia balance sheet ya shirika yenye billioni $2 and 20,000 houses it as if asilimia kubwa ya hizo nyumba kajenga yeye.

Kumaliza mzuzu wa fitina kwanini asitoe financial report we all know hiyo balance sheet large contribution ni value ya majengo sio cash assets; na income kubwa ni rent ambazo anan'gamua wananchi ndio zinazosaidia kuonekana shirika lina pesa lakini sio miradi yake binafsi aliyobuni walidai nyumba mchikichini zimeisha leo wanapangisha tena kwa wabantu tu wakawaida.

It was all predictable bila ya rent hike alizokuja nazo sasa hivi angeshakuwa chali yaani n'gombe wa maziwa serikari iliyomuachia awakamue atakavyo kwa madai ya kuwa wako chini na bei ya soko ndio wanaomfichia madeni yake na ubovu wa miradi yake the guy is useless.
 
NCHI hii ina watu MASIKINI wengi mno. Unapodai malipo/mshahara wafikirie na hao wanaoishi kwa chini ya shs elfu1 kwa siku.
 
Mimi nasikitika sana hawa jamaa wa NHC wameingia ubia na wahindi kujenga majengo mengi na makubwa yakiwemo yaloanguka na lile linalovunjwa bila kutangaza tenda.PPRA uko wapi ? hayo majengo ni ya serikali walichotakiwa NHC ni kutangaza mtu anaetaka kuingia ubia wa ujenzi ,basi watoe tender ! wao wanafuata wahindi kimya kimya ! na wahindi kwa kutumia hati miliki za NHC wanapata mikopo kiulaini ndo wanajenga na zingine zikibaki mambo mengine ! halafu eti mnamsifia Mchechu ? watu wanapiga hela ndefu hapo ! hawa jamaa wanatumia Landcruisers za kisasa kila director wakati kila mmoja wao amekopeshwa Landcruiser mpya ! sasa kwa nini wasitumie hizo walizokopeshwa NHC ikawapa mafuta ? wamekopeshwa magari na bado wanatumia magari ya kisasa ya NHC jamani huu si ndo ufisadi wa waziwazi ?mi nashangaa mheshimiwa raisi hajatujumbua jipu hili ! mehishiwa Raisi NHC ni jipu kubwa sana.
 
Napendekeza Msechu awe CEO wa AIR TANZANIA baada ya Magufuli kununua ndege alizoahidi na kuwaondoa watumishi wote. Halafu alipwe 40M! Huyu kijana in hazina ya Taifa! Tuache wivu!
 
Napendekeza Msechu awe CEO wa AIR TANZANIA baada ya Magufuli kununua ndege alizoahidi na kuwaondoa watumishi wote. Halafu alipwe 40M! Huyu kijana in hazina ya Taifa! Tuache wivu!
He He he yaani huna mtu mwingine mwenye vision na exposure ya nini kinaendelea duniani ila Mchechu. Pole for that 46 m people you only see one. sitaki kufikiri upeo wako wa kufikiria ila nihisi umetumia hisia zaidi kuliko kichwa chako. Na kama ni kichwa fanya mabadiliko haraka utaachwa na wakati. wewe huoni arguments zinazotolewa ukaelewa kwa mapana nini kinaendelea onaongelea wivu. Wacha uvivu wa kufikiri bwana.
 
Mkuu Projects zimeanza mwaka juzi tu hapa.. Walikuwa na strategic plan ya 2010/11-2014/15 sasa labda muanze kujudge kulingana na strategic plan yao inavyosema... Hivi kweli Project ya miaka mitano tu mnataka tayari leo tuanze kufaidika?? Jamaa anapigana shirika lifikie BEP ili aanze kujenga nyumba kwa fedha zake wenyewe lakini watu wanataka kumkwamisha na kumkatisha tamaa... Tuachane na mambo ya kuwa na wasomi wengi, hebu pitia hilo profile lake huyo jamaa then upime kama hadeserve hiyo pesa anayolipwa...

Kingine tutachukua wa bei rahisi alafu atuangushe tushindwe hata kulipa hizo pesa tulizokopa... Acheni Mchechu apige kazi, muda aliopewa akishindwa kulifikisha shirika kule ambako serikali ilipanga ndio tumjudge...
Mimi ninavyo jua serikalini hakuna kunigotiate malipo, yapo kwa elimu ,miaka ya kazi na vyeo kulingana na muundo wa sehemu husika. sasa ile post ilikuwa na benefit zake kilichofanyika ni kuvuruga scheme kwa manufaa ya MCHECHU does it worth that transformation ? Je huo sio uvunjwaji wa sheria za ajira serikalini? kwanini ifanyike hivyo? analipwaje zaidi ya katibu mkuu wake au waziri toeni reason sio hakuna mtu kama yeye wakati wato tena hawata piga dili yaani waadilifu zaidi Subiri post inapatiwa mtu.
 
Nimekuwa nafuatilia mjadala hasa wa Rais Mtukufu bwana Magufuli kuhusu mishahara ya watumishi kuwa mikubwa.

KIMSINGI Nadhani rais ana nia njema ya kujenga moyo wa uzalendo kwa watu ili watangulize maslahi ya Taifa kwanza na yao binafsi yaje baadae.

Tatizo langu nikwamba watu wengi tumejikita zaidi kumshambulia Nehemia Mchechu CEO wa NHC. Eti tu kwa kiwango tunachokiita kikubwa cha mshahara wa M35. Wengi wetu hatuzungumzii Mchechu alikutoka alikuwa analipwa 26M.

Na alianza project ya kujenga nyumba akiwa kwenye taasisi yake ya zamani. So serikali iliona atafunika NHC zaidi kwasababu ni wazi shirika lilishakuwa kinapumulia mipira.

NHC kifupi ikishakaribia kufa Bwana Mchechu hakuomba kazi NHC serikali ilimfuata. Mchechu amefanya kazi kubwa sana NHC ukilinganisha na ilivyokuwa mwanzo. Mchechu anastahili kulipwa zaid ya hapoo.

NHC ni shirika la 3 now kwa Ubora wa mashirika ya Nyumba africa lakwanza NHS ya SA yapili Ethiopia na Tatu Tanzania. Sasa mnataka huyu kijana wa watu afanye nini? Watu wanaongea hoja ya nyumba za NHC kuwa za bei kali sio za watu wa hali ya Chini.

Thats true but we have to know kwamba Sera ya NHC haijawahi kuwa na sera hiyo ya nyumba za bei nafuu kwa watu wa Hali ya Chini. Hakuna mahala popote NHC iliwekwaa kwaajili ya kujenga makazi ya Wanyonge.

So kama kuna watu tunahitaji NHC iwe ya wanyonge ni kuwakumbusha watunga Sera wetu wakabadili sera ya NHC kuacha kujiendesha kibiashara. Mchechu hata kwa hako ka M30 anatuhurumia tuu.

Wenye vyeo kama chake huko kwenye taasisi aliyotoka sasa hivi wanakula mpaka M75. Ifike mahali tusisukumwe kwa wivu pekee juu ya Mchechu tuache wivu tumuache afanye kazi.

mchechu hakutaka kuafanya kazi serikalini kwa sababu mbalimbali na mojawapo mishahara midogo. serikali ikamfuata na kutaka huduma yake, ni wazi jamaa ameweka dau analolitaka. sio kila mtu anaenjoy mishahara midogo na ukiritimba, na sio kila mtu yuko tayari kuwahudumia watanzania kwa kufanya kazi serikalini. kama magufuli na watanzania wengine wanafikiri mchechu anachofanya ni kibaya then wakatishe mkataba wake. aliamua kwenda private sector kwa sababu zake, msifamfanye awe sehemu ya kutoa nyongo zenu za chuki bila sababu za msingi
 
He He he yaani huna mtu mwingine mwenye vision na exposure ya nini kinaendelea duniani ila Mchechu. Pole for that 46 m people you only see one. sitaki kufikiri upeo wako wa kufikiria ila nihisi umetumia hisia zaidi kuliko kichwa chako. Na kama ni kichwa fanya mabadiliko haraka utaachwa na wakati. wewe huoni arguments zinazotolewa ukaelewa kwa mapana nini kinaendelea onaongelea wivu. Wacha uvivu wa kufikiri bwana.
Mkuu huyo jamaa ulie mjibu amemtaja Mchechu nadhani baada yakuona kazi anayofanya hapo NHC kwa kumthibitishia kwamba NCHI hii sio Mchechu tu sivibaya ukataja baadhi ya Vijana wengine kama yy wanaofanya kazi zinazoonekana
 
Mimi ninavyo jua serikalini hakuna kunigotiate malipo, yapo kwa elimu ,miaka ya kazi na vyeo kulingana na muundo wa sehemu husika. sasa ile post ilikuwa na benefit zake kilichofanyika ni kuvuruga scheme kwa manufaa ya MCHECHU does it worth that transformation ? Je huo sio uvunjwaji wa sheria za ajira serikalini? kwanini ifanyike hivyo? analipwaje zaidi ya katibu mkuu wake au waziri toeni reason sio hakuna mtu kama yeye wakati wato tena hawata piga dili yaani waadilifu zaidi Subiri post inapatiwa mtu.
Mkuu unaweza kuthibitisha hii
 
Mkuu huyo jamaa ulie mjibu amemtaja Mchechu nadhani baada yakuona kazi anayofanya hapo NHC kwa kumthibitishia kwamba NCHI hii sio Mchechu tu sivibaya ukataja baadhi ya Vijana wengine kama yy wanaofanya kazi zinazoonekana
Kuna kazi huoni kwa macho kwa maana ya majengo lakini zipo documented sasa utasemaje. wapo walimu wazuri sana lakini utasifia wanafunzi kuwa wanaakili husifii mwalimu aliye mfundisha, kunaadministrators wazuri sana huwezi kuona utasikia wanasifiwa. Kuona majengo kunakufanya usifie mtu je umejua yanaleta faida gani katika uchumi wa nchi? Nini lengo la uanzishwaji NHC kujengea kina nani ? umefanya uchunguzi ni kina nani wanunuzi wa hizo nyumba? Baada ya miaka kadhaa nini itakua hali ya Mabenki ambayo yamefacilitate ujenzi wa majumba hayo? kuna mkakati gani wa kuzuia kilichotokea Dubai kiuchumi kisitokee huku? ukisha nijibu hayo maswali Mlipe Mchechu 35M will be very happy. naomba tuangalie kwa misingi hiyo sio kutaja majina ya watu
 
Angaliwe upya! Hana haja ya mshahara wote huo, maana anachokifanya sio faida kwa Watanzania walio wengi!

Mtu kama Mkurugenzi wa Muhimbili Hosp alistahili kulipwa zaidi ya Mchechu, maana anaokoa
Mkurugenzi wa MUHIMBILI analipwa shilingi ngapi
kazi kwako kufuatilia.....!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom