Tra hasira za nini kwa chadema?

nguluvisonzo

JF-Expert Member
Dec 27, 2010
515
71
TRA imetangaza vita na CDM,imeanza kuifanyia uchunguzi wa kukwepa KODI,HI mamlaka siko zote huwa naiita chombo cha CCM cha kukandamiza wale wanaoikaidi au kwa wale au Taasisi inayodhaniwa ni hawaipendi CCM au kwa namna moja au nyingine wapinzani wa CCM wanasaidika kutoka kwao.Mimi ninao mfano hai wakati Mrema lyatonga akigombea uraisi kwa kupitia NCCR mara kwanza,katika kampeni zake mkoani Iringa tajiri mmoja alikuwa anamiliki hoteli pale mjini kama sikusahau ilikuwa inaitwa Living light mmiliki nakumbuka alikuwa anaitwa jina la mwisho ni Ilomo,jamaa alifurahi sana kujaza hoteli angalau kwa siku mbili tatu,baada ya hapo alikabwa koo na TRA mpaka akakauka.
Sasa yamehamia kwa CDM kisa wameambiwa mafisadi,wenyewe walikataa lakini Tango mwenyewe kanena wajibu linalowasibu wasikimbilie kuwafunga midomo, sasa CDM wanatafuta nini? kama si njama za kudhofisha CDM?Chombo hiki kimekuwa kikilaumiwa sana juu ya utendaji wake kazi,kimekwumbwa na upepo wa siasa muda mrefu sana,kwa kiwango kikubwa TRA wamekuwa wakifanya kazi kama chombo cha siasa.Natoa ushauri kuwa wafanye kazi zao na siasa waiche pembeni kwani hujui kesho anakuja nani watafanyeje?
Hata misamaha ya kodi ukichunguza sana utaona kuna element za politics ndani yake,TRA ninachosema kuwa msikimbilie kukanusha na kuweka vitisho mjue hakuna mtu mwenye busara akaropoka ni lazima amefanya uchunguzi kwanza ndipo akasema,mnachotakiwa kufanya ni kutafakari kwanza ndio muwe na uamuzi wa kusema au kutokusema,maana unaweza kusema kwa kupinga kumbe mwenzako anayo mengi ni hatari sana.
No Research no ************** to speak.
 
wanacheza na nguvu ya umma sio? hivi hawajui umma ukisema no ni no tu? watakimbia maofisi hayo we wache tu
 
wanahangaika kunyamazisha sauti ya umma.... very big mistake!!!

wakimaliza waende ccm
 
Sielewi kwanini taasisi zinazotakiwa kuwa na heshima kama TRA wanapoongozwa na matakwa ya kisiasa ya baadhi ya watu!
Kwanini TRA wasiheshima professions zao wakafanya kazi bila kupiga makelele kwenye vyombo vya habari kama hivi?
 
walianza na ukanda,ukabila,wakaja na udini then maandamano ya cdm wakasema ni uhaini leo wamekuja na kodi (tax evasion). watamaliza yote lakini wajue mwisho wao umefika. ama tumwage damu km wenzetu kenya kipindi kile au waachie ngazi kwa demokrasia. tushachoka,watz wa sasa hv sio wa kipindi cha miaka ya 80 au 90,tumeelimika na bado tunaendelea kuelimisha vijana wetu.
 
Panapo-nishangaza ni pale watu wanaporusha madongo bila kuweka ushahidi.
 
CCM wanalipz kodi? nadhani kuna kitu hii TRA inatafuta toka kwa nguvu ya umma, wanadhani tutakaa kimyaa tu! nangojea kwa hamu sana upuuzi wa TRA, hovyooooooo kabisa hawa watu
 
Penye Haki hapakosi fitna hivyo CDM wana haki yakudai haki!Fitina inatoka hukoooooooo............!But end of the day People Power!
 
Kinachonifurahisha zaidi kwenye hili ni kwamba ndani ya TRA kuna chadema pia... naamini wanachojifanya ni siri tutakipata na kukiweka wazi..Stay tuned...
 
Back
Top Bottom