TRA - Napasuwa Ufisadi Mwingine!

kupata ushahidi kirahisi ni ngumu, lakini kama kuna ufisadi, ilikuwa ni kazi ya serikali kuzisaka hizo documents kwa sababu wananchi tayari wameshatoa wasiwasi wao upo kwa nani.

lakini hilo tuote tu kwa kuwa halitotokea hapa tanzania katika miaka hii ya karibu.
anaetishia kuwafichua mafisadi anakufa taratibu , na habari tunapewa wiki baada ya kufa
 
Mafisadi wa design hii ni wengi sana.Na ufisadi kusema kweli uko nchi nzima.Vyombo vya kisheria havina meno kwa hawa majambazi.Wana influence kila mahali.

Ni watu wa kutoa michango haraka haraka kwenye dhifa mbalimbali.Ni watu wanaoweza kufanya lolote ili kubaki katika life style waliyonayo.

Hata hivyo kuwataja pekee haitoshi.Tunahitaji kupata haidhuru nyaraka zinazoweza kutupa pa kuanzia.

Mimi naona kila ofisi ya serikali ya jiji au serikali kuu ninayoifikia nikiwa na shida ya kuhudumiwa napewa maswali na masharti ya kifisadi ili niache pesa pale.

Najitahidi kuwa mtu mwaminifu lakini katika shughuli najikuta nina mafisadi wa ofisini hadi barabarani ninakopita.

Sheria zimewekwa lakini wenye kitu wanazipinda na kuchukua wanachokiona madhali wana power ya pesa.

Ndugu zangu wa JF tunaweza kweli kunyoosha mambo hapa nchini? Tunawezaje kuishi bila ufisadi? Mtu umelala na ukiamka asubuhi unakuta open space mtu kajenga.

Watu wanatengeneza documents fake na kukopa mabilioni kisha wanapotea lakini wewe mwenye kibanda cha halali unafika benki na kupewa masharti kibao hadi unakata tamaa ya kupata mkopo.Ufisadi umeemea kila mahali,kwenye vyombo vya fedha,vyombo vya kutoa huduma na hata vyombo vya sheria.

Nani atuokoe jamani genge la wajivuni limeshika kila kitu? Twende wapi?


Nakubaliana na wewe baadhi ya maeneo kama vile kudai pesa maeneo mengi yawe ya serikali kuu au hata serikali za mitaa lakini kwa suala la majambazi hilo nakukatalia kwa sasa limepungua sana maan mara yangu ya mwisho nakumbuka majambazi ambao wameripotiwa ni wale ambao wamekuwa wakibia wateja katika nyumba za kulala wageni tu kwa kuwavizia huko wakati wamelala na si vinginevyo tofauti na ilivyokuwa hapo awali wakati majambazi yalipokuwa yameshika hatamu yalikuwa yanaweza kupora machana kweupe yaliweza kupora kwenye maduka ya kubadirishia na kufanikiwa kutoroka bila ya kukamatwa
 
Ufisadi mwingine unajulikana wazi lakini kwa kuwa umewatajirisha wanene, wengi wao, mpaka wakubwa wa polisi wanapokea mishahara kutoka kwa haka katajiri fisadi. Haka katajiri kanafumbiwa macho na Takukuru na Usalama wa Taifa na hata hiyo polisi yenyewe. Kwa nini? Kwa sababu tuu eti haka kajitu kana fedha na kana kutajirisha kwa kukaachia ukalinde (mafia style). Kana julikana sana haka kajitu kwa kutembelewa na wanene wa TRA na hata mkuu wa kanda maalum ya polisi alikuwa akimtembelea, bila shaka kuchukuwa chake.........................

...........Huyu si mwingine bali ni Saidi Saad au almaarufu kama Saidi Mahonda anajulikana sana Dar. Kwa machachari yake, dharau zake, dhuluma zake (nyingi tuu) na anatambia fedha zake za ufisadi.

Tushirikiane kufichuwa mafisadi.

JE INAWEZEKANA SAID MWEMA AMEKUSIKIA SOMA HAPA CHINI....

