Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,466
- 113,551
Wanabodi
Leo saa 11:30 alfajiri nimepokea simu ya Da Mwajuma Mchuka kunijulisha kuhusu huu msiba!.
Hii ni thread ya Tribute kuhusu nilivyomfahamu marehemu, Halima Mchuka.
Kwanza jikumbushe sauti yake
Video kwa hisani ya Aboubakar Liongo.
Pia Baadhi ya Tasirwa mbalimbali za Halima Mchuka
My Tribute To Halima Mchuka!
Halima Mchuka alipoajiriwa RTD, batch yangu ndiyo iliwatangulia!. Ilitokea tuu huyu dada tukawa tulielewana sana na alikuja kutokea kuwa ni mtu wangu wa karibu!.
Wakati huo akiishi na dada yake anayefanya kazi ATC, Mwajuma Mchuka sisi tukimwita kwa kifupi Da Mwajuma. Da Mwajuma alikuwa anamiliki flat ya familia mbili hapo Ilala Shariff Shamba nyumba ya pili kutoka lile ghorofa refu pale kituo cha Bungoni.
Wakati huo mimi nikiishi Mikocheni, kwa Wazazi, na kufuatia umbali kati ya RTD Pugu Rd (Sasa Nyerere Rd) na Mikocheni enzi hizo lazima upande mabasi matatu.
Kwanza utoke Mikocheni na upandishe kwa miguu njia ya TPDC mpaka kituo cha Maji Machafu (siku hizi Sayansi), pale ndio upande gari ya Mwenge Kariakoo ushuke Magomeni. Upande gari ya Ilala Drive-In ushuke Ilala Boma, upande gari ya Buguruni Kariakoo, ushuke Buguruni kisha utembee kwa miguu mpaka Tazara ndipo uingie ofisini jengo la BH!.
RTD walikuwa na basi moja la wafanyakazi route yangu basi hilo, halipiti, hivyo mimi nilikuwa ni mtu wa kuchelewa kufika kazini kila siku ambazo sikuwa zamu. Siku ukiwa zamu, unafuatwa na gari mpaka nyumbani.
Kufuatia kuchelewa huko, Halima Mchuka akanishauri kwanini nisihame nyumbani na kuhamia eneo la karibu na kazini?. Akasema kama vipi azungumze na dada yake, Da Mwajuma, aniruhusu nitumie chumba kimoja kwenye flat yao ambayo ni two in one, ina vyumba 4 vya kulala, na wao wako watatu, yeye, Halima Mchuka, dada yake Da Mwajuma Mchuka na mdogo wake Rehema, Rehema Mchuka!.
Da Mwajuma alikubali ombi la mdogo wake Halima hivyo mimi nikakaribishwa rasmi Ilala na huo ndio ukawa mwanzo wangu wa maisha ya kujitegemea!.
Asante sana Halima Mchuka kunifungulia milango ya maisha ya kujitegemea!.
Wakati nikiishi hapo yeye na Da Mwajuma walinichukulia kama mwanafamilia, sikuwahi kupika, kufanya usafi au kuosha vyombo, niliishi kama hotelini!. Asante sana Halima Mchuka kwa yote!.
Baada ya kipindi kifupi, Da Mwajuma alihamia kwenye nyumba yake Masaki hivyo kutuachia flat lote zima la two apartments za two bedrooms each, mimi na Halima, ndipo Halima akachukua upande wake na mimi upande wangu ambapo nami nikamkaribisha mtangazaji mwenzangu Aboubakar Liongo, tukiishi maisha ya ujana.
Tuliishi vizuri tuu akaanza Halima kuolewa na Nasoro Mkupama, na kuishi na mumewe kule upande wake, nikafutia mimi nikaoa hapo hapo familia ilipoanza kuwa kubwa, mimi nikahama na kumuchia Abou ambaye nae aliolea hapo hapo!.
Halima ameacha mume, watoto watatu, Amina, Yekini na Prince Naseem.
Thanks a Millions Halima Mchuka, Mungu Aiweke Roho yako mahala pema peponi.
RIP Halima Mchuka!.
Pasco.
Update Two.
Mwili utaswaliwa msikiti wa Muhimbili saa 3:30 asubuhi na maziko yatafanyika makaburi ya Msasani.
Update 3.
Leo asubuhi, Mwili wa Halima Mchuka, umeswaliwa katika msikiti wa Muhimbili na kuagwa na umati mkubwa wa waombolezaji ukiongozwa na rais Jakaya Kikwete, mkuu wa mkoa wa DSM, mawaziri, wabunge, likiwemo kundi kubwa la wanahabari.
Msafara kuelekea mazikoni makaburi ya Msasani ukafuatia na hatimaye kuzikwa na umati mkubwa wa watu.
Halima Mchuka pata pumziko la milele...
Amen.
Final Update.
Familia ya Mchuka wa Dar es Salaam, pamoja na ndugu wote walioko Miono na Kibindu-Bagamoyo, wanatoa shukrani za dhati kwa wote mlioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kipindi kigumu cha msiba wa mpendwa wao, Halima Mohamed Mchuka uliotokea tarehe 29/12/2011 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuzikwa tarehe 30/12/2011 katika makaburi ya Msasani Dar es Salaam.
Shukrani za pekee ziwaendee, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo,Mhe. Dkt.Emanuel Nchimbi, Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto, Mhe. Sofia Simba, Naibu Waziri wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo,Mhe. Dkt. Fenella Mukangara, Waheshimiwa wabunge wa Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam, IGP, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam na Mstahiki Meya wa Ilala.
Shukrani nyingine ziwaendee viongozi na wafanyakazi wa TBC wakiongozwa na M/Kiti wa Bodi ya TBC, Wilfred Nyachia na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Clement Mshana, wafanyakazi wastaafu wa RTD, wafanyakazi wa kampuni ya Ndege Tanzania, Madaktari na wauguzi wa hospitali za Dar Group na Muhimbili, viongozi wa vyama vya michezo, waandishi wa habari na watangazaji wa vyombo mbalimbali vya habari, Uongozi wa CCM Wilaya ya Bagamoyo, BAMITA, majirani wa Karakata, Msasani, Mabibo na Mbezi, pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wote wa familia ya MCHUKA wa ndani na nje ya nchi. Tunawaomba mpokee shukrani zetu za dhati kwa kutufariji kufuatia kifo cha HALIMA MCHUKA.
Arobaini ya Marehemu itafanyika Miono Bagamoyo siku ya Ijumaa Tarehe 3/02/2012 kuanzia saa 11:00 jioni na Hitma itasomwa Jumamosi ya Tarehe 04/02/2012 saa 3 :00 asubuhi.Nyote mnakaribishwa.
Kwa taarifa zaidi wasiliana na wanafamilia moja kwa moja au kupitia simu namba 0713477790 au 0784737253.Karibuni.
INNA LILLAH WAINNA ILAYHI RAAJIUN
Leo saa 11:30 alfajiri nimepokea simu ya Da Mwajuma Mchuka kunijulisha kuhusu huu msiba!.
Hii ni thread ya Tribute kuhusu nilivyomfahamu marehemu, Halima Mchuka.
Kwanza jikumbushe sauti yake
Video kwa hisani ya Aboubakar Liongo.
Pia Baadhi ya Tasirwa mbalimbali za Halima Mchuka
My Tribute To Halima Mchuka!
Halima Mchuka alipoajiriwa RTD, batch yangu ndiyo iliwatangulia!. Ilitokea tuu huyu dada tukawa tulielewana sana na alikuja kutokea kuwa ni mtu wangu wa karibu!.
Wakati huo akiishi na dada yake anayefanya kazi ATC, Mwajuma Mchuka sisi tukimwita kwa kifupi Da Mwajuma. Da Mwajuma alikuwa anamiliki flat ya familia mbili hapo Ilala Shariff Shamba nyumba ya pili kutoka lile ghorofa refu pale kituo cha Bungoni.
Wakati huo mimi nikiishi Mikocheni, kwa Wazazi, na kufuatia umbali kati ya RTD Pugu Rd (Sasa Nyerere Rd) na Mikocheni enzi hizo lazima upande mabasi matatu.
Kwanza utoke Mikocheni na upandishe kwa miguu njia ya TPDC mpaka kituo cha Maji Machafu (siku hizi Sayansi), pale ndio upande gari ya Mwenge Kariakoo ushuke Magomeni. Upande gari ya Ilala Drive-In ushuke Ilala Boma, upande gari ya Buguruni Kariakoo, ushuke Buguruni kisha utembee kwa miguu mpaka Tazara ndipo uingie ofisini jengo la BH!.
RTD walikuwa na basi moja la wafanyakazi route yangu basi hilo, halipiti, hivyo mimi nilikuwa ni mtu wa kuchelewa kufika kazini kila siku ambazo sikuwa zamu. Siku ukiwa zamu, unafuatwa na gari mpaka nyumbani.
Kufuatia kuchelewa huko, Halima Mchuka akanishauri kwanini nisihame nyumbani na kuhamia eneo la karibu na kazini?. Akasema kama vipi azungumze na dada yake, Da Mwajuma, aniruhusu nitumie chumba kimoja kwenye flat yao ambayo ni two in one, ina vyumba 4 vya kulala, na wao wako watatu, yeye, Halima Mchuka, dada yake Da Mwajuma Mchuka na mdogo wake Rehema, Rehema Mchuka!.
Da Mwajuma alikubali ombi la mdogo wake Halima hivyo mimi nikakaribishwa rasmi Ilala na huo ndio ukawa mwanzo wangu wa maisha ya kujitegemea!.
Asante sana Halima Mchuka kunifungulia milango ya maisha ya kujitegemea!.
Wakati nikiishi hapo yeye na Da Mwajuma walinichukulia kama mwanafamilia, sikuwahi kupika, kufanya usafi au kuosha vyombo, niliishi kama hotelini!. Asante sana Halima Mchuka kwa yote!.
Baada ya kipindi kifupi, Da Mwajuma alihamia kwenye nyumba yake Masaki hivyo kutuachia flat lote zima la two apartments za two bedrooms each, mimi na Halima, ndipo Halima akachukua upande wake na mimi upande wangu ambapo nami nikamkaribisha mtangazaji mwenzangu Aboubakar Liongo, tukiishi maisha ya ujana.
Tuliishi vizuri tuu akaanza Halima kuolewa na Nasoro Mkupama, na kuishi na mumewe kule upande wake, nikafutia mimi nikaoa hapo hapo familia ilipoanza kuwa kubwa, mimi nikahama na kumuchia Abou ambaye nae aliolea hapo hapo!.
Halima ameacha mume, watoto watatu, Amina, Yekini na Prince Naseem.
Thanks a Millions Halima Mchuka, Mungu Aiweke Roho yako mahala pema peponi.
RIP Halima Mchuka!.
Pasco.
Update 1.
Msiba wa Halima Mchuka, upo nyumbani kwa dada yake mkubwa Mwajuma Mchuka, Mbezi Beach nyuma ya maghorofa ya BOT.
Mazishi ni kesho saa 5 asubuhi katika makaburi ya Msasani. Mwili utaswaliwa katika msikiti wa Msasani kabla ya swala ya Ijumaa.
Chanzo cha kifo ni shinikizo la damu. Jana mchana alitangaza kipindi cha salaam za mchana TBC-Taifa na inasemekana alitangaza vizuri ajabu!. Kitu cha ajabu jana aliwatumia sms wanae wawili waliopo nchini, na kuwaambia wamsikilize akitangaza akawaambia na muda. Masikini kumbe ndio kama kuwaaga kiaina kwa kuwaambia waisikilize sauti yake kwa mara ya mwisho!. Mara baada ya kipindi ndipo pressure ikampanda, akakimbizwa pale hospitali ya Dar Group na baadae Hospitali ya Taifa ya Muhimbili mauti yalipomkuta!.
Update Two.
Mwili utaswaliwa msikiti wa Muhimbili saa 3:30 asubuhi na maziko yatafanyika makaburi ya Msasani.
Update 3.
Leo asubuhi, Mwili wa Halima Mchuka, umeswaliwa katika msikiti wa Muhimbili na kuagwa na umati mkubwa wa waombolezaji ukiongozwa na rais Jakaya Kikwete, mkuu wa mkoa wa DSM, mawaziri, wabunge, likiwemo kundi kubwa la wanahabari.
Msafara kuelekea mazikoni makaburi ya Msasani ukafuatia na hatimaye kuzikwa na umati mkubwa wa watu.
Halima Mchuka pata pumziko la milele...
Amen.
Final Update.
HALIMA M. MCHUKA (18 Mar.1967- 29 Dec. 2011)
Familia ya Mchuka wa Dar es Salaam, pamoja na ndugu wote walioko Miono na Kibindu-Bagamoyo, wanatoa shukrani za dhati kwa wote mlioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kipindi kigumu cha msiba wa mpendwa wao, Halima Mohamed Mchuka uliotokea tarehe 29/12/2011 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuzikwa tarehe 30/12/2011 katika makaburi ya Msasani Dar es Salaam.
Shukrani za pekee ziwaendee, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo,Mhe. Dkt.Emanuel Nchimbi, Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto, Mhe. Sofia Simba, Naibu Waziri wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo,Mhe. Dkt. Fenella Mukangara, Waheshimiwa wabunge wa Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam, IGP, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam na Mstahiki Meya wa Ilala.
Shukrani nyingine ziwaendee viongozi na wafanyakazi wa TBC wakiongozwa na M/Kiti wa Bodi ya TBC, Wilfred Nyachia na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Clement Mshana, wafanyakazi wastaafu wa RTD, wafanyakazi wa kampuni ya Ndege Tanzania, Madaktari na wauguzi wa hospitali za Dar Group na Muhimbili, viongozi wa vyama vya michezo, waandishi wa habari na watangazaji wa vyombo mbalimbali vya habari, Uongozi wa CCM Wilaya ya Bagamoyo, BAMITA, majirani wa Karakata, Msasani, Mabibo na Mbezi, pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wote wa familia ya MCHUKA wa ndani na nje ya nchi. Tunawaomba mpokee shukrani zetu za dhati kwa kutufariji kufuatia kifo cha HALIMA MCHUKA.
Arobaini ya Marehemu itafanyika Miono Bagamoyo siku ya Ijumaa Tarehe 3/02/2012 kuanzia saa 11:00 jioni na Hitma itasomwa Jumamosi ya Tarehe 04/02/2012 saa 3 :00 asubuhi.Nyote mnakaribishwa.
Kwa taarifa zaidi wasiliana na wanafamilia moja kwa moja au kupitia simu namba 0713477790 au 0784737253.Karibuni.
INNA LILLAH WAINNA ILAYHI RAAJIUN