Travelling vp; makamu wa rais dkt bilal afanya mahojiano na mtangazaji wa un redio new york

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na mtangazaji wa Redio ya Umoja wa Mataifa (UN) Flora Nducha wakati mtangazaji huyo alipofika kwa ajili ya kufanya mahojiano naye kuhusu maudhui ya mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Ukimwi uliofanyika jijini New York, na unatarajiwa kumalizika leo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiwa katika mahojiano na mtangazaji wa Redio ya Umoja wa Mataifa (UN) Flora Nducha muda mfupi baada ya kuhudhuria mkutano wa majadiliano kuhusu masuala ya ukimwi ulioandaliwa na Umoja wa Mataifa unaofanyika jijini New York leo. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa na baadhi ya viongozi wenzake kutoka nchi mbalimbali wakati akishiriki mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Ukimwi unaofanyikajijini New York jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiwa katika picha ya pamoja na mshauri Mkuu wa ufundi na Asasi ya Viongozi wa Afrika inayohusika na vita dhidi ya Malaria Dkt. Melanie Renshaw (wa pili kulia) na Balozi wa Tanzania wa Umoja wa Mataifa Ombeni Sefue (kulia) na Mkurugenzi wa Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa inayohusika na vita dhidi ya Malaria Saleemah Abdul-Ghafur (kushoto) wakati walipomtembelea Makamu wa rais jijini New York Juni 9 na kufanya mazungumzo. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Tacaids Dkt. Fatma Mrisho (kushoto) na Mkurugenzi wa Tume ya Ukimwi Zanzibar Dkt. Omari Shauri (kulia) wakati walipomtembelea Makamu wa rais jijini New York Juni 9 na kufanya mazungumzo..(Picha na Muhidin Sufiani-OMR).
 
Back
Top Bottom