Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,877
- 2,758
Hii ni kwa wote wanaotumia junction ya ubungo mataa. wale trafiki wanapendelea sana hii barabara ya Morogoro na kupuuzia hizi za Mandela na Sam Nujoma. wakati mwingine kwa makusudi kabisa wanapuuzia hizi barabara. wasidhani wao ni wajanja sana. kama kuna aliyewatuma kufanya huo upuuzi basi anataka kuwaponza. awali walishapigwa na wanajeshi. sasa hivi watapigwa na wananchi wenye hasura zao. haiwezekani gari itoke Mbezi ipite mataa wakati anayetoka Tabata na yuko hapo songas awe anang'aa macho tu. Hii inachosha akili na mwili na madhara yake yanaweza kuwa si madogo. nadhani kamanda wa kikosi cha barabarani atapewa habari hizi. WAAMBIE VIJANA WAKO HII IS ALMOST ENOUGH. watu kusubiri dakika 20 mataa kisa magari ya morogoro road yanaruhusiwa ni ubinafsi na si ustaarabu. asitake wananchi wabuni njia mbadala ya kukomesha hili tatizo, njia ambayo italeta madhara kwa wanausalama na raia pia. nadhani ujumbe huu umefika