HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,566
Mtambuzi wengi huwa tunatamani haya uliyoyazungumza, lakini ukweli ni kuwa moyo uliopenda ni mgumu sana kubadili nia kirahisi. Nimeshuhudia watu wakinyanyasika na kuteseka kwenye mahusiano yao lakini bado wanang'ang'ana. Kwa kweli upendo ni kitu cha ajabu sana.
Ila kwa ushauri naungana na wewe kwa wale wenye ujasiri wa kuvunja mahusiano mara wanapotamkiwa kuwa hawapendwi tena ni bora kufanya hivyo ili kuepuka baaadaye kuja kufanyia vitendo vya kikatili ikiwemo kuchomana visu au kuunguzana moto au pengine hata kukatana mapanga kama tulivyoshuhudia kwenye baadhi ya mahusiano fulani fulani.
Ila kwa ushauri naungana na wewe kwa wale wenye ujasiri wa kuvunja mahusiano mara wanapotamkiwa kuwa hawapendwi tena ni bora kufanya hivyo ili kuepuka baaadaye kuja kufanyia vitendo vya kikatili ikiwemo kuchomana visu au kuunguzana moto au pengine hata kukatana mapanga kama tulivyoshuhudia kwenye baadhi ya mahusiano fulani fulani.
Last edited by a moderator: