Michael Amon
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 8,775
- 3,610
Katika hali ya kushangaza treni la Kampuni ya Reli (TRL) iliyokuwa ikitoka Mpanda kuelekea Tabora Machi 23 mwaka huu, iliishiwa wese (mafuta) katikati ya pori na kuwaweka roho juu abiria waliokuwa wakisafiri.
Akizungumzia tukio hilo Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Athumani Mfutakamba alisema kitendo kilichofanyika ni cha kinyama na hakikubaliki katika utendaji wa kazi za shirika hilo na kwamba wamejipanga kuhakikisha matatizo kama hayo hayatokei tena.
Alisema kwamba haiingii akilini treni kuishiwa mafuta njiani wakati bajeti ya mafuta inajulikana.
Tayari watumisho watatu akiwemo dereva wa treni wa Kampuni ya Reli (TRL), wamesimamishwa kazi katika sakata la kusababisha treni ya abiria kusimama porini baada ya kuishiwa mafuta.
Mhandisi wa TRL, Muungani Kaupunda alithibitisha hilo.
E-mail: meezy@youngmaster.co.tz