Kima mdogo
JF-Expert Member
- Sep 17, 2011
- 303
- 46
Wanandoa hawa walikutana na wakiwa na hali duni kimaisha, wakaoana na kujaliwa kupata mtoto 1 wakike. Kadiri siku zilivyoenda MUNGU akawajalia wakafanikiwa kimaisha na wanamiliki mali kadhaa. Miaka 7 ikapita mke akabeba mimba kwa bahati mbaya mimba ikatoka, akamweleza mama mkwe wake hapo ndo matatizo yalipoanza. Mama mkwe na Mume wakaanza kumsengenya kuwa hazai. Mama mkwe akafikia hatua ya kusema mwanae aoe mwanamke mwingine. Mke akawa analia na Mungu kila siku,Siku 1 mama mkwe akaja akamkuta mke huyo anaumwa akasema wala haumwi ni mamizimu ya huko kwao,huyu dada aliumia sana kwani hajui uchawi wala mizimu akamweleza mumewe maneno aliyoongea mama yake, mume kumuuliza mama yake akakataa katakata na kudai kuwa mwali wake kamsingizia ili asije kwa mwanae, kwa bahati nzuri Mke akapata ujauzito mume wake akaanza kumnyanyasa, kumtukana na kumnyima hela ya matibabu kwa shinikizo la mama yake kuwa alimsingizia, pia mama huyo akasema huyo mtoto hatazaliwa ng'o, kwa ufupi Mume na mama yake waliungana kumnyanyasa mwanamke(mke).
Mke yule akawa anaomba Mungu na kumwambia mumewe kuwa ni kweli mama yake amemwambia yy ni mchawi na anamauvimbe hazai lakini mume hakumwelewa na manyanyaso yakaendelea,mke akapata matatizo makubwa ikabidi madaktari wampasue wamtoe mtoto wa miez 7 kwani alinyongwa na kitovu karibu afe. Wiki 3 baada ya kujifungua mama mkwe akaja akamwambia niletee mtoto nimkague nataka niondoke,yule mke akashindwa kumpa mtoto akamwambia mumewe aje ampe yeye,mume hakuja na mama akaondoka,siku zikapita yule mume akamwambia mkewe kw hataki mtoto mke akamwambia atawajibia kumlea mwenyewe,ikabidi baba wa kijana aingilie kati na kumuonya kijana wake kuwa mama yk anapenda kuongea uongo na kukana hivyo asimnyanyase mke wake,kijana akakurupuka akaongea uongo kuwa mke wake amemuita mama yake mbwa,kwakweli mke yule aliumia sana akawa anafunga na kuomba Mungu,miez 2 baadae yule mama akaanza kuumwa kupima akakutwa na uvimbe kwenye kibofu na presha na sasa anaumwa sn,je nani anamakosa na nini kifanyike? Ushaur please
Mke yule akawa anaomba Mungu na kumwambia mumewe kuwa ni kweli mama yake amemwambia yy ni mchawi na anamauvimbe hazai lakini mume hakumwelewa na manyanyaso yakaendelea,mke akapata matatizo makubwa ikabidi madaktari wampasue wamtoe mtoto wa miez 7 kwani alinyongwa na kitovu karibu afe. Wiki 3 baada ya kujifungua mama mkwe akaja akamwambia niletee mtoto nimkague nataka niondoke,yule mke akashindwa kumpa mtoto akamwambia mumewe aje ampe yeye,mume hakuja na mama akaondoka,siku zikapita yule mume akamwambia mkewe kw hataki mtoto mke akamwambia atawajibia kumlea mwenyewe,ikabidi baba wa kijana aingilie kati na kumuonya kijana wake kuwa mama yk anapenda kuongea uongo na kukana hivyo asimnyanyase mke wake,kijana akakurupuka akaongea uongo kuwa mke wake amemuita mama yake mbwa,kwakweli mke yule aliumia sana akawa anafunga na kuomba Mungu,miez 2 baadae yule mama akaanza kuumwa kupima akakutwa na uvimbe kwenye kibofu na presha na sasa anaumwa sn,je nani anamakosa na nini kifanyike? Ushaur please