KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Mpanda mkoani Rukwa PC Omary, amenusurika kufa baada ya kupinduka mtoni wakati akiendesha gari alilomnyang'anya dereva mmoja akimtuhumu kufanya makosa.
Mbali na kupinduka mtoni, askari huyo mwenye namba F 1634 alimgonga na kumvunja miguu yote miwili mwanafunzi wa darasa la sita Shule ya Msingi Mpanda, Juma Kilombili(13) aliyekuwa akiogoa mtoni.
Kabla ya tukio hilo, askari huyo alilikamata gari hilo Toyota Mark II namba T253 AHD linalotumika kama teksi baada ya kufanya makosa ya kawaida ya barabarani na kuamua kuliendesha mwenyewe ndipo alishindwa kulimudu na kutumbukia mto Misungumilo.
Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo, Bi Matilda Walunde, baada ya gari hilo kutumbukia mtoni, lilimjeruhi vibaya kijana huyo ambaye alikimbizwa hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa matibabu.
Akizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili , dereva wa gari hilo aliyejitambulisha kwa jinala Bw. Frank Nicholaus (23), alisema tukio hilo lilitokea Julai 12 saa 6 mchana wakati akimpeleka mteja wake eneo la Shule ya Wasichana Mpanda.
Alisema alipofika maeneo ya mto Misungumilo, alikutana na trafiki huyo ambaye alimsimamisha na kumyang'anya kadi ya gari huku akimwamuru ampeleke mteja huyo halafu arudi eneo hilo.
"Niliporudi, aliniamuru kushuka kwenye gari, mimi nilimtaarifu bosi wangu kwa simu kuwa gari limekamatwa. Askari huyo alininyang'anya funguo na kujaribu kuliendesha, kwa kuwa nililiegesha pembeni mwa barabara alipowasha tu, liliserereka kwa kasi na kutumbukia mto uliokuwa karibu na kumgonga mtoto aliyekuwa akioga baada ya kufua nguo zake hapo mtoni,"alisimulia dereva huyo.
Kwa upande wake mmiliki wa gari hilo aliyejimbambulisha kwa jina la Bw. Charles Kaholilo mkazi wa kitongoji cha Msasani Mpanda, alisema amepata hasara kubwa kutokana na uzembe na 'ujuaji' wa trafiki huyo kwa kuwa gari hilo limekufa injini yake kutokana na ajali hiyo.
Mmoja wa wauguzi wa hospitali ya wilaya ya Mpanda aliyeomba jina lake lihifadhiwe kwa madai kuwa si msemaji wa hospitali hiyo, alikiri kumpokea mtoto huyo na kwamba baada ya matibabu ya awali wamemsafirisha kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa matibabu zaidi kutokana na kuvunjika miguu yote miwili na kupata majeraha mengine makubwa mwilini.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa Bw. Isunto Mantage amekiri kupokea taarifa za tukio hilo na kuongeza kuwa Jeshi hilo linamhoji trafiki huyo na atapandishwa kizimbani wakati wowote baada ya upelelezi kukamilika.
Source: Majira
Mbali na kupinduka mtoni, askari huyo mwenye namba F 1634 alimgonga na kumvunja miguu yote miwili mwanafunzi wa darasa la sita Shule ya Msingi Mpanda, Juma Kilombili(13) aliyekuwa akiogoa mtoni.
Kabla ya tukio hilo, askari huyo alilikamata gari hilo Toyota Mark II namba T253 AHD linalotumika kama teksi baada ya kufanya makosa ya kawaida ya barabarani na kuamua kuliendesha mwenyewe ndipo alishindwa kulimudu na kutumbukia mto Misungumilo.
Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo, Bi Matilda Walunde, baada ya gari hilo kutumbukia mtoni, lilimjeruhi vibaya kijana huyo ambaye alikimbizwa hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa matibabu.
Akizungumza kwa njia ya simu na gazeti hili , dereva wa gari hilo aliyejitambulisha kwa jinala Bw. Frank Nicholaus (23), alisema tukio hilo lilitokea Julai 12 saa 6 mchana wakati akimpeleka mteja wake eneo la Shule ya Wasichana Mpanda.
Alisema alipofika maeneo ya mto Misungumilo, alikutana na trafiki huyo ambaye alimsimamisha na kumyang'anya kadi ya gari huku akimwamuru ampeleke mteja huyo halafu arudi eneo hilo.
"Niliporudi, aliniamuru kushuka kwenye gari, mimi nilimtaarifu bosi wangu kwa simu kuwa gari limekamatwa. Askari huyo alininyang'anya funguo na kujaribu kuliendesha, kwa kuwa nililiegesha pembeni mwa barabara alipowasha tu, liliserereka kwa kasi na kutumbukia mto uliokuwa karibu na kumgonga mtoto aliyekuwa akioga baada ya kufua nguo zake hapo mtoni,"alisimulia dereva huyo.
Kwa upande wake mmiliki wa gari hilo aliyejimbambulisha kwa jina la Bw. Charles Kaholilo mkazi wa kitongoji cha Msasani Mpanda, alisema amepata hasara kubwa kutokana na uzembe na 'ujuaji' wa trafiki huyo kwa kuwa gari hilo limekufa injini yake kutokana na ajali hiyo.
Mmoja wa wauguzi wa hospitali ya wilaya ya Mpanda aliyeomba jina lake lihifadhiwe kwa madai kuwa si msemaji wa hospitali hiyo, alikiri kumpokea mtoto huyo na kwamba baada ya matibabu ya awali wamemsafirisha kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa matibabu zaidi kutokana na kuvunjika miguu yote miwili na kupata majeraha mengine makubwa mwilini.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa Bw. Isunto Mantage amekiri kupokea taarifa za tukio hilo na kuongeza kuwa Jeshi hilo linamhoji trafiki huyo na atapandishwa kizimbani wakati wowote baada ya upelelezi kukamilika.
Source: Majira