Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,466
113,543
Wanabodi,

Tuliwahi kusema humu, Tanzania inachohitaji sio a one man show, bali tunahitaji mifumo imara na thabiti, yaani an effective system. Ukiishakuwa na mfumo imara, na thabiti, kila kitu kinachofanyika kwenye taasisi, kinafanyika ndani ya mfumo thabiti, kinakuwa automated, na very transparent, chochote kitakachofanyika out of system kinakuwa detected automatically na kuwa ejected out of system, hivyo hakutakuwa hata na haja ya kutumbua tumbua, once the system is there, anyone who goes against it, anakuwa ejected out of system automatically hivyo anajitumbua mwenyewe kwa ku fall out of system.

Mimi sio mchumi ila humu jf tuna wachumi lukuki, hivyo naomba ndugu zetu wachumi wa humu, jitokezeni mtusaidieni kutuelimisha kuhusu haya mambo ya fedha, na kutuelimisha kuna dhambi gani kufungua FDA ili fedha kiduchu taasisi inazopewa zihifadhiwe huku zinazaliana angalau kukidhi mahitaji ukilinganisha na kuzihifadhi tuu fedha hizo kule BOT ambako hazizalishi hata sentí moja?!.

Mwezi Julai nilifanya mahojiano na CAG Prof.Musa Assad kuhusu kupigwa panga kwa budget ya CAG. Kumbe sio ofisi ya CAG pekee iliyopigwa panga, bali wizara zote na idara zote pia zimepigwa panga na kupewa only 40% ya mahitaji yake ya kibajeti.

Sasa kama TRA imepewa hicho kidogo kisichotosheleza mahitaji, menejmenti ikajenga hoja za msing kwenye bodi wafungue FDA ili hicho kidogo walichopewa ambacho hakikidhi mahitaji, angalau kiongezeke kupunguza nakisi, kwa maoni yangu, hili ni jambo jema na kama linafanyika kwa nía njema na kwa uwazi, kuna ubaya gani?.

Hivi ni kweli hizi FDA za taasisi za umma ikiwemo TRA, zimefunguliwa ili bodi na menejmenti wazipige hizo interest?!. Yaani bodi zenye watu wenye weledi walioteuliwa na rais na waziri husika, tena kukiwemo mwakilishi kutoka kule kwa wale 'jamaa zetu', halafu wote wacollude na menejimenti ya taasisi zao, kufungua FDA, ili waziibe hizo interest?!, japo kuna watu wanaamini everthing is possible in Tanzania!, mimi siamini hili linawezekana!, kwa sababu hata ikitokea kuwa ni kweli, wengine wote wanaweza kuwa ni majizi!, lakini hata wale 'jamaa zetu' wale?!, kama hili ni kwel na limekuwa likitendeka, then, Tanzania tuna tatizo kubwa zaidi kuliko tunavyojidhania, yaani tutakuwa tuna a rotten system!, yaani mfumo uliooza kabisa na unanuka!. Ndio maana nasisitiza Tanzania we need an effective systems zenye maximum transparency na sio hizi one man show zinazoendelea sasa.

Kwa vile Mkuu sio mchumi, ila amezungukwa na wasaidizi ambao ni wachumi waliobobea wanaojua uchumi kinyumenyume, ambao wanajua kama ni kweli rais ametoa amri fedha zote kabisa za umma na taasisi zote za umma zitumie BOT pekee kwa shughuli zake zote za fedha, then wanajua wazi kwamba he is not doing the right thing na wameamua kulinyamazia hili na kukaa kimya bila kumweleza mkuu kuwa hili haliwekan, ba badala yake wakimwacha tuu afanye anavyotaka kwa kumuogopa tuu, wajue ni wao ndio watakaohukumiwa kwa sababu wao ndio wanaojua na huyo mtendaji yeye hatahukumiwa, kwa sababu hajui atendalo!.

