Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Mzee Mwanakijiji,
Kama kuna kituko cha Kisiasa na Uchanga (ndio natumia herufi kubwa kama msisitizo) ambacho kimetokea Tanzania na mchakato wa Siasa, ni vuguvugu la kuanzishwa kwa CCJ na matokeo yaliyotokea sasa hivi ambapo wamekosa usajili na kila Chama cha Upinzani unawaangukia na kuwaomba wajiunge kwao.
Kwangu mimi nasema hivi, ilikuwa ni kosa kubwa sana kwa CCJ kukimbilia kutaka kusajiliwa ili kishiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu kutokana na sababu kuu moja: CCJ kuwa chama kimbilio kwa wale ambao wanatarajia kutemwa na CCM na ambao wanaona aibu kuingia vyama vingine au kula matapishi yao ya kudharau haki za msingi za Uraia kama vile kuundwa kwa katiba mpya au kukemea uchafu ulioko ndani ya CCM.
CCJ walikuja kwa kujiamini sana, lakini kasi yao ilinitia shaka hasa kung'angania kusajiliwa ili kishiriki Uchaguzi Mkuu. Inawezekana kina Itikadi ambayo ni ya mkono wa kushoto wa siasa kali, lakini badala ya kukijenga chama (kama vile Mchungaji anavyotaka kuanzisha PPPT) kuanzia vijijini na kusambaza moto wa CCJ unaoambatana na Itikadi na Sera ambazo ni tofauti na CCM, CCJ waliingia kichwa kichwa mtego ule ule wa kukimbilia kutaka kuing'oa CCM kupitia Uchaguzi Mkuu na kuitikisa Tanzania hasa ukizingatia kuwa atokeo ya uchaguzi wa Wagombea wa CCM, ungezaa mateka wengi ambao wangehamia CCJ (haya ni maoni na mtazamo wangu) baada ya kutema na CCM.
Utaona wazi Mpendazoe alikuwa Bangusilo la wale ambao wako ndani ya CCM ambao wanasubiri kikao hiki cha Bajeti kiishe wapate mshiko wao wa nguvu, ndipo waamue kuutangazia umma Uzalendo wao uko wapi.
Rafiki yangu Mzee Mwanakijiji, umefanya kazi kubwa sana kuwatangaza CCJ, lakini pamoja na utaalamu wako, bado ulisahau kuwa CCM ina mbinu chafu na kuwa si CCM pekee ambao wangetishika kuundwa na kukubalika kwa Chama hiki hususan wakati huu wa Uchaguzi bali hata vyama vingine vya upinzani.
Tatizo ni kila mmoja anataka kuchukua madaraka kutoka CCM, lakini hawataki kutumia muda na mbinu nzuri kukibomoa CCM.
CHADEMA wamejaribu na vita vya ufisadi, lakini mafanikio ni madogo sana zaidi ya msisimko mdogo na mazingaombwe yaliyosababisha Lowassa kujivua Uwaziri Mkuu. CUF walijaribu miaka ile, lakini wameamua kuwa ngamia na kuingiza kichwa kwenye hema na yaelekea wanaweza ingiza nundu nzima lakini ni kwenye lile hema dogo la kuhifadhia kuni na si kwenye hema kuu.
Sasa nikirudi kwa CCJ, sidhani kama Ajenda ya Change itafanikiwa ikiwa CCJ watakazania kusema kuwa ni lazima kwanza waingie Ikulu, ndipo tuanze kuona Cheche zao.
CCJ inabidi irudi kambini na kujipanga upya na si kwa lengo la kusubiri wagombea huru, bali ni kutumia hizo ajenda za Change na Cheche zake kukiangusha CCM bila wao kushiriki Uchaguzi Mkuu!
Kikubwa na hili nawapa CCJ changamoto ni wao kuja na Itikadi na Sera ambazo zitaonyesha wazi kuwa wao ni tofauti na kila mtu na kwamba hata kama hawashiriki Uchaguzi Mkuu mwaka huu, bado watakachokihubiri kwa Watanzania, kitaleta mabadiliko siku ya kupiga kura.
Labda ni kutokana na kutofahamika huku kwa Itikadi yao, ndiyo maana leo hii Viongozi wa Vyama vingine vya Upinzani wanatoa mialiko na kutandika mazulia mekundu kwa CCJ wajiunge nao. Sasa sijui kujiunga huku ni kuachana na CCJ au ni ushirikiani wa kukichambua CCM ili kiangushwe.
Cha msingi ni CCJ kuonyesha na kuegemea kwenye jambo moja kuu kama nguzo yao kuu ya kuondoa adha zinazowakera Watanzania nalo ni ujenzi wa mfumo bora wa kiuchumi ambao utainua viwango vya maisha ya Watanzania.
Sasa hivi suala si Mkapa na Kiwira, Lowassa na Richmond au Rostam na Dowans! Sasa hivi ni kuhusu vipi Tanzania itapunguza deni na kuanza kujitegemea kiuchumi! Sasa hivi ni kushambulia uamuzi wa Serikali kukopa kwenye mabenki huku ikiongeza matumizi badala ya kupunguza matumizi na kupunguza ukubwa wa Serikali ili fedha zitumike kwa mambo ya maendeleo na maslahi ya Mwananchi.
Uchaguzi huu ni kuhusu mishahara ya wafanyakazi, bei za mazao ya wakulima, kuneemeka kwa afya za Watanzania, elimu ya watoto wetu, Utunzaji wa Rasilimali zetu na kuwepo kwa miundombinu imara ya kuimarisha uchumi ambao utampunguzia Mtanzania kejeli za Umasikini, Ujinga na Maradhi.
Itakuwa ni makosa makubwa sana, kama CCJ wakiendelea kung'ang'ania wapewe usajili ili wachukue fomu za uchaguzi! Waachane na Uchaguzi, waanze kuwa kushambulia CCM na sera zake na kufungulia mbwa! Matunda ya kazi yao yasiwe kwa ajili ya CCJ pekee, bali yawe kwa Watanzania wote.
Kama CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, DP na hata wanaojiita Wapiganaji ndani ya CCM ni waoga wa kuparuana na kuchafuana na CCM na Serikali yao kisa ni Ruzuku na nguvu ya Dola, basi CCJ ndio wawe attack dogs wa Watanzania kwa kuwaambia wazi kuwa Maisha Bora kwa Mtanzania yanawezekana na tuna uwezo kwa nguvu na mtaji wetu wenyewe kufanikisha hili na hatuhitaji Wawekezaji.
Narudia tena, hili la kudai vita vya Ufisadi si tija tena, maana Watanzani wameridhika na Ufisadi na ni mfumo ulioshamiri, hivyo kutaja majina na fedha zilizoibiwa hakuleti mabadiliko yoyote zaidi ya mapovu ya hapa na pale.
Natofautiana nawe rafiki yangu katika vita hivi vya kuing'oa CCM, nawe unalielewa hilo.
Natamka wazi kutaka kuleta hitimisho kwa madhambi yaliyotufikisha hapa si kigezo bora cha kushinda uchaguzi, kutoa ahadi kuwa tutawafunga au kufilisi si kigezo au mali kwa Watanzania. Si kwamba haya yasifanyike, bali Watanzania hawako tayari kupiga kura ili yatimilike na ushahidi uko wazi katika Chaguzi ndogo zote na uchaguzi wa TAMISEMI mwaka jana.
Hivyo basi kishindo cha CCJ, kimezimwa kutokana na woga wa vyama vingine ya kisiasa na zaidi ni makosa ya kujianda kivita na kimapambano kulikofanywa na CCJ ambako kumefanya leo Tendwa awapige mpira na kuwafanya waonekane ni watoto na wasiojua wanalokifanya. Yawezekana ni pupa. ashiki au midadi ya kuamini kuwa wakipata usajili, basi CCM itaanguka! Kazi hiyo si rahisi, waulizeni CUF kule Zanzibar au kina CHADEMA, NCCR na wengine.
Ningekuwa mimi CCJ, ningejiandaa vizuri na kujijenga ili nishiriki vizuri Uchaguzi Mkuu 2015. Ningejenga nguzo imara, kutangaza Itikadi na Sera huku nikiichambua CCM na Itikadi zake na Sera na kuonyesha ni vipi hazina manufaa tena kwa Watanzania.
It is not too late to join the fight, I extend my welcome to CCJ to join the battle, but they need to be good listeners and keep a distance from ghalasa kutoka CCM ambao wameshindwa kusimama kidete na kumtetea Mtanzania ndani ya CCM na sasa wanatafuta namna ya kuendeleza mlo na kutia samli vitumbua vyao.
Mzee Mwanakijiji, usikate tamaa, bado ujumbe wako wa Change utafanikiwa. Subira yavuta heri na haraka haraka haina baraka! Njoo bwana tumalize kukijenga PPPT tutafanikiwa!
Wako katika mapambano ya kuleta Mapinduzi na Mabadiliko ya Fikra,
Kama kuna kituko cha Kisiasa na Uchanga (ndio natumia herufi kubwa kama msisitizo) ambacho kimetokea Tanzania na mchakato wa Siasa, ni vuguvugu la kuanzishwa kwa CCJ na matokeo yaliyotokea sasa hivi ambapo wamekosa usajili na kila Chama cha Upinzani unawaangukia na kuwaomba wajiunge kwao.
Kwangu mimi nasema hivi, ilikuwa ni kosa kubwa sana kwa CCJ kukimbilia kutaka kusajiliwa ili kishiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu kutokana na sababu kuu moja: CCJ kuwa chama kimbilio kwa wale ambao wanatarajia kutemwa na CCM na ambao wanaona aibu kuingia vyama vingine au kula matapishi yao ya kudharau haki za msingi za Uraia kama vile kuundwa kwa katiba mpya au kukemea uchafu ulioko ndani ya CCM.
CCJ walikuja kwa kujiamini sana, lakini kasi yao ilinitia shaka hasa kung'angania kusajiliwa ili kishiriki Uchaguzi Mkuu. Inawezekana kina Itikadi ambayo ni ya mkono wa kushoto wa siasa kali, lakini badala ya kukijenga chama (kama vile Mchungaji anavyotaka kuanzisha PPPT) kuanzia vijijini na kusambaza moto wa CCJ unaoambatana na Itikadi na Sera ambazo ni tofauti na CCM, CCJ waliingia kichwa kichwa mtego ule ule wa kukimbilia kutaka kuing'oa CCM kupitia Uchaguzi Mkuu na kuitikisa Tanzania hasa ukizingatia kuwa atokeo ya uchaguzi wa Wagombea wa CCM, ungezaa mateka wengi ambao wangehamia CCJ (haya ni maoni na mtazamo wangu) baada ya kutema na CCM.
Utaona wazi Mpendazoe alikuwa Bangusilo la wale ambao wako ndani ya CCM ambao wanasubiri kikao hiki cha Bajeti kiishe wapate mshiko wao wa nguvu, ndipo waamue kuutangazia umma Uzalendo wao uko wapi.
Rafiki yangu Mzee Mwanakijiji, umefanya kazi kubwa sana kuwatangaza CCJ, lakini pamoja na utaalamu wako, bado ulisahau kuwa CCM ina mbinu chafu na kuwa si CCM pekee ambao wangetishika kuundwa na kukubalika kwa Chama hiki hususan wakati huu wa Uchaguzi bali hata vyama vingine vya upinzani.
Tatizo ni kila mmoja anataka kuchukua madaraka kutoka CCM, lakini hawataki kutumia muda na mbinu nzuri kukibomoa CCM.
CHADEMA wamejaribu na vita vya ufisadi, lakini mafanikio ni madogo sana zaidi ya msisimko mdogo na mazingaombwe yaliyosababisha Lowassa kujivua Uwaziri Mkuu. CUF walijaribu miaka ile, lakini wameamua kuwa ngamia na kuingiza kichwa kwenye hema na yaelekea wanaweza ingiza nundu nzima lakini ni kwenye lile hema dogo la kuhifadhia kuni na si kwenye hema kuu.
Sasa nikirudi kwa CCJ, sidhani kama Ajenda ya Change itafanikiwa ikiwa CCJ watakazania kusema kuwa ni lazima kwanza waingie Ikulu, ndipo tuanze kuona Cheche zao.
CCJ inabidi irudi kambini na kujipanga upya na si kwa lengo la kusubiri wagombea huru, bali ni kutumia hizo ajenda za Change na Cheche zake kukiangusha CCM bila wao kushiriki Uchaguzi Mkuu!
Kikubwa na hili nawapa CCJ changamoto ni wao kuja na Itikadi na Sera ambazo zitaonyesha wazi kuwa wao ni tofauti na kila mtu na kwamba hata kama hawashiriki Uchaguzi Mkuu mwaka huu, bado watakachokihubiri kwa Watanzania, kitaleta mabadiliko siku ya kupiga kura.
Labda ni kutokana na kutofahamika huku kwa Itikadi yao, ndiyo maana leo hii Viongozi wa Vyama vingine vya Upinzani wanatoa mialiko na kutandika mazulia mekundu kwa CCJ wajiunge nao. Sasa sijui kujiunga huku ni kuachana na CCJ au ni ushirikiani wa kukichambua CCM ili kiangushwe.
