TPN, Jamiiforums na Michuzi Blog Yakabidhi Tena Misaada Ya Wahanga Wa Mafuriko

Jul 14, 2008
1,820
1,031
attachment.php

Gari ambayo ilileta misaada ya namna mbalimbali ofisi za Red Cross


attachment.php

Katibu Mkuu wa TPN Mzalendo Method Bakuza, akikabidhi misaada ambayo imekusanywa na TPN na Wadau wake (Jamiiforums.com na Michuzi.blogspot.com) kwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Peter Mlebusi



attachment.php

Mzalendo Sanctus Mtsimbe ambaye ni Rais wa TPN na Meneja Mauzo na Masoko wa SimbaNET (T) Limited akisikiliza maelezo kutoka kwa naibu katibu Mