Treni ya umeme inakuja July 2017

Huwa ninafurahishwa sana na optimism ya JPM anapozungumzia miradi mikubwa "FEDHA IPO"- lakini ukichimbua kwenye bajeti ya serikali huoni hiyo helaimetengwa wizara gani na kwenye kifungu kipi?
Pesa anajua yy cos n rais mkuu
 
Yote anayoyasema Rais J.P.M. yanawezekana kwa asilimia 70. Kinachotusumbua watanzania ni hali ya kujiona hatutaweza na kujiviisha umasikini kwa kufuata yale tu tulioambiwa na waliotutangulia na hasa wakoloni.Utasikia mtanzania anasema wazi wazi hata kabla hajatafakari kuwa: "sisi ngozi nyeusi hatuna tunaloliweza" au "sisi watanzania bado sana" hii utaisikia hata katika mambo ambayo tunaweza kufanya wenyewe.Ukiangalia maliasilia ya nchi hii ambazo hazijatumika kabisa kuzalisha mali ni nyingi kuliko zile tunazozitumia hivi sasa tena kwa kiwango cha chini kabisa.Mali zetu nyingi hazisimamiwi vizuri na hivyo kuwafaidisha wachache waliominiwa kuziendesha.Ufisadi,uzembe, kutokujali, masihara ndio yanayotugharimu na kushindwa kupiga hatua. Mimi naamini sana kuwa iwapo JPM ataendelea hivi bila kulegeza kamba, na hasa akizidisha usimamizi zaidi na kuwaadhibu wazembe wachache wanaotuharibia kama mchwa,nathubutu kusema miaka yake mitano ikiisha tutakuwa na maendeleo makubwa ambayo wengi wanayaona kama hayawezekani.
 
Ndani ya miezi 11 tu kishaongeza deni la taifa kwa 55.8% toka 43 Trillioni hadi kufikia 67 Trillion. Kwa mwendo huu wa kukurupuka na one man show government mpaka 2020 deni la Taifa linaweza kufika 250 Trilioni. Tanzania ya Magufuli AKA mtakatifu wa Ikulu Tanzania ya kukurupuka na mwendo kasi.
 
ahadi zinaendelea sijui kampeni hazijaisha bado? tuliambiwa fly over ikaja njia sita ikaja reli ya standard gauge,zote zimebaki kwenye makaratasi yao na miaka inakwenda kasi tu
Miaka inazd kwenda kwan rais tangu ateuliwe anamiaka mingap madarakan,?ukpata jibu jiulze n mangap katekleza kwa muda aliokaa madarakn?
 
  • Thanks
Reactions: MC7
06c1b297e3102cc648160f084c31ec22.jpg



Throwback thursday
Kipindi hicho n cha madaraka ya mipasho sasa hv n hapa kaz tuu....
 
Watu wana hofu tu. Kujenga treni ya umeme haichukui muda mrefu siyo gharama kubwa. Serikali inaweza jenga under PPP law. Ulaya ni vitu vya kawaida. You must think big.Nampongeza JPM ktk hili. It is very possible kutekelezwa. Maendeleo ni kuthubutu(to dare). Ukiwa na hofu huwezifanya jambo la maendeleo.
Saaana....
 
Mwambieni aboreshe maisha ya mkulima na mfugaji! Miji ya kisasa na flyovers wakati wananchi wengi tuko vijijini na kilimo tunapiga lakini mtandao Wa soko hakuna,na usafiri ni shida? Kama mnatujali maskini na mnataka nchi tuifaidi wote msisitizo/kipaumbele kikubwa kiwe kubadili maisha ya mtanzania wa kijijini. Tujenge kwa bei nafuu,tukopeshwe na benki sio madalali,tupewe ruzuku kwa wakati na yakutosha bila urasimu,tupunguziwe kodi kwenye zana za kilimo,tutengenezewe mfumo Wa kilimo cha umwagiliaji,kuwe na afsa masoko wilayani Wa kutushauri tuuze wapi bidhaa zetu(iwe ndani ama nje ya nchi),barabara vijijini zipitike.
Navoona badala ya fly overs bora tutengeneze kwanza miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji! au sababu hiyo haitotujenga kisiasa? Rais pia atutembelee vijijini,ranch za mifugo,mashamba nk. nikama kajali sana ya mambo ya mujini...dayamondi platinamu ndio anatakiwa abaki mjini tuu( nmeona nichomekee kidogo)
 
Umeme upo wapi bana?

Hata likijengwa ni kwa ajili ya kujitangaza kisiasa tu si kutatua matatizo ya wananchi.

Amini usiamini, nimeomba niingiziwe umeme katika mashine ya kusaga. Kila kitu kimeshapita na nimeshalipia, leo hii ni mwezi wa pili sijaingiziwa umeme, kisa eti waya za 3 phase hazipo. Naendelea kusubiri. Pazuri hapo!!!!!!!!

Mkuu naona mleta mada akuelewa Rais alicho maanisha kuhusu suala la train alimaanisha train ya Diesel Electric yaani engine ya Diesel ni prime mover ya kuzungusha genereta ya umeme alafu umeme unapelekwa kwenye magurudumu ya train magurudumu yenyewe ni DC Motors (Traction motors)

Train ambazo zinatumia umeme wa grid zipo, lakini kwa Tanzania hiyo tutasubiri sana mpaka pale miundo mbinu ya umeme nchini itakapo kaa sawa.
 
naweza kuja ila sio kwa muda huo ya mafuta tuu imetusumbua miundo mbinu ya hiyo kitu inataka muda sio ujanja ujanja... Gautren kipande kidogo tuu Pretoria Airport na Johannesburg walitumia miaka miaka mitatu.. sasa hiyo ya mwakani july zitakuja zikae godown au...
 
Back
Top Bottom