TRA wameniomba rushwa lakini sitoi rushwa kwenye maisha yangu

Kaka wala usipate tabu TRA inauwezo (Caspacity) ya kuwashughulikia hao watu Tatizo ni kuwa Haipati ushirikiano wa Kutosha (Rushwa ni Siri). Kwa taarifa yako na Umma ni kuwa Mamlaka ya Mapato inacho kitengo kinaitwa "Internal Affairs" Kazi yake ni Kufanya uchunguzi (Investigation) kwa Tuhuma zote zinazohusiana na Maadili na Utendaji kazi wa Watumishi wake. Kitengo kina wachunguzi mahiri na kimeshafanya kazi zilizoathiri ufanisi na katika masuala ya Maadili ndani na nje ya mamlaka kinatambuliwa sana.NAMNA YA KUWASILIANA NA KITENGO:ili kukipa kitengo meno na Uhuru katika chunguzi zake kitengo kinapata maelekezo kutoka kwa Kamishna mkuu wa TRA na kitoa ripoti zake kwake. Kama unalo shitaka tuhuma tuma kwa barua kwa KAMISHNA MKUU MAMLAKA YA MAPATO TANZANIADar es salaam Tanzania Box 11491 +255222116453 +255222138866
 
pole sana mkubwa na hongera sana kwa moyo wako mwema kusaidia nchi yako.naomba chonde usighaili kufunga ivo vifaa-tiba bongo jitahidi kufatilia mamlaka husika ili ujue nini kinatakiwa kulipiwa kodi na nini hakitakiwi yani uwe na uwigo mkubwa wa kujua ndicho na sicho (kama polisi wetu wehu ukijua sheria wanabaki wanakuangalia ni kukomaa tu nao).TRA walio wengi ni wezi hasa hao maofisa wa chini www ruka nao ofisini idara husika,ungekua apa nilipo ningekuunganisha na mtakukuru mmoja tu ninaemwamini angemshikisha adabu kwa simu tu angeachia uo mzigo!!!
about jk,anaongea sana uyo m.kwere ila anajua kilicho chini nn kinaendelea ufisadi na ujambazi wa watendaji wake na hana maamuzi magumu ya kuwatimua na kuwachukulia hatua za kisheria,ila kitu kingine mmngekua mnamwuliza anapopaa kuja newyork anashughulikiaje ujamabazi uliojaa ktk systems za serikalini na upataji vibali???mumsikia au ao anaoongozana nao katika msafara

yani nina hasira nao hao wezi acha
 
Kaka wala usipate tabu TRA inauwezo (Caspacity) ya kuwashughulikia hao watu Tatizo ni kuwa Haipati ushirikiano wa Kutosha (Rushwa ni Siri). Kwa taarifa yako na Umma ni kuwa Mamlaka ya Mapato inacho kitengo kinaitwa "Internal Affairs" Kazi yake ni Kufanya uchunguzi (Investigation) kwa Tuhuma zote zinazohusiana na Maadili na Utendaji kazi wa Watumishi wake. Kitengo kina wachunguzi mahiri na kimeshafanya kazi zilizoathiri ufanisi na katika masuala ya Maadili ndani na nje ya mamlaka kinatambuliwa sana.NAMNA YA KUWASILIANA NA KITENGO:ili kukipa kitengo meno na Uhuru katika chunguzi zake kitengo kinapata maelekezo kutoka kwa Kamishna mkuu wa TRA na kitoa ripoti zake kwake. Kama unalo shitaka tuhuma tuma kwa barua kwa KAMISHNA MKUU MAMLAKA YA MAPATO TANZANIADar es salaam Tanzania Box 11491 +255222116453 +255222138866
kaka mbona nimepiga hizo namba wananiambia kuwa hiyo idara ya internal affairs wanahusika na internal ethics
za watumishi wa mamlaka,lakini rushwa niliport pccb,sasa kweli hapo tutapata msaada maana wamenizungusha na kunizuga zuga tu kwenye simu ,wakati mm nina malalamiko kibao na wameshakula hela zangu nyingi tu hawa watu wa tra
 
wote tuwe waumini wa kanuni namba 5 ya Tanu"Rushwa ni adui wa haki,sitatoa wala sitapokea rushwa"

Ukweli ni kwamba TRA iko pale kukadiria na kukusanya mapato ya serikali kwa mujibu wa sheria na kwa haki bila kumwonea mtu yeyote na pia vitendo vyovyote vya rushwa havikubaliki na hatua kali huchukuliwa kwa mfanyakazi yeyote wa TRA anayebainika kujihusisha na rushwa. Hivyo ndugu mtoa mada toa taarifa kwa namba ifuatayo - Kaimu Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi simu namba 0784411991 e-mail akiula@tra.go.tz au fika ofisini TRA Makao Makuu onana na Meneja wa kitengo cha Maadili (Internal Affairs Unit). Tuna hakika hatua stahili zitachukuliwa


KIMUNDU Tafadhali kama bado unasumbuliwa piga simu hii 0784411991 ili usaidiwe. RUSHWA HAIKUBALIKI TRA
 
Nimebahatika kufanikiwa kupeleka vitu vya kufungua Hospitali Tanzania ambavyo nimevipata hapa USA kwa miaka miwili na nusu. Vitu vyote ni vya Hospitali na sijachanganya Container langu na kitu chochote ambacho sio cha hospitali. Nina List niliyopewa na barua zakuonyesha kuwa vitu ni vya misaada kwa Hospitali mpya ninayotaka kufungua. Sasa bandarini Tanzania watu wa TRA wanasema eti sio vitu vyote vina msamaha wa kodi na kusema vitu kama vitanda havina msamaha. Vitanda ambavyo ni vichache ninavyo ni vya Hospitali na ni vifaa vya kihospitali sio vitanda vya vyumbani, Dialysis Chair sio kitu cha nyumbani bali ni kiti cha kutumia wakati wa kufanya Dialysis. Sasa sisi tunahangaika huku kujaribu kusaidia kwa kufanya kazi usiku na mchana ili kufungua Clinics ambazo ukiangalia vizuri hatupati kitu lakini vikwazo visivyo vya msingi vimewekwa na TRA ili kupata sababu ya kuomba rushwa. Sasa huyo jamaa wa TRA anaomba rushwa kama nataka vitu hivyo vitoke vyote na mimi sitatoa rushwa kwa mtu yeyote. Vitu vyangu vikipigwa Mnada mimi na Tanzania basi! nilikuwa nataka kuleta CT Scan ambazo ni hadimu Tanzania lakini nikiendelea kusumbuliwa bila sababu ya msingi sitafanya hivyo tena na watakao umia ni Watanzania masikini. Raisi yuko New York anaomba misaada lakini sisi Watanzania wenzake tunaofanya jitihada za kusadia nchi na uchumi tumekuwa watu wa kunyanyaswa bila sababu za msingi. Kama Watanzania wanaofanya kwenye hizi sehemu hawana uzalendo je mnategemea vipi nchi yetu kuendelea. Je kama Tanzania itatukosa sisi ambao tumetumia pesa zetu, muda wetu kuleta vitu kama vya hospitali na kusumbuliwa je tutategemea wazungu watusaidie mpaka lini badala ya kujisaidia wenyewe. Kama nivyosema siku za nyuma kama hutuwezi kubadilika tusilalamike kwa umasikini.
Pole sana, hiyo ndiyo Tanzania. Si wewe peke yako, hata investor wengi tu wanaokuja kuwekeza Tanzania wakileta mizigo yao wanaombwa rushwa pale bandari, hivyo sura ya wafanyakazi (TRA na bandari) ni mbaya sana kwa watu wa nje na ndiyo wanaochangia kuharibu na kurudisha nyuma uwekezaji. Mi ningekushauri fikisha suala lako PCCB, ongea na huyo mtu anayetaka rushwa halafu wasiliana na PCCB ili akamatwe. Ukiwaendekeza kweli vitu vyako vitapigwa mnada.
 
je umemuambia sikupi rushwa face to face au umeondoka kinyonge tu? i mean umegombana naye?
tatzo letu watz ni kwenda kulalamikia mbali ungempa ukweli wake, liwalo na liwe, acha upole wewe...
 
