nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Wednesday, 18 May 2011 11:55 newsroom
Na Mwandishi Wetu Gazeti la Uhuru
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeanza uchunguzi wa ukwepaji kodi unaodaiwa kufanywa na CHADEMA, imebainika. TRA imeanza uchunguzi baada ya kuwepo madai kuwa chama hicho kimekwepa kodi katika ununuzi na uingizaji vifaa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana na mishahara ya wafanyakazi wake. Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Placidus Luoga, juzi alikiri kuwepo ufuatiliaji huo na kuwa tayari uchunguzi wa suala hilo umeanza.
"TRA inafuatilia suala hili kwa umakini na endapo itathibitika kodi haikulipwa, lazima sheria itafuata mkondo wake. "Uchunguzi wetu hautakuwa wa kumuonea mtu au chama, bali utasimamia maadili na sheria zinazotuongoza ili kuhakikisha haki inapatikana,'' alisema. Luoga alisema lengo la kufanya uchunguzi ni kuhakikisha kila mtu, chama au taasisi inayopaswa kulipa kodi inafanya hivyo kwa mujibu wa sheria. Alisema baada ya ufuatiliaji itajulikana endapo CHADEMA ilikwepa kulipa kodi ilipoingiza nchini vifaa vya uenezi kutoka China. Vifaa hivyo ni kofia, fulana na bendera. Vifaa hivyo vilinunuliwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana na ilidaiwa vilipitishwa njia za panya katika eneo la Holili mkoani Kilimanjaro, baada ya kupata sh. milioni 100 kutoka kwa mfanyabiashara Mustapha Sabodo.
Ununuzi wa vifaa hivyo unadaiwa kugubikwa na ufisadi kutokana na uamuzi wa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, kudai aliongeza sh. milioni 188 katika ununuzi, hivyo kufanya kiasi cha fedha kilichotumika kuwa sh. milioni 288. Utata kuhusu ununuzi huo unathibitishwa na habari za kuaminika kutoka ndani ya CHADEMA, pale Mbowe aliposema anakidai chama hicho sh. milioni 188 ambazo aliongeza ili kununua vifaa, lakini ameshindwa kuonyesha risiti aliyotumia kulipa wakati wa kuviingiza nchini ili kuthibitisha madai yake. Akizungumzia mishahara ya wafanyakazi wa chama hicho kutokatwa kodi, Luoga alisema sheria ipo wazi kuwa mishahara yote ya wafanyakazi lazima ikatwe kodi. "Mwajiri atawajibika kumlipia kodi mtumishi wake ikiwa TRA itaona mfanyakazi anastahili kulipa kodi, hivyo CHADEMA wakibainika kwenye hilo basi itabidi walipe kodi,'' alisema.
Gazeti hili lilifichua kuwa mshahara wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa ni zaidi ya sh. milioni saba ambazo ni nyingi kuliko za wabunge alizowahi kuzipigia kelele. Pia mshahara huo haukatwi kodi na TRA. Siku moja baada ya taarifa hizo kuvuja, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa CHADEMA, Anthony Komu na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mabere Marando, waliitisha mkutano na waandishi wa habari kukanusha taarifa hizo, jambo ambalo baadhi ya viongozi wa CHADEMA wamefichua kwamba ufafanuzi uliotolewa na viongozi hao ni wa uongo. "Komu kudai Dk. Slaa analipwa mshahara wa sh. 1,725,000 na lita 1,000 za mafuta kila mwezi ni uongo wenye lengo la kutaka kuficha jinsi baadhi ya viongozi waandamizi walivyounda mtandao wa kutumbua fedha za CHADEMA," chanzo cha habari kilisema.
UHURU ilipata waraka unaoonyesha mapendekezo ya posho ya Dk. Slaa kama Azimio la Kamati Kuu iliyokaa Januari 29 hadi 30 mwaka huu, Dar es Salaam ni tofauti na maelezo waliyotoa Komu na Marando.
Kwa mujibu wa waraka huo, ambao hauonyeshi kiwango kinachokatwa kodi, posho ya Dk. Slaa imegawanywa katika sehemu sita za posho ya mwezi, fedha za mafuta, majukumu, viburudisho, nyumba na utendaji kazi.
Wakati Komu katika ufafanuzi wake alisema Dk. Slaa analipwa mshahara (basic) wa sh. 1,725,000 waraka unaonyesha analipwa sh. 2,300,000. Mbunge analipwa sh. 2,305,000 kabla ya kukatwa kodi.
Kwa upande wa posho, Dk. Slaa analipwa fedha za mafuta sh. 1,387,500 kwa lita 750 kwa mwezi, huku fedha za majukumu zikiwa sh. 575,000, mawasiliano sh. 460,000 na nyumba sh. 1,000,000.
Posho nyingine ni kwa ajili ya viburudisho sh. 462,500 na utendaji kazi sh. 989,000. Mshahara huo umefanywa maalumu kwa Dk. Slaa pekee na iwapo chama hicho kitapata katibu mkuu mwingine hawezi kulipwa hivyo.
Dk. Slaa akiungwa mkono na Mbowe anadaiwa kujipatia posho ya nyumba mara mbili, kwani ilishapendekezwa alipwe sh. milioni 40 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa nyumba yake eneo la Mbweni, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam anakoishi.
Licha ya kupewa fedha hizo, Dk. Slaa ameendelea kupewa posho ya nyumba ya sh. 1,000,000 kila mwezi.
Na Mwandishi Wetu Gazeti la Uhuru
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeanza uchunguzi wa ukwepaji kodi unaodaiwa kufanywa na CHADEMA, imebainika. TRA imeanza uchunguzi baada ya kuwepo madai kuwa chama hicho kimekwepa kodi katika ununuzi na uingizaji vifaa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana na mishahara ya wafanyakazi wake. Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Placidus Luoga, juzi alikiri kuwepo ufuatiliaji huo na kuwa tayari uchunguzi wa suala hilo umeanza.
"TRA inafuatilia suala hili kwa umakini na endapo itathibitika kodi haikulipwa, lazima sheria itafuata mkondo wake. "Uchunguzi wetu hautakuwa wa kumuonea mtu au chama, bali utasimamia maadili na sheria zinazotuongoza ili kuhakikisha haki inapatikana,'' alisema. Luoga alisema lengo la kufanya uchunguzi ni kuhakikisha kila mtu, chama au taasisi inayopaswa kulipa kodi inafanya hivyo kwa mujibu wa sheria. Alisema baada ya ufuatiliaji itajulikana endapo CHADEMA ilikwepa kulipa kodi ilipoingiza nchini vifaa vya uenezi kutoka China. Vifaa hivyo ni kofia, fulana na bendera. Vifaa hivyo vilinunuliwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana na ilidaiwa vilipitishwa njia za panya katika eneo la Holili mkoani Kilimanjaro, baada ya kupata sh. milioni 100 kutoka kwa mfanyabiashara Mustapha Sabodo.
Ununuzi wa vifaa hivyo unadaiwa kugubikwa na ufisadi kutokana na uamuzi wa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe, kudai aliongeza sh. milioni 188 katika ununuzi, hivyo kufanya kiasi cha fedha kilichotumika kuwa sh. milioni 288. Utata kuhusu ununuzi huo unathibitishwa na habari za kuaminika kutoka ndani ya CHADEMA, pale Mbowe aliposema anakidai chama hicho sh. milioni 188 ambazo aliongeza ili kununua vifaa, lakini ameshindwa kuonyesha risiti aliyotumia kulipa wakati wa kuviingiza nchini ili kuthibitisha madai yake. Akizungumzia mishahara ya wafanyakazi wa chama hicho kutokatwa kodi, Luoga alisema sheria ipo wazi kuwa mishahara yote ya wafanyakazi lazima ikatwe kodi. "Mwajiri atawajibika kumlipia kodi mtumishi wake ikiwa TRA itaona mfanyakazi anastahili kulipa kodi, hivyo CHADEMA wakibainika kwenye hilo basi itabidi walipe kodi,'' alisema.
Gazeti hili lilifichua kuwa mshahara wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa ni zaidi ya sh. milioni saba ambazo ni nyingi kuliko za wabunge alizowahi kuzipigia kelele. Pia mshahara huo haukatwi kodi na TRA. Siku moja baada ya taarifa hizo kuvuja, Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa CHADEMA, Anthony Komu na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mabere Marando, waliitisha mkutano na waandishi wa habari kukanusha taarifa hizo, jambo ambalo baadhi ya viongozi wa CHADEMA wamefichua kwamba ufafanuzi uliotolewa na viongozi hao ni wa uongo. "Komu kudai Dk. Slaa analipwa mshahara wa sh. 1,725,000 na lita 1,000 za mafuta kila mwezi ni uongo wenye lengo la kutaka kuficha jinsi baadhi ya viongozi waandamizi walivyounda mtandao wa kutumbua fedha za CHADEMA," chanzo cha habari kilisema.
UHURU ilipata waraka unaoonyesha mapendekezo ya posho ya Dk. Slaa kama Azimio la Kamati Kuu iliyokaa Januari 29 hadi 30 mwaka huu, Dar es Salaam ni tofauti na maelezo waliyotoa Komu na Marando.
Kwa mujibu wa waraka huo, ambao hauonyeshi kiwango kinachokatwa kodi, posho ya Dk. Slaa imegawanywa katika sehemu sita za posho ya mwezi, fedha za mafuta, majukumu, viburudisho, nyumba na utendaji kazi.
Wakati Komu katika ufafanuzi wake alisema Dk. Slaa analipwa mshahara (basic) wa sh. 1,725,000 waraka unaonyesha analipwa sh. 2,300,000. Mbunge analipwa sh. 2,305,000 kabla ya kukatwa kodi.
Kwa upande wa posho, Dk. Slaa analipwa fedha za mafuta sh. 1,387,500 kwa lita 750 kwa mwezi, huku fedha za majukumu zikiwa sh. 575,000, mawasiliano sh. 460,000 na nyumba sh. 1,000,000.
Posho nyingine ni kwa ajili ya viburudisho sh. 462,500 na utendaji kazi sh. 989,000. Mshahara huo umefanywa maalumu kwa Dk. Slaa pekee na iwapo chama hicho kitapata katibu mkuu mwingine hawezi kulipwa hivyo.
Dk. Slaa akiungwa mkono na Mbowe anadaiwa kujipatia posho ya nyumba mara mbili, kwani ilishapendekezwa alipwe sh. milioni 40 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa nyumba yake eneo la Mbweni, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam anakoishi.
Licha ya kupewa fedha hizo, Dk. Slaa ameendelea kupewa posho ya nyumba ya sh. 1,000,000 kila mwezi.