Cha msingi ni CCJ kuonyesha na kuegemea kwenye jambo moja kuu kama nguzo yao kuu ya kuondoa adha zinazowakera Watanzania nalo ni ujenzi wa mfumo bora wa kiuchumi ambao utainua viwango vya maisha ya Watanzania.
Sasa hivi suala si Mkapa na Kiwira, Lowassa na Richmond au Rostam na Dowans! Sasa hivi ni kuhusu vipi Tanzania itapunguza deni na kuanza kujitegemea kiuchumi! Sasa hivi ni kushambulia uamuzi wa Serikali kukopa kwenye mabenki huku ikiongeza matumizi badala ya kupunguza matumizi na kupunguza ukubwa wa Serikali ili fedha zitumike kwa mambo ya maendeleo na maslahi ya Mwananchi.
Uchaguzi huu ni kuhusu mishahara ya wafanyakazi, bei za mazao ya wakulima, kuneemeka kwa afya za Watanzania, elimu ya watoto wetu, Utunzaji wa Rasilimali zetu na kuwepo kwa miundombinu imara ya kuimarisha uchumi ambao utampunguzia Mtanzania kejeli za Umasikini, Ujinga na Maradhi.
Itakuwa ni makosa makubwa sana, kama CCJ wakiendelea kung'ang'ania wapewe usajili ili wachukue fomu za uchaguzi! Waachane na Uchaguzi, waanze kuwa kushambulia CCM na sera zake na kufungulia mbwa! Matunda ya kazi yao yasiwe kwa ajili ya CCJ pekee, bali yawe kwa Watanzania wote.
Kama CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, DP na hata wanaojiita Wapiganaji ndani ya CCM ni waoga wa kuparuana na kuchafuana na CCM na Serikali yao kisa ni Ruzuku na nguvu ya Dola, basi CCJ ndio wawe attack dogs wa Watanzania kwa kuwaambia wazi kuwa Maisha Bora kwa Mtanzania yanawezekana na tuna uwezo kwa nguvu na mtaji wetu wenyewe kufanikisha hili na hatuhitaji Wawekezaji.
Narudia tena, hili la kudai vita vya Ufisadi si tija tena, maana Watanzani wameridhika na Ufisadi na ni mfumo ulioshamiri, hivyo kutaja majina na fedha zilizoibiwa hakuleti mabadiliko yoyote zaidi ya mapovu ya hapa na pale.
Natofautiana nawe rafiki yangu katika vita hivi vya kuing'oa CCM, nawe unalielewa hilo.
Natamka wazi kutaka kuleta hitimisho kwa madhambi yaliyotufikisha hapa si kigezo bora cha kushinda uchaguzi, kutoa ahadi kuwa tutawafunga au kufilisi si kigezo au mali kwa Watanzania. Si kwamba haya yasifanyike, bali Watanzania hawako tayari kupiga kura ili yatimilike na ushahidi uko wazi katika Chaguzi ndogo zote na uchaguzi wa TAMISEMI mwaka jana.
Hivyo basi kishindo cha CCJ, kimezimwa kutokana na woga wa vyama vingine ya kisiasa na zaidi ni makosa ya kujianda kivita na kimapambano kulikofanywa na CCJ ambako kumefanya leo Tendwa awapige mpira na kuwafanya waonekane ni watoto na wasiojua wanalokifanya. Yawezekana ni pupa. ashiki au midadi ya kuamini kuwa wakipata usajili, basi CCM itaanguka! Kazi hiyo si rahisi, waulizeni CUF kule Zanzibar au kina CHADEMA, NCCR na wengine.
Ningekuwa mimi CCJ, ningejiandaa vizuri na kujijenga ili nishiriki vizuri Uchaguzi Mkuu 2015. Ningejenga nguzo imara, kutangaza Itikadi na Sera huku nikiichambua CCM na Itikadi zake na Sera na kuonyesha ni vipi hazina manufaa tena kwa Watanzania.
It is not too late to join the fight, I extend my welcome to CCJ to join the battle, but they need to be good listeners and keep a distance from ghalasa kutoka CCM ambao wameshindwa kusimama kidete na kumtetea Mtanzania ndani ya CCM na sasa wanatafuta namna ya kuendeleza mlo na kutia samli vitumbua vyao.
Mzee Mwanakijiji, usikate tamaa, bado ujumbe wako wa Change utafanikiwa. Subira yavuta heri na haraka haraka haina baraka! Njoo bwana tumalize kukijenga PPPT tutafanikiwa!
Wako katika mapambano ya kuleta Mapinduzi na Mabadiliko ya Fikra,