Ukweli ni kwamba TRA iko pale kukadiria na kukusanya mapato ya serikali kwa mujibu wa sheria na kwa haki bila kumwonea mtu yeyote na pia vitendo vyovyote vya rushwa havikubaliki na hatua kali huchukuliwa kwa mfanyakazi yeyote wa TRA anayebainika kujihusisha na rushwa. Hivyo ndugu mtoa mada toa taarifa kwa namba ifuatayo - Kaimu Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi simu namba 0784411991 e-mail akiula@tra.go.tz au fika ofisini TRA Makao Makuu onana na Meneja wa kitengo cha Maadili (Internal Affairs Unit). Tuna hakika hatua stahili zitachukuliwa

Mkuu inaonekana unaifahamu uzuri TRA na huamini kama kuna rushwa TRA. Au umekuja tu kitetea hii hoja. Hao makamishna wenyewe unaosema wakaonwe ni usumbufu na urasimu wa kufa mtu. Kama hayo unayosema ni kweli nani angelalamikia rushwa?
Whatever, huyu jamaa anayeleta hvi vifaa mnafikiri ataokoa maisha ya watu wamgapi? Kwann yeye aanze kuzunguka na makaratasi kubembeleza? Kwann system isiwe flexible mtu analeta vifaa vya hosp kwann asumbuke? Mbona hao Aga Khan hawalipi kodi? Au mbona the so called ''wawekezaji'' wanawekewa red carpets wapite na misamaha ya kodi kwao ni shwari tu? Why not mzawa anayekuja kusaidia wazawa? Hao TRA wanajua watanzania wangapi wanapoteza maisha kwa kukosa huduma za dialysis?
Inasikitisha na inachosha!
 
Kamundu,haina haja ya kufanya hasira,umeamua kuwasaidia wa-TZ simamia hlo hadi mwisho. Ukisema sasa basi sifanyi tena,sawa lakini naamini kila utakaposikia mtanzania amekufa kwa kukosa huduma za dialysis,CT Scan au MRI au kingine cjui kama utakuwa na amani moyoni. Mimi najua wa-TZ wanavopoteza maisha kila uchao kwa kukosa huduma za tiba na kupata watu wenye uchungu na kuamua kusaidia nyumbani ni wachache. Naamini kupitia ushauri unaopata hapa mambo yatakwenda salama.
Nchi hii km tumelaaniwa,cjui kwann tunakumbatia wageni tena wasiosaidia kuboresha maisha ya mtanzania bali kumnyonya na bado hawalipi kodi wala nini.
Usikate tamaa najua wanasoma humu JF na wakiona wataogopa na utafanikiwa.
 