Nasisitiza Mkuu hatahukumiwa kwa sababu kila analoliwaza, analolisema na analolitenda, anayafanya yote hayo kwa nía njema na dhamira safi, lakini kumbe masikini wa watu, hata hajui atendalo kwenye uchumi wa nchi hii kwa sababu hajaambiwa, hivyo yeye hana kosa.

Sekta binafsi yenye nguvu ndio injini ya uchumi wowote imara wa taifa lolote, sekta binafsi nchini iko kwenye hati hati ya ku collapse kutoka na kupungua kwa mzunguko wa fedha, huku sote tukiitwa ni wapiga dili!. Hivi kweli kila mwenye kilio cha hali ngumu ya uchumi ni mpiga dili?!.

Kama issue ni mabenki binafsi kutengeneza faida kwa amana ya fedha za umma, then BOT wafungue kitengo cha BOT Commercial Bank, na wawe na matawi nchini nzima ili hizo pesa za taasisi za umma zinazokula kiyoyozi tuu kwenye strong rooms za BOT, ili zisiote uvundo, zifunguliwe FDA huko huko BOT, ili zizalishe interest, na sisi sekta binafsi pia turuhusiwe twende tukakope BOT turudishe fedha kwenye mzunguko.

Vinginevyo hata hii Tanzania ya viwanda inayohubiriwa sasa ni hadithi tuu, hata serikali ikitegemea capital injection ya uchumi wa viwanda itoke kwenye FDI (Foreign Direct Investment), bila a strong private sector, bila DDI (Domestic Direct Investment), kwenye hiyo Tanzania ya viwanda Watanzania watakuwa ni watazamaji tuu hiyo Tanzania ya viwanda badala ya kuwa ni washirika, ila hata hiyo raw materials ya kushibisha uchumi wa viwanda itatoka wapi?.

Wachumi jitokezeni mtuelimishe maana sisi wengine sio Wachumi maana naona kwa Tanzania kila kitu ni siasa, siasa ni siasa, jamii ni siasa hata uchumi sasa ni siasa! . Tuachage siasa kwenye mambo mengine jameni sisi huku mitaani tunaumia, tunapigika kweli kweli!.

Paskali.
Update.
Kwanza asanteni wachumi wa jf mliojitokeza kwenye uzi huu, ila Msajili wa Hazima, ameifunga rasmi mjadala huu kwa kauli hii.

Aliyoyasema msajili
1. Sii kweli rais amezuia taasisi za umma kutumia benki za biashara, bali makusanyo yote ya umma, government revenue, ndio sasa yatatunzwa BOT.

2. Tasisi zote zitaendelea kutumia mabenki kwenye operesheni zake.

3. Hakuna ubaa wowote kufungua FDA.

4. Kama ni kweli kulikuwa na wizi kwenye FDA, CAG ameagizwa kufanya ukaguzi maalum, hili likibainika, sheria itaachiwa kuchukua mkondo wake.

Asanteni.

Paskali
 
Mkuu. Taaluma haizingatiwi siku hizi. Ndio maana unamuona Mkuu wa Mkoa anahamisha ofisi kwenda kwenye Vyombo vya Habari.
Fedha ikikaa BOT haizalishi chochote zaidi ya kutumika.
Fedha ikikaa kwenye FD za commercial Bank inazaa interest na inakuza deposits za mabenki hivyo yanakuwa na uwezo wa kukopesha wafanyabiashara, wafanyakazi na wakulima.
Pia Bank zinapata income na kuongeza ajira na kulipa kodi. Hiyo inaitwa Multiplier & Acceleration Principles in economics.
 