•Mabadiliko makubwa Polisi, Tibaigana ang'atuka

*Kova achukua nafasi yake, Rwambow aenda Mwanza

Na Reuben Kagaruki

JESHI la Polisi limefanya mabadiliko makubwa katika safu yake ya uongozi kuanzia ngazi ya wilaya, mikoa na wakuu wa upelelezi kufuatia maofisa wake wengi kufikisha umri wa kustaafu kwa lazima ifikapo Julai 1, mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Said Mwema, Kamishna wa Utawala na Fedha, Bw. Clodwig Mtweve, alisema Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Alfred Tibaigana anastaafu na nafasi yake inachukuliwa na Bw. Suleiman Kova, aliyekuwa Mbeya.

Atakayeziba nafasi ya Bw. Kova ni Kamanda wa Mkoa wa Bw.Stephen Zelote ambaye nafasi yake inachukuliwa na Bw. Jamal Rwambow, akitokea Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni.

Alisema Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Bw. David Saibullu anastaafu na nafasi yake inachukuliwa na Bw. Liberatus Lyimo Barlow, ambaye kabla ya uteuzi huo, alikuwa Ofisa Nadhimu Utawala na Fedha Kanda Maalum ya Dar es Salaam.

Aliyeteuliwa kushika nafasi ya Bw. Rwambow Mkoa wa Kinondoni ni Bw. Mark Kalunguyeye, ambaye kabla ya uteuzi wake alikuwa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Bw. Ray Karama, aliyekuwa Kikosi cha Kutuza Ghasia, Dar es Salaam ameteuliwa kuwa Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia Wezi wa Mifugo Makao Makuu Arusha.

Bw. Mtweve alisema, Bw. Abdallah Msika amehamishwa kutoka mkoani Kagera na kupelekwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam huku ASP Salewi aliyekuwa Kamanda Mkoa wa Pwani akipelekwa kuziba nafasi yake.

Mabadiliko hayo pia yamemgusa Bw. Mwakyoma aliyekuwa Makao Makuu ya Polisi na sasa anaenda kuwa RPC Mkoa wa Pwani huku RPC wa Tabora, Bw. Mshahili akirejeshwa makao makuu Dar es Salaam na nafasi yake kuzibwa na Bw. Emson Mmari, aliyekuwa Makao Makuu ya Upelelezi.

Bw. Lucas Kusima aliyekuwa Baraza la Ulinzi na Usalama, amehamishiwa Makao Makuu na nafasi yake itazibwa na Bw. Brown Lakey kutoka Makao Makuu ya Upelelezi.

Katika mabadiliko hayo pia yamewagusa wanawake wawili ambapo Bi. Marry Nzuki aliyekuwa OCD Mkoa wa Dodoma anakwenda kuwa Kaimu Kamanda wa Polisi TAZARA huku SSP Lucy Makelemo aliyekuwa OCS Uwanja wa Ndege Mwanza anakuwa Staff Officer I Dar es Salaam.

Alisema mabadiliko hayo pia yamewagusa wakuu wa upelelezi wa mikoa Mara, Kigoma, Shinyanga na Mbeya. Wanaotarajia kustaafu nafasi zao zimechukuliwa na Bw. Msato Marijani aliyekuwa OCD Wilaya ya Biharamulo (Kigoma), Bw. Deusdit Kato (Mara). Kabla ya hapo alikuwa OCD Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam.
 
Labda tuanze mkakati wa kuwachoma moto hawa jamaa kama wa south wanavyowafanyia unyama ma black wenzao. Tuwatokomeze hawa jamaa waishilie mbali. Kuna haja ya kuunda Mungiki ya Bongo. Hali hii inakera saaana, na inatuumiza mno!

