Mombo Wetu
JF-Expert Member
- Aug 5, 2008
- 377
- 36
Pasco, it was never a joke. It is not an easy thing to start a party simply by saying tunataka uing'oa CCM. Chama ni lazima kiwe na taswira ya namna yake ambayo itakitofautisha na na wengine wote.
Wengi hapa wanakimbilia kusema kuwa na Itikadi na Sera si za msingi, wanasahau kuwa bila kuwa na utambulisho na imani ya kinachoeleweka, si rahisi kujenga political base kwa Tanzania. Ama kila mtu analenga kwenye short term goals, kuing'oa CCM, lakini hawafikirii beyond kuing'oa CCM na kitakachotokea baada ya kuing'oa CCM!
Kama miaka 20 ya Upinzani haijatupa funzo la kujifunza na kuelewa kuwa bila kuwa na Itikadi na Sera zinazoeleweka, kamwe huwezi kuwa na mvuto au uwezo wa kuleta mshikamano wa kuiondoa CCM.
Leo hii kila mwaka wa uchaguzi, vyama viliyoko vinapigana vikumbo kugombania nani ana mgombea maarufu zaidi ili kuchukua jimbo au urais. Wamekaa chini mara kadhaa kutaka kujenga ushirika, lakini wameuvunja na kununiana.
Turudi pale ilipoanzishwa NCCR, kila mtu alikuwa huko, lakini kutokana na kila mtu kuwa na fikra na mtazamo wake na badala ya kujenga mfumo, itikadi, sera na taswira moja na wote kushikamana, chama kika sambaratika!
Leo hii hatuwezi kuing'oa CCM ambayo inajiita Chama cha Kijamaa na kukimbilia kuingia madarakani kumfunga Mkapa, Rostam, Lowassa au mafisadi, kisa wananchi tumechoka kunyanyaswa na kuonewa.
Hatuwezi kuwa na uimara ilhali CCM bado ni chama kilichojijenga kisera na kiitikadi ndani ya Watanzania na ni rahisi sana kwa CCM kurudi madarakani katika muda mfupi sana na kuwafanya Wapinzani waonekane wajinga machoni pa Watanzania.
Kuiangusha CCM, si watu wawili ambao wanaisumbua nchi, inapaswa kuingia na nguvu za kuhakikisha CCM inashindwa kihoja, kisera na kiitikadi. Leo tukishawafunga kina Lowassa je tutakifuta CCM usajili au kudai tukitaifishie mali zake kukivunja nguvu? Kama kuna mawazo kama hayo ni dhahiri basi sisi hatuna tofauti na CCM.
Wanapodai CCM inawenyewe, ingawa kwa dhihaka tunawatukana kuwa ni mafisadi, lakini wenye CCM bado ni wananchi na kuna kundi kubwa sana la wafuasi wa CCM ambao ni safi na ni rahisi kwa wao kujipukut mavumbi baada ya kuanguka na kujijenga upya na kuwa Chama mbadala!
Tusikimbilie kuing'oa CCM au kukimbilia Ikulu kisa eti tutaondoa onyonge wa Mtanzania kwa siku mmoja! Tusisahau kuwa iwehe vile, katika miaka 25 ijayo, CCM inauwezo wa kuwa na asilimia 45-70 ya viti vya Bunge, na hiki ni chama kimoja tu, tofauti na vyama vingine ambavyo vitapaswa kujikusanya viti viwili vitatu ili vipate umoja wenye nguvu huku kati yao hawaaminiani!
Kule kwenye hoja ya Mtei, Shalom kanipa majibu kuwa mwaka huu, kati ya viti karibu 400 vya ubunge, CHADEMA inatarajia kupata viti 70, ambayo ni asilimia 17, CUF nao labda watapata idadi hiyo hiyo hivyo kuwafanya jumla yao kua kiwango kidogo sana juu ya theluthi moja.
HIvyo miswaada yote ikija Bungeni, bado CCM itaipitisha na kuiburuza, na tusisahau kuwa CCM imeshaanza kujianda kujisuka upya na kujijenga kwa uchaguzi wa 2015 na si huu wa mwaka huu tena.
Wakati nimeandika PPPT, nilitamka wazi lengo si kukimbilia uchaguzi mkuu au kuwa na malengo ya muda mfupi ambayo hayana matunda ya kudumu bali ni kujenga chama imara ambacho kitaanzia kwenye vijijiji, na kuishi na Watanzania katika kila ngazi na kadri matunda ya mahusiano yetu yatakavyokuwa yakiongezeka, ndivyo basi uimara utakapoongezeka na kutufikisha kwenye lengo la kuomba dhamana ya kuwaongoza Watanzania.
CCM inayoogopa CCJ, si Chama bali ni kundi la watu wachafu waliokichafua Chama kwa matakwa binafsi na kukitumia Chama na dhamana ya kuongoza nchi kwa maslahi binafsi na hivyo kuendekeza Uhujumu na utawala mbovu.
Sisi tunapaswa kuwaogopa wale CCM makini ambao wanajijenga kimywa kimya kuchukua hatamu za Chama chao, hawa ni wale vijana kati ya miaka 18-45, ambao wamesha kula yamini ya Ujamaa na Kujitegemea na si hawa wa miaka 50-80 ambao wameshaloea utamu wa madaraka na wameshindwa kumkomboa Mtanzania kutoka Umasikini, Ujinga na Maradhi.
It is all about strategy na hili ni wazi kama watu kam CHADEMA wakiwaachia kina Mnyika na Zitto ambao ni vijana wakawa Sauti kuu na nguvu ya Chama, itakuwa ni rahisi sana kwa CHADEMA na hata CUF kuweza kupata nguvu kubwa na ufuasi wa kweli kwenye sanduku la kura.
Rev thanks kwa maelezo yako lakini mimi natatizo dogo tu katika hili jambo la CCM unayoiongelea hasa hapo kwenye red colour; hivi CCM bado ni CCM ya 1977 pale ilipo anzishwa kiitikadi au ndo imebaki kama ilivyo leo CRDB bank kwamba si ile iliyoanzishwa by then kwaajili ya rural development ila imebakia nembo tu kwaajili ya kuvuta wateja? Why I ask this kama CCM bado kipo kiitikadi kama ilivyo kuwa 1977 yaani zile alama mbili ya jembe na nyundo kwa maana halisi basi I dont need CCJ lakini mimi ninachokiona CCM is more of the last words in red colour na wana waandaa hao unaowaita vijana kukomaza hiyo itikadi yao ndo maana nashindwa kuitetea CCM popote pale kama ambavyo ningependa kufanya hivyo IFF it would have been that of 1977 kiitikadi.