Binafsi sio mchumi ila namkubali sana Gavana Ndulu
na kama yeye ni mjumbe wa bodi TRA na aliridhia maamuzi
basi uamuzi utakuwa ni sahihi
na hivyo Magufuli kachemka

but kuna suala la hiyo faida ya riba kwenda kwa watu binafsi kama sikosei
hilo sijalielewa kabisa alimaanisha nini?
kwamba fedha za TRA zikishakaa kwenye FD hiyo riba wanapewa watu?
kwenye akaunti zao binafsi?
 
unataka kusema mkuu amekurupuka kuwafukuza?
unataka kusema tumedanganywa hyo faida haikuwa inakwenda kwa hao wakubwa?
kwenye mahesabu ya TRA hyo income ipo au haipo?
ila katika yote mkuu si alitoa amri hela zote ziende BOT ? hata kama ni kwa nia nzuri kwanini walipeleka fedha huko kwenye mabenki ya biashara wakati amri ilishatoka? au kwa vile wana mashare huko? maswali ni mengi kuliko majibu hao mabwana wana makosa mimi naona watumbuliwe tu .
 
Binafsi sio mchumi ila namkubali sana Gavana Ndulu
na kama yeye ni mjumbe wa bodi TRA na aliridhia maamuzi
basi uamuzi utakuwa ni sahihi
na hivyo Magufuli kachemka

but kuna suala la hiyo faida ya riba kwenda kwa watu binafsi kama sikosei
hilo sijalielewa kabisa alimaanisha nini?
kwamba fedha za TRA zikishakaa kwenye FD hiyo riba wanapewa watu?
kwenye akaunti zao binafsi?
hata kama kuna faida na faida ilikuwa inaenda TRA ingawaje hatuna jibu hili la msingi
Magufuli mara nyingi amepiga marufuku public institutions kuweka pesa za walipa kodi kwenye mabenk ya kibiashara. Sasa kwa nini TRA ilikiuka haya maelekezo? tuanzie hapo
 
Siasa inapoendesha wachumi......

Mtu hana kozi hata ya 3month kuhusu uchumi lakini anawaelekeza maprofesor Wa uchumi kwa amri..........

Mtu hajawai kufanya biashara yeyote ikafaamika anazifundisha bank jinsi ya kufanya biashara.............

Economic crisis inatukabiri mazuzu yanashangilia utumbuaji Wa majibu ya kutafuta media publicity.......
 
kama kuna mambo ambayo yanaliangamiza hili taifa ni siasa kwenye mambo ya msingi yanayo hitaji taaluma.

Nampongeza sana comredi Mkapa kwa kutamka ukweli juu ya mambo yanavyopelekwa bila majadiliano.

Mwisho wa siku tatajikuta hatuja fanya maendeleo zaidi ya kutumbuana na pangua pangua.
 
Labda Mhe. Rais atueleze sababu nyingine tofauti kwa kuvunja bodi hii kwa sababu haiwezekani kuwa bodi ilipanga kuweka katika FD kwa manufaa yao binafsi!

Ikumbukwe kuwa katika bodi hii kuna Katibu Mkuu wizara ya fedha ambaye pamoja na majukumu mengine yeye ndiye huwa anaidhinisha kufunguliwa kwa akaunti za serikali! Isitoshe katika bodi hii yupo Gavana wa Benki Kuu ambaye ndiye anatunza hazina ya nchi hii!! Na kwa vyo vyote vile akaunti hii ya FD hukaguliwa na wakaguzi wa ndani na CAG!!

Hivi kweli watu wote hawa walitaka kupiga dili kama ambavyo tunataka kuaminishwa?!
 
hata kama kuna faida na faida ilikuwa inaenda TRA ingawaje hatuna jibu hili la msingi
Magufuli mara nyingi amepiga marufuku public institutions kuweka pesa za walipa kodi kwenye mabenk ya kibiashara. Sasa kwa nini TRA ilikiuka haya maelekezo? tuanzie hapo

Kama hakuna faida binafsi na faida itaenda TRA basi wako sahihi
kuhusu kukiuka maagizo.....Rais sio mchumi mkuu wa taifa
masuala ya uchumi wao wanamsikiliza mchumi mkuu wa taifa
ndo maana board ina gavana wa BOT....