Nimebahatika kufanikiwa kupeleka vitu vya kufungua Hospitali Tanzania ambavyo nimevipata hapa USA kwa miaka miwili na nusu. Vitu vyote ni vya Hospitali na sijachanganya Container langu na kitu chochote ambacho sio cha hospitali. Nina List niliyopewa na barua zakuonyesha kuwa vitu ni vya misaada kwa Hospitali mpya ninayotaka kufungua. Sasa bandarini Tanzania watu wa TRA wanasema eti sio vitu vyote vina msamaha wa kodi na kusema vitu kama vitanda havina msamaha. Vitanda ambavyo ni vichache ninavyo ni vya Hospitali na ni vifaa vya kihospitali sio vitanda vya vyumbani, Dialysis Chair sio kitu cha nyumbani bali ni kiti cha kutumia wakati wa kufanya Dialysis. Sasa sisi tunahangaika huku kujaribu kusaidia kwa kufanya kazi usiku na mchana ili kufungua Clinics ambazo ukiangalia vizuri hatupati kitu lakini vikwazo visivyo vya msingi vimewekwa na TRA ili kupata sababu ya kuomba rushwa. Sasa huyo jamaa wa TRA anaomba rushwa kama nataka vitu hivyo vitoke vyote na mimi sitatoa rushwa kwa mtu yeyote. Vitu vyangu vikipigwa Mnada mimi na Tanzania basi! nilikuwa nataka kuleta CT Scan ambazo ni hadimu Tanzania lakini nikiendelea kusumbuliwa bila sababu ya msingi sitafanya hivyo tena na watakao umia ni Watanzania masikini. Raisi yuko New York anaomba misaada lakini sisi Watanzania wenzake tunaofanya jitihada za kusadia nchi na uchumi tumekuwa watu wa kunyanyaswa bila sababu za msingi. Kama Watanzania wanaofanya kwenye hizi sehemu hawana uzalendo je mnategemea vipi nchi yetu kuendelea. Je kama Tanzania itatukosa sisi ambao tumetumia pesa zetu, muda wetu kuleta vitu kama vya hospitali na kusumbuliwa je tutategemea wazungu watusaidie mpaka lini badala ya kujisaidia wenyewe. Kama nivyosema siku za nyuma kama hutuwezi kubadilika tusilalamike kwa umasikini.

pole mkuu ila sasa inatakiwa hukuTRA na sehemu nyingine zote wanazotoa huduma wavae name tag shingoni ili tujue ni nani na nani wana utata wakitajwa na watu zaidi ya mara tano basi walakini utajulikana.MAANA SASA IMEKUWA TOO MUCH.... RUSHWA RUSHWA
 
Kamundu

Una vita tatu kuu hapo

  1. Ya TRA na rushwa, hii si ngumu ila itakuchelewesha, kuna namba umepewa hapo juu ifanyie kazi, lakini pia hakikisha consignment yako ni clean, haina vitu vya ziada na kila product ina profile safi kabisa with all supporting documents. Nijuavyo mimi Kitilya ni msikivu kama ukimuapproach vizuri. na ikibidi waweza hata kutafuta entry point nyingine, USIKATE TAMAA
  2. Vita ya pili ni ya competitors, kuna siasa na umafia wa hali ya juu hasa mtanzania akitaka kufungua hospitali, maabara au any ultra modern facility, kumekua na mikingamo mingi sana kwenye usajili, ushirikiano na vitu kama hivyo
  3. Cha tatu ni machines standards na validation ya some results, sometimes utaambiwa mashine yako haitambuliki hivyo hatuwezi kukukabidhi watanzania uchezee afya zao, pambana sana hapo..... Ni ulaji tu wa watu. Tied to this ni ile type ya umeme wetu, ANGALIA SANA HILO

While sorting out TRA, hakikisha una dossiers za machines zote na any approvals za validations za tests zitakulinda

Si vibaya ku-consult competitors wako
 
Nimelitoa Container bila rushwa bahati nzuri jamaa ambaye alikuwa ni mwamuzi wa mwisho kwenye swala la kodi nimesoma naye Form Five! hivyo sijalipia kodi kama inavyotakiwa kwenye vifaa vya hospitali. Cha ajabu ni kwanini nilikuwa nasumbuliwa hivi? na wasio na marafiki ni vipi na watafanya nini?. Tunakazi kweli!!!
 
Pole sana Mzalendo, usikate tamaa VUMILIA.....kuwa mpole na mkali wakati huohuo....wanajua una dola kibao na wanavyokuona umewiva ndio wanajua ndio pa kuponea...na wanataka ukate tamaa ili waubebe huo mzigo kwa njia ya mnada.....Kaza buti na nenda pale unanuka jasho la Bongoland ili wajue ushakuwa mmbongo na mgumu...watavitoa tu so far umekamilisha taratibu zote...ingawa utachelewa. Usilegeze uzi. Kila la kheri
 
Back
Top Bottom