Kweli zaidi ya hapo hakuna kwani serikali yetu ipo nao kwa sasa. Wanawaficha hawa mafisadi. Kwa mfano, huyu saidi mahonda akihisi tuu kuwa umemuibia katika maduka yake anakufungia ndani ya store na kuanzan kukupa mkong'oto yeye na ndugu zake. Wameshamfanyia kijana mmoja alikuwa akifanya kazi kwao, halafu wakamweka ndani, ufisadi ni hatari kweli, yaani hu8yo kijana wamempiga halafu wakamweka ndani sijui siku ngapi, kawekwa pale kituo cha polisi Msimbazi bila kufikishwa mahakamni na mwisho wakamwachia kwa kula mateso na wazee wake wakasema wao watalipa hizo tuhuma kwa kulipa wanachosema kaiba. Yaani hakufikishwa mahakamani kwa masiku tele na Said Mahonda kuwa vituo kama vya msimbazi anavimiliki, pesa anazogawa huko zinatosha kufanya asishikwe na aweze kumuweka au kumtowa ndani yeyote yule kwa kosa lolote lile.

Hata mdogo wake kwa Jina la Abdallah, alisha mvunja mkono mtu kwa kudhani kuwa kaiba dukani kwao na hata baada ya kupelekwa kituo cha Msimbazi hakuna alichofanywa na badala yake yule alievunjwa mkono ndio kawekwa ndani kwa kubambikizwa, huyo huyo ndugu yake alishikwa kwa kutowa bastola hadharani, akawekwa Msimbazi wakala fedha wakamwachia. Jamani Serikali iko wapi? mna kula kiasi hamjali hata raia zenu masikini kwa ajili ya ufisadi na kushirikiana na mafisadi?

Hebu wale wema kidogo na mlio kwenye madaraka na mnapitia humu, fuatilieni hizi habari kwa manufaa yetu.
 
Hatari, sasa wazee wa kulindana wataanza kuteteana,ohh hakuna ushaidi ni tuhuma tu! weka mambo hadharani waone aibu kama mzee wa container terminal!
 
Hii ingali ipo katika malumbano? Kuna hatua zozote zimeshachukuliwa?
 
Ufisadi mwingine unajulikana wazi lakini kwa kuwa umewatajirisha wanene, wengi wao, mpaka wakubwa wa polisi wanapokea mishahara kutoka kwa haka katajiri fisadi. Haka katajiri kanafumbiwa macho na Takukuru na Usalama wa Taifa na hata hiyo polisi yenyewe. Kwa nini? Kwa sababu tuu eti haka kajitu kana fedha na kana kutajirisha kwa kukaachia ukalinde (mafia style). Kana julikana sana haka kajitu kwa kutembelewa na wanene wa TRA na hata mkuu wa kanda maalum ya polisi alikuwa akimtembelea, bila shaka kuchukuwa chake.

Kafisadi haka (kwani ni kajitu kadogo tu, wala hukadhanii) kametajirika kwa record time kwa kushirikiana na mafisadi wenzake wa mostly TRA na sehemu zingine kama vile polisi na wizara ya mambo ya ndani (kwa protection). Kameshasikika kakisema kuwa, hakuna ataeweza kumkamata kwani ana akili nyingi sana na amesha torosha fedha nyingi sana (alizozipata kwa ufisadi) kwa hiyo, kwa sasa hakuna mwenye ujanja wa kumkamata wala kumfikisha mahakamani kwani kanajigamba kuwa kana juwa kula na wakubwa na kucheza na makaratasi.

Mbinu moja ya kifisadi aliyotumia kujitajirisha haraka na ambayo anajigamba kuwa imemtajirisha yeye, na wafanya biashara wengine aliokuwa akiwahudumia na maafisa wakubwa wa TRA (wengine wameshaachishwa kazi lakini washajilimbikizia mali kibao kwa njia za ufisadi walipokuwa kazini), ni ya kuwa clearing agent asiye rasmi. Ki-vipi asiye rasmi? Kwa kushirikiana na baadhi ya mafisadi wa TRA, alikuwa akifunguliwa kampuni za ku-clear mizigo (of course) siyo kwa jina lake, na alikuwa anawaambia matajiri wengi tuu wanaoleta mali kutoka China, Dubai, India na kwingineko watumie kampuni zake, yeye mara nyingi hutowa huduma ya kusafirisha mizigo (containers) toka inapotoka na kui-clear kwa kutumia bandari ya Dar. Na mingine kupitia bandari ya Mombasa na kupitia mipaka ya Kenya na Tanzania, ambako kote huko aliji/walijijengea ka-network chao, yeye, mafisadi wa TRA na polisi ambapo mizigo hiyo anayoihudumia yeye (of course kwa majina yale ya kampuni ambazo si kwa jina lake) hutolewa kwa kulipiwa ushuru mdogo sana. Huwa wanamwambia mwenye mzigo (mteja wao), wewe tutakuchaji million 7 au 10 au 15 au 20 kwa kukutolea kontena lako kila kitu inclusive mpaka tunakukabidhi mwenyewe, wao wanahakikisha gharama zote za kulipia na kulifikisha kontena mpaka kwa mteja halizidi million mbili au tatu au ikizidi sana million tano, zinazobaki ndio mgao wao, yeye na TRA na kina polisi hao wanene huambulia chochote wafunge macho na midomo yao.

Volume ya biashara na (makampuni yaliyosajiliwa na kubarikiwa na TRA kwa zoezi hili) ni kubwa kiasi cha kutamba kuwa alikuwa anaingiza mpaka billioni moja kwa mwezi na hii ni kwa muda mrefu.

Katika Mali alijzojilimbikizia kwa muda mfupi, of course anasema yeye ni mjanja na hawawezi kumshika kwa kuwa mali hizo zote au nyingi katika hizo hajatumia jina lake na hutumia majina ya ndugu, jamaa na marafiki ni pamoja na majumba kadhaa ya Ghorofa Kariakoo, kiwanda, viwanda vya mashuka na mito ambavyo mpaka leo vina exemption za ushuru kwa kutumia mtandao wake na loop-holes za sheria za exemptions, hoteli aliyoinunuwa kwa US$ 8 million hapo Dubai, Hoteli aliyoinunuwa kwa US$ 6 million huko kwao Yemen (asili ya babake ni myemeni, mama yake ni mtanga na ana udugu au ujamaa na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani wa zamani na baadae balozi wa Tanzania uchina na mpaka sasa ni partner wake wa kisiri katika huu ufisadi, aidha kibiashara au kiulinzi (God Father)). Majumba masaki, Dar., majumba keko, majumba mikocheni na kwingine kwingi. Maduka Kariakoo, Uhindini, Mlimani complex, Arusha, Zambia na kwingine kwingi tuu.

Ukitazama mali zote anazomiliki yeye, na ndugu zake na muda alioishi Tanzania, na biashara za halali alizonazo (mwenyewe anaziita "danganya toto") hata uzipigie hesabu maisha huwezi kuja na jibu la faida za kuweza kutajirika kiasi hicho kwa muda mfupi, kwani kwa kipindi kirefu alikuwa nje ya Tanzania na huko nje alikuwa akiajiriwa vikazi vya kawaida na si vya kumpatia utajiri aliokuwa nao, utaona kwamba kaweka mtandao wa kifisadi wa hali ya juu, na anatamba kuwa ana akili anajulikana na hakuna wakumfanya chochote wanene wengi kawatajirisha na wapo mfukoni mwake.

Huyu si mwingine bali ni Saidi Saad au almaarufu kama Saidi Mahonda anajulikana sana Dar. Kwa machachari yake, dharau zake, dhuluma zake (nyingi tuu) na anatambia fedha zake za ufisadi.

Takukuru, Usalama wa taifa, mawaziri waadilifu, waathirika wa ufisadi mnafanya kazi gani au na nyinyi kawatia mfukoni?

Tushirikiane kufichuwa mafisadi.

Habari hii iliwahi kuandikwa kwenye Gazeti la Raia Mwema wiki chache tu zilizopita!! Kumbe ni stori ya siku nyingi sana!!!

TRA ilimeshaidia watu wengi sana kutajirika haraka haraka: ama wafanya biashara au waajiriwa wa TRA. Kama ambavyo law of conservation of energy inavyofundisha, utajiri unaotokana na TRA ni husibababisha serikali kukosa mapato yake tena kwa kiasi kikuba sana, jambo ambalo huchangia serikali yetu kushindwa kujitegemea.
 
Wakuu zangu hivi nyie ndio leo mnayajua haya? mbona ni NDIVYO ILIVYO kwa sisi kina NDIVYO TULIVYO?..mchezo huu upo miaka wala sii huyo peke yake, matajiri woote wanaingiza fedha zao huko na siku hizi wanafungua storage za container ambazo wanakawiza makusudi kutoa mizigo ili mteja alipie gharama za storage. It's a big business kiasi kwamba mizigo mingi ya kwenda nchi za nje hasa Kongo na Rwanda zinapitia Bandari ya Mombasa. Zanzibar nako mchezo tayari umeingia...Ndio Bongo...
 
Nchi yetu kwisha habari yake kumbe hizi news ziko siku nyingi..
Nilizisoma juzujuzi Raia Mwema..kumbe hata hiyo kamati iliyoundwa na bodi ya TRA ni geresha tuu
hayo mambo yanajulikana toka zamani..kwanini wasichukue hatua??? wanawaogopa au wako katika payroll???
Taifa halitatoka kwenye umaskini kama tuteendelea kufumbia macho watu wachache kwa Fedha za magumashi...
 
Ufisadi mwingine unajulikana wazi lakini kwa kuwa umewatajirisha wanene, wengi wao, mpaka wakubwa wa polisi wanapokea mishahara kutoka kwa haka katajiri fisadi. Haka katajiri kanafumbiwa macho na Takukuru na Usalama wa Taifa na hata hiyo polisi yenyewe. Kwa nini? Kwa sababu tuu eti haka kajitu kana fedha na kana kutajirisha kwa kukaachia ukalinde (mafia style). Kana julikana sana haka kajitu kwa kutembelewa na wanene wa TRA na hata mkuu wa kanda maalum ya polisi alikuwa akimtembelea, bila shaka kuchukuwa chake.


Kafisadi haka (kwani ni kajitu kadogo tu, wala hukadhanii) kametajirika kwa record time kwa kushirikiana na mafisadi wenzake wa mostly TRA na sehemu zingine kama vile polisi na wizara ya mambo ya ndani (kwa protection). Kameshasikika kakisema kuwa, hakuna ataeweza kumkamata kwani ana akili nyingi sana na amesha torosha fedha nyingi sana (alizozipata kwa ufisadi) kwa hiyo, kwa sasa hakuna mwenye ujanja wa kumkamata wala kumfikisha mahakamani kwani kanajigamba kuwa kana juwa kula na wakubwa na kucheza na makaratasi.

Mbinu moja ya kifisadi aliyotumia kujitajirisha haraka na ambayo anajigamba kuwa imemtajirisha yeye, na wafanya biashara wengine aliokuwa akiwahudumia na maafisa wakubwa wa TRA (wengine wameshaachishwa kazi lakini washajilimbikizia mali kibao kwa njia za ufisadi walipokuwa kazini), ni ya kuwa clearing agent asiye rasmi. Ki-vipi asiye rasmi? Kwa kushirikiana na baadhi ya mafisadi wa TRA, alikuwa akifunguliwa kampuni za ku-clear mizigo (of course) siyo kwa jina lake, na alikuwa anawaambia matajiri wengi tuu wanaoleta mali kutoka China, Dubai, India na kwingineko watumie kampuni zake, yeye mara nyingi hutowa huduma ya kusafirisha mizigo (containers) toka inapotoka na kui-clear kwa kutumia bandari ya Dar. Na mingine kupitia bandari ya Mombasa na kupitia mipaka ya Kenya na Tanzania, ambako kote huko aliji/walijijengea ka-network chao, yeye, mafisadi wa TRA na polisi ambapo mizigo hiyo anayoihudumia yeye (of course kwa majina yale ya kampuni ambazo si kwa jina lake) hutolewa kwa kulipiwa ushuru mdogo sana. Huwa wanamwambia mwenye mzigo (mteja wao), wewe tutakuchaji million 7 au 10 au 15 au 20 kwa kukutolea kontena lako kila kitu inclusive mpaka tunakukabidhi mwenyewe, wao wanahakikisha gharama zote za kulipia na kulifikisha kontena mpaka kwa mteja halizidi million mbili au tatu au ikizidi sana million tano, zinazobaki ndio mgao wao, yeye na TRA na kina polisi hao wanene huambulia chochote wafunge macho na midomo yao.

Volume ya biashara na (makampuni yaliyosajiliwa na kubarikiwa na TRA kwa zoezi hili) ni kubwa kiasi cha kutamba kuwa alikuwa anaingiza mpaka billioni moja kwa mwezi na hii ni kwa muda mrefu.

Katika Mali alijzojilimbikizia kwa muda mfupi, of course anasema yeye ni mjanja na hawawezi kumshika kwa kuwa mali hizo zote au nyingi katika hizo hajatumia jina lake na hutumia majina ya ndugu, jamaa na marafiki ni pamoja na majumba kadhaa ya Ghorofa Kariakoo, kiwanda, viwanda vya mashuka na mito ambavyo mpaka leo vina exemption za ushuru kwa kutumia mtandao wake na loop-holes za sheria za exemptions, hoteli aliyoinunuwa kwa US$ 8 million hapo Dubai, Hoteli aliyoinunuwa kwa US$ 6 million huko kwao Yemen (asili ya babake ni myemeni, mama yake ni mtanga na ana udugu au ujamaa na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani wa zamani na baadae balozi wa Tanzania uchina na mpaka sasa ni partner wake wa kisiri katika huu ufisadi, aidha kibiashara au kiulinzi (God Father)). Majumba masaki, Dar., majumba keko, majumba mikocheni na kwingine kwingi. Maduka Kariakoo, Uhindini, Mlimani complex, Arusha, Zambia na kwingine kwingi tuu.

Ukitazama mali zote anazomiliki yeye, na ndugu zake na muda alioishi Tanzania, na biashara za halali alizonazo (mwenyewe anaziita "danganya toto") hata uzipigie hesabu maisha huwezi kuja na jibu la faida za kuweza kutajirika kiasi hicho kwa muda mfupi, kwani kwa kipindi kirefu alikuwa nje ya Tanzania na huko nje alikuwa akiajiriwa vikazi vya kawaida na si vya kumpatia utajiri aliokuwa nao, utaona kwamba kaweka mtandao wa kifisadi wa hali ya juu, na anatamba kuwa ana akili anajulikana na hakuna wakumfanya chochote wanene wengi kawatajirisha na wapo mfukoni mwake.

Huyu si mwingine bali ni Saidi Saad au almaarufu kama Saidi Mahonda anajulikana sana Dar. Kwa machachari yake, dharau zake, dhuluma zake (nyingi tuu) na anatambia fedha zake za ufisadi.

Takukuru, Usalama wa taifa, mawaziri waadilifu, waathirika wa ufisadi mnafanya kazi gani au na nyinyi kawatia mfukoni?

Tushirikiane kufichuwa mafisadi.


the only way to clear up this madness is thru assassination ..... i am serious ningekuwa kiongozi ningetengeneza kundi flani la searial killers kwa ajili ya maslahi ya taifa... nikiona kuna mgogoro mkubwa ambayo kisheria hautotupa haki kama taifa... tunamuua huyo fisadi na kundi lake na kuwaacha wengine wajue bila ya kua na ushahidi ili wajue kula NATIONAL SECURITY HAS ITS PRICE... kama wao wanatunyonya na hatuna ushahidi wa wazi na wao tunawaua huku wakijua na bila ya kuwa na ushahidi wa wazi...
 
mmmhh, mtabaki hivyo mlivyo kunung'unika kwenye majarida huku mali zenu zikisombwa, mkiambiwa fanyeji mabadiliko ya system hamtaki ndo kwanza mnakuwa na vihelehele vya kuwachangia watu waende wakachukuwe forms za kugombea tena uongozi, unafikili serikali iliyoimara itafanya upuuzi kama huo? angalia mataifa ambayo leo hii yamepiga hatua ktk uchumi duniani kama yanaendekeza ujuha huu, nini faida ya kuwa na wasomi katika nchi? mikataba mibovu ni yetu, umasikini ni wetu, siasa chafu na zisizo na tija ni zetu, viongozi vihiyo ni wetu, mafisadi ni wetu, hakika nasema Taifa hili kuendelea ni mpaka kizazi hiki kiishe kwanza ktk uso huu wa dunia na kianze kizazi kingine, inatia hasira sana hakuna rasilimali utakayouliza ktk hii nchi ukaambiwa haipo, kila kitu kipo, tuna mali asili nyingi na zenye faida, lakini kwa upeo mdogo na masilahi binafsi ya watawala wetu wanathubutu kuwekeza hata kwenye kuwinda swala tena wanapewa waarabu, huu ni umasikini wa mawazo, na kukosa mipango makini, mtaji kiasi gani unaohitajika kuwinda? mimi natamani kilichobaki kwa sasa ni popote alipokiongozi anayetukwaza ni kuhakikisha watu wanajitoa mhanga tu basi, huu ni upuuzi tena wa hovyohovyo, kila mwaka tunaambiwa uchumi wa taifa umependa kwa asilimia sufuri nukta kadhaa, watu wanakula hela za mapato ya nchi tena bila hata haya, ni sekta ipi yenye unafuu? kote uozo utupu. KONTENA imekamatwa ughaibuni ikiwa na shehena ya mali asili zetu mpaka leo kimya! waziri wa utalii anacheka tu, TICTS uozo mtupu nini kinafanyika kama si ujinga mtupu, Reli ndo kabisa ni bora hata watu wakatembea kwa miguu kuliko huo upuuzi , IPTL, RICHMOND, MEREMETA, nk nini kimetokea kama si kuwakejeli watanzania, inanifanya niaamini ndani ya Tanzania kuna nchi nyingi, hivyo ni ngumu kufikia maendeleo. katiba yenyewe ni butu tena kibogoyo, sheria za nchi zimefanywa kama verse za nyimbo tena soft songs a.k.a R&B, kiasi kwamba hata mafisadi wanazipenda kwani zinawambembeleza na kuwaletea usingizi mnono, kila kukicha ushahidi haujakamilika! hao wanaochunguza wanataka tuamini nini sasa? kwamba kazi imewashinda ama? upelelezi gani unaochukuwa zaidi ya miongo kadhaa? mwisho unaambia mashahidi waliotakiwa kuja kutoa ushahidi walishafariki, hizi ni janja zao tu, wanabaki kuhukumu kesi za wizi wa kuku, bata, mbuzi. akina Endrew chenge wanaendelea kunywa whisky tu kana kwamba hawajafanya lolote baya, siku watanzania wenye nia ya kweli watakapoamka toka kwenye usingizi mzito ambao umewapitia miaka mingi sasa, ndipo hapo tanzania itakapo endelea vinginevyo ni mazingaombwe tu
 
Duh, kumbe hii habari ni ya siku nyingi? Vyombo vyetu vya usalama vimelala usingizi fofofo. Wangeliifanyia kazi tungeliweza kuokoa mabilioni.. ah, --- au zingetumika kwenye safari za mzee na mama??
 
Hapa ndipo quality ya JF inapojiweka wazi yenyewe. Nchi yetu haina mlinzi, wananchi wakijitolea kutoa habari hakuna anayeziamini wala anayeshinikiza uchunguzi. no more to be done ni kuganga maisha tu sasa.
 
Hapa ndipo quality ya JF inapojiweka wazi yenyewe. Nchi yetu haina mlinzi, wananchi wakijitolea kutoa habari hakuna anayeziamini wala anayeshinikiza uchunguzi. no more to be done ni kuganga maisha tu sasa.

Tangu 2008 habari zilishawekwa wazi..... leo ndio wanajifanya kuunda tume???? Agrrr
 
Hats off to JF. Nimeisoma hii habari majuzi tu kwenye gazeti la Raia Mwema kumbe wakuu walishaimwaga humu 2008! Basi tukubali tu kuwa kwa kadiri tutakavyoendelea kuubeba utawala huu tusitegemee jipya zaidi ya nchi kuendelea kuliwa na wahuni hawa wa kiwango cha chini hasa.
 
Angalau hata kapicha,ili na sisi wa huku Bwendanseko tumuone anafananaje...
 
Back
Top Bottom