Magufuli hajui ABC za uchhumi hapaswi kusikilizwa kila anachoongea
wachumi wanajua kuwa hajui masuala ya uchumi ndo maana wanakiuka maagizo yake

Wewe ukiwa unaumwa utasikiliza maagizo ya baba yako mzazi ambae sio dokta
au utasikiliza maagizo ya daktari?
 
Pascal Mayalla wewe una lako unalotafuta, Tz inatumia mfumo wa cash budget, ela wanayoingiza ndiyo inayotumika. Ukiipeleka ela fixed deposit ukapewa rate ya 10% halafu kuna shirika jingine la serikali linaenda tena kukopa benki hiyo hiyo kwa 15-22% ni hasara kwa serikali. Magu ana point na ukweli anaokoa pesa, sote tunajua serikali ina madeni kwenye mabenki ya ndani na mashirika ya kijamii. Kama wangekuwa wanatumia mfumo huu, sehemu kubwa tu ya deni ingepungua.
 
Siasa inapoendesha wachumi......

Mtu ana kozi hata ya 3month kuhusu uchumi lakini anawaelekeza maprofesor Wa uchumi kwa amri..........

Mtu ajawai kufanya biashara yeyote ikafaamika anazifundisha bank jinsi ya kufanya biashara.............

Anguko lake alitasahaulika.......
Mkuu una heshima kwenye hili jukwaa, zingatia makosa ya kiuandishi(herufi) yasiishushe heshima yako
 
Sasa Paschal Mayalla nina Swali...

Je Sera na sheria zinaruhusu hicho kitu?

Je, Kwa mfano, Mmeweka Pesa kwenye Fixed Account, halafu, kukatokea Inflation, yaan mfumuko wa bei, sasa, Bei ya bidhaa au huduma au gharama za mradi kusudiwa zikawa zimetoka kwa mfano, ilikuwa Sh. Bilioni 20 sasa baada ya Inflation bei au gharama za mradi zikawa Juu kwa Bilioni 22, hapo itakuwaje? Je mtaacha kutekeleza mradi husika au kununua bidhaa au huduma husika?

Je, Ina maana katazo la Mh. Rais halikufahamika mapema?

Je, Tunaweza kujiridhisha vipi kuwa ile faida baada ya kuweka pesa kwenye Fixed Account ingetumika kwenye shughuli husika na si binafsi na ikizingatiwa Uadilifu wa watendaji wetu unatia shaka?
 
Sikio la kufa......... Rais anamshauri wake na inawezekana mshauri wake ana akili kama zake au anaogopa kumweleza. Yawezekana tra walifungua kwa nia njema ila aliyepeleka taarifa kwa mkuu hakuifikisha ipaswavyo au alivyopokea taarifa alikuwa na mawazo ya wizi hivyo kudhani hata hilo wazo la tra ni wizi fulani. Nadhani sasa tumefika mahali ambapo hakuna mfanyakazi wa serikali anayeaminika mbele ya mkuu zaidi ya yule.......

Nawaza tu
 
Kama hakuna faida binafsi na faida itaenda TRA basi wako sahihi
kuhusu kukiuka maagizo.....Rais sio mchumi mkuu wa taifa
masuala ya uchumi wao wanamsikiliza mchumi mkuu wa taifa
ndo maana board ina gavana wa BOT....

Magufuli hajui ABC za uchhumi hapaswi kusikilizwa kila anachoongea
wachumi wanajua kuwa hajui masuala ya uchumi ndo maana wanakiuka maagizo yake

Wewe ukiwa unaumwa utasikiliza maagizo ya baba yako mzazi ambae sio dokta
au utasikiliza maagizo ya daktari?
hii ni case tofauti kwani hao kina governor si ni washauri wa raisi kuhusu uchumi? wakati anatoa amri hakuna kuweka fedha huko mabenk ya biashara walikuwa wapi? si walikubaliana nae na ndo walizipokea BOT? inakuwaje tena waje wazihamishe kisirisiri?
 
Back
Top Bottom