TRA kwa mtindo huu mtindo mtakusanya kweli kodi?

SUYA

Senior Member
Jun 24, 2009
131
21
Niko Hapa Tra samora nakata road lincece nimeomba ruhusa kazini tangu asubuhi na mapema,nimewahi kabla hawaja fungua,nimeshalipia bank nasubiri hyo stiker malalamiko nikiyokutana nayo yamenichosha .kwan wapo waliolipia tangu tar 27/6 na hawaja pata .najiuliza swali kwa usumbufu huu watu wataacha kuchakach
ua kweli? nawasilisha.
 
Shida nchi yetu iko nyuma miaka 27 hivi ukilinganishwa na jinsi mitandao ilivyorahisisha kazi.Sasa hapo watatafuta mtaalam kutoka World Bank au nchi za wenzetu kuja ku evaluate system.Hivyo usiwashangae lazima uchukue siku moja nzima na ikiwezekana nenda jtatu kabisa
 
Niko Hapa Tra samora nakata road lincece nimeomba ruhusa kazini tangu asubuhi na mapema,nimewahi kabla hawaja fungua,nimeshalipia bank nasubiri hyo stiker malalamiko nikiyokutana nayo yamenichosha .kwan wapo waliolipia tangu tar 27/6 na hawaja pata .najiuliza swali kwa usumbufu huu watu wataacha kuchakach
ua kweli? nawasilisha.

Tembea na risiti uliyolipia achana na rd license
 
Hii taasisi ni USANII kwa kwenda mbele na inahitaji kuangaliwa kwa makini kuna ukiritimba wa kupindukia na watu kijidai miungu watu
 
taratibu ndugu zangu! tatizo la watanzania hatutaki kutumia channel zilizowekwa kufuatilia tatizo na ikiwezekana kulalamika. binafsi, nilishalalamikia benki mbili, kampuni ya simu na sehemu zingine ambako nilidhani sikutendewa haki. na imani yangu ilikuwa kwamba angalau, kwenye organisation yenye watu mia angalao wapo hata 10 wanaojali, na kweli katika baadhi ya sehemu nilikolalamikia uzembe wa baadhi ya wafanyakazi, walionesha kujali na kushukuru kwa taarifa niliyowapa, ukiacha kampuni ya simu Voda, mpaka leo hawataki hata kujibu, nasikia walipeleka majibu TCRA ambako nako nilipeleka malalamiko yangu, nina mpango wa kufuatilia...ukiacha hilo, ndani ya TRA kuna taratibu kwa wafanyakazi na kuna mkataba kwa wateja ambapo baadhi ya huduma zinatakiwa kutolewa ndani ya siku moja, na ikiwa kuna tatizo, mhusika anapaswa kueleza sababu kwa mteja/mlipakodi na awe na ushahidi wa hilo tatizo, mfano akisema system hai-respond, anapaswa kuwa na ushahidi wa kuripoti tatizo hilo kwa wahusika ikiwa atatakiwa kueleza.kibaya ambacho watanzania wenzangu hawataki ni kulalamika wanapokutana na uzembe wa mfanyakazi mmoja au wawili, mfano unapokwenda pale kaunta unaona kuna foleni, lakini anayetoa huduma afuati utaratibu katika kutoa huduma muuulize kwa nini anafanya hivyo, waweza kumuona mkuu wa kitengo na ikibidim meneja wa idara, haiwezekani wote hao wakawa bogus to that extent.zaidi kuna kadi za mrejesho ambazo wateja wanapewa, mteja anaweza na kwa hakika anapaswa kuijaza na kutumbukiza maoni yake katika masanduku ya maoni, isije ikawa tunalalamika nje, lakini wahusika wanaohitaji kuboresha huduma wanatafuta ushahidi kama huo hawaupati
 
Wazembe kweli hao,tembea na risiti ya banki mpaka utakapopata nafasi tena ya kurudi kwa hao wazembe
 
Customer care ni zero katika ofisi za serikali. Nobody cares, yaani wao wanaona kutoa huduma kwa wateja ni kama kuwafanyia favour vile. Mlolongo mrefu sana. Train watu wachache wenye uzalendo walipe vizuri wapatie mtandao wa computer na vitendea kazi bora, kazi ya kukata stika inaweza fanywa ndani ya 30 minutes. Tumia branch za mabenk nchini kote kama collection points. Unakuwa na mtu wa TRA kila branch, mwenye mtandao na printer ya risiti. Katika wakati huu ambapo serikali inashindwa hata kulipa wafanyakazi on time, unahitaji ku-encoutage ulipaji wa kodi ili uwe rahisi na kuufanya kero.

Kuna wakati huwa nasema nchi inaendeshwa kama kijiwe fulani hivi. Wananchi hawaju pa kulalamikia na hawajui nani wa kumlalamikia basi tabu tupu, matokeo ya watu wamekuwa ajasiliamali wazuri kufogi mambo yanayoweza ikosesha nchi mapato. Yaani Tanzania mtu akiteuliwa kuwa Boss wa sehemu kazi yake ni kusubiri kusiani documents na kusubiri mshahara na posho na kuchonga madili ya kifisadi. Watu hawafikiri uboreshaji wa huduma kwa wateja.
 
Wazembe kweli hao,tembea na risiti ya banki mpaka utakapopata nafasi tena ya kurudi kwa hao wazembe

Mkuu sasa kutembea na risiti si unakuwa tena umempatia traffic ulaji maana hatakuacha na yeye. Yaani tabu tupu. Tatizo ni kwamba wengi wa hawa wafanyakazi wa serikalini wamewekwa na watu na wanajua kuwa wanalindwa. Kwa mtu mwenye kuthamini kazi yake atajituma sana tu. Ukiwakuta wanamatumbo makubwaaa!, toothpick midomoni wanajizunguusha kwenye viti tu, huku mkono kila wakati kwenye leso anajifuta jasho na kupiga simu kuuliza madili mbalimbali ya wizi kwa siku hiyo.
 
sijawahi kuona road licence inatoka siku hiyo hiyo.....huwa wanakuandikia tar ya kurudi kwenye ile form uliyojaza kwa ajili ya malipo.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom