TTCL yaomba bil.70/- kujiimarisha

PayGod

JF-Expert Member
Mar 4, 2008
1,259
57
TTCL yaomba bil.70/- kujiimarisha


CHAMA cha Wafanyakazi wa Sekta ya Huduma za Mawasiliano nchini (TEWUTA) kupitia Shirika la Simu (TTCL), kimeitaka serikali kulikopesha sh bilioni 70 kwa ajili ya kufufua utendaji wa shirika hilo la kizalendo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Katibu Mkuu wa Tewuta Junus Ndaro alisema kupatikana kwa kiasi hicho cha fedha kutakuwa suluhu ya TTCL kuanzisha miradi mbalimbali na kutoa huduma bora ya mawasiliano katika soko la ushindani wa makampuni mengi ya simu kutoka nje.
Alisema kukwama kwa shirika hilo kumetokana na hujuma iliyofanywa na makampuni ya kigeni dhidi ya TTCL ambayo yaliingia ubia kupitia wafanyakazi wasio wazalendo.
Ndaro alisema fedha hizo zitaendesha miradi ya kampuni hiyo nchi nzima kwa na kufanikisha uwepo wa mawsiliano nafuu na wananchi kuendelea kunufaika na huduma kutoka kwa wazalendo.
Alisema TTCL mwaka 2001 ilikuwa na sh bilioni 250 benki lakini baada ya utitiri wa makampuni ya simu ambayo hayana uwezo kuingia ubia na shirika hilo kulisababisha kutafunwa kwa fedha hizo na kuliacha shirika kuwa ombaomba.
"Tunaiomba dhamana serikali kuweza kukopa sh bilioni 70 kwa kuanzia ili kuweza kulisimamisha shirika letu kiutendaji zaidi kwa kutoa huduma bora kwa bei nafuu" alisema wakili huyo.
Alisema shirika hilo linashindwa kuendelea kutokana na wadeni wao kushindwa kulipa ikiwemo serikali ambayo inadaiwa sh bilioni tisa hivyo.
Ndaro alisema serikali inayo haja ya kuipa dhamana TTCL kuliko kuendelea kuilipa Dowans mabilioni ya fedha ambazo haziwezi kimsingi ni kumkandamiza mwananchi wa kipato cha chini.
"Ifike mahala Watanzania kuwa na uchungu wa kuendeleza shirika lao kuliko kuendelea kuwa na makampuni ya kigeni na kinyonyaji kwa walipakodi wa nchi hii" alisema Ndaro



Imefika wakati sasa TTCL , kufanya biashara kwa umakini, kwa mfano kama wakiamua kuwekeza kwenye internet service kiumakini zaidi watapata faida kubwa coz, wanamtandao mkubwa kuliko hata kampuni nyingine za simu.
 
Lakini it is obvious serikali haiwezi kuisapoti TTCL ili kui-nourish wakati akina king-maker wapo Voda ambao watakuwa direct competitors. Hapa ni kutwanga maji kwenye kinu.
 
Enzi za mashirika ya umma kubebwa na serikali kwa fedha za watanzania kila yanapofuja fedha zilikwishapita.
 
Enzi za mashirika ya umma kubebwa na serikali kwa fedha za watanzania kila yanapofuja fedha zilikwishapita.
Kaka nadhani wao wanaomba tu udhamini ili wakakope sijui wapi. Lakini still naona wanaeza kufanya biashara yenye faida na kueza kushusha bei ya huduma za data kwa ujumla nchini, ila hakuna political will ya kuwawezesha kufanya hivyo kutoka serikalini due to obvious reasons.
 
TTCL yaomba bil.70/- kujiimarisha


CHAMA cha Wafanyakazi wa Sekta ya Huduma za Mawasiliano nchini (TEWUTA) kupitia Shirika la Simu (TTCL), kimeitaka serikali kulikopesha sh bilioni 70 kwa ajili ya kufufua utendaji wa shirika hilo la kizalendo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Katibu Mkuu wa Tewuta Junus Ndaro alisema kupatikana kwa kiasi hicho cha fedha kutakuwa suluhu ya TTCL kuanzisha miradi mbalimbali na kutoa huduma bora ya mawasiliano katika soko la ushindani wa makampuni mengi ya simu kutoka nje.
Alisema kukwama kwa shirika hilo kumetokana na hujuma iliyofanywa na makampuni ya kigeni dhidi ya TTCL ambayo yaliingia ubia kupitia wafanyakazi wasio wazalendo.
Ndaro alisema fedha hizo zitaendesha miradi ya kampuni hiyo nchi nzima kwa na kufanikisha uwepo wa mawsiliano nafuu na wananchi kuendelea kunufaika na huduma kutoka kwa wazalendo.
Alisema TTCL mwaka 2001 ilikuwa na sh bilioni 250 benki lakini baada ya utitiri wa makampuni ya simu ambayo hayana uwezo kuingia ubia na shirika hilo kulisababisha kutafunwa kwa fedha hizo na kuliacha shirika kuwa ombaomba.
"Tunaiomba dhamana serikali kuweza kukopa sh bilioni 70 kwa kuanzia ili kuweza kulisimamisha shirika letu kiutendaji zaidi kwa kutoa huduma bora kwa bei nafuu" alisema wakili huyo.
Alisema shirika hilo linashindwa kuendelea kutokana na wadeni wao kushindwa kulipa ikiwemo serikali ambayo inadaiwa sh bilioni tisa hivyo.
Ndaro alisema serikali inayo haja ya kuipa dhamana TTCL kuliko kuendelea kuilipa Dowans mabilioni ya fedha ambazo haziwezi kimsingi ni kumkandamiza mwananchi wa kipato cha chini.
"Ifike mahala Watanzania kuwa na uchungu wa kuendeleza shirika lao kuliko kuendelea kuwa na makampuni ya kigeni na kinyonyaji kwa walipakodi wa nchi hii" alisema Ndaro



Imefika wakati sasa TTCL , kufanya biashara kwa umakini, kwa mfano kama wakiamua kuwekeza kwenye internet service kiumakini zaidi watapata faida kubwa coz, wanamtandao mkubwa kuliko hata kampuni nyingine za simu.

1. Kwanini wakopeshwe maana hili shirika na lenyewe kwa kufuja fedha nao wamo, there are others means za kupata hizo fedha not necessarily kutegemea serikali
2. Simuelewi anaposema "Imefika wakati sasa TTCL , kufanya biashara kwa umakini" so there were not serious at all.
 
Wasipewe, mbona mashirika binafsi tena madogo kulio yao yanajiendesha vizuri sana na hatuyasikii kufilisika tena yanakuwa haraka haraka. Juzi tu, tumeona kina Sasa tel, wakianza leo ni one of the players kwenye ligi ya mawasiliano.

Funga au uza hiyo. Same thing kwa Tanesco.
 
kama kampuni ya biashara ikope yenyewe bila msaada wa serikali, wao walichemka na mobile system yao ya cdma. nadhani ni suala la kibiashara na wakubali loss hiyo, wamekuja na product ngumu sijui wachina waliwalambisha au vipi.

wakope just like any other business entity and be accountable incase of failure, hili suala la kukimbilia serikalini kukopa itakuwa ATCL ya pili hii.
 
Libinafsishwe tu hili shirika .....apewe mtu aajiri wafanyakazi anaowahitaji, wafanyakazi waliopo sasa wengi wao kuanzia juu(CEO, etc ) mpaka chini hawana work attitude nzuri kuweza kufanya kazi kwenye soko la ushindani.
 
Unaposema wakope benki kweni wewe wamekuambia wanaikopa serikali.... Unaona poa kuilipa dowans .....
 
Acha wafe tuu wengine watakuja,hakuna haja ya kulea wazembe...TANESCO nayo ife tuu ndio mwanzo wa matatizo yote ya umeme TZ!
 
Kwa serikali ya sasa iliyopo madarakani bora tu life kupitia 'natural death' kwanza serikali yenyewe kama ailipi bills zake maana yake inachangia kulimaliza shirika. Not to mention ma CEO wa Tanzania kwenye haya mashirika ya Umma naona hawana tofauti na mawaziri kiutendaji (ili mradi kusema kuna kiongozi) maendeleo patupu na wala sidhani kama kuna mtu anajali mafanikio ya hawa viongozi.

Mashirika ya Umma yanakufa wakati yana monopoly kwenye market only in Tanzania, Kwa stahili safari yetu ni ndefu.
 
Kwa serikali ya sasa iliyopo madarakani bora tu life kupitia 'natural death' kwanza serikali yenyewe kama ailipi bills zake maana yake inachangia kulimaliza shirika. Not to mention ma CEO wa Tanzania kwenye haya mashirika ya Umma naona hawana tofauti na mawaziri kiutendaji (ili mradi kusema kuna kiongozi) maendeleo patupu na wala sidhani kama kuna mtu anajali mafanikio ya hawa viongozi.

Mashirika ya Umma yanakufa wakati yana monopoly kwenye market only in Tanzania, Kwa stahili safari yetu ni ndefu.

Kaka ndio hapo watu tunashindwa kuelewa. Shirika kama Tanesco linawezaje kuwa mahututi wakati kuna demand kubwa ya umeme, watu wanafuatilia miezi kueza kuunganishwa? Haya na hawa TTCL, ok fine wanacompetition kwene cellular...lakini wana edge kubwa sana kwene network kama watafanya biashara ya data, mambo ya internet na pengine hata cabled TV mambo ya HDTV etc etc.

Sababu kubwa ya kufeli kwa haya mashirika ni kwamba hakuna system ya kueleweka ya utendaji na utawala na wajanja wachache wanatumia udhaifu huo kujinufaisha. Hakuna nia ya dhati ya kuyafanya haya makampuni yajiendeshe kwa faida, yawe totally autonomous na yaweze pengine kujiweka kwene soko la hisa na kuuza shares. Ni serikali ya Tz ni kituko kikubwa.
 
Tatizo kubwa la ttcl ni ukosefu wa serikali makini ktk kusimamia mashirika ya umma. Ttcl ibinafsishwee kimakini harakaa sana,pawepo uongozi wenye maono ya kibiashara na liingie dse baadae tununue hisa,period. Ugonjwa wake ni sawa na akina atcl,trl,tpa,tpb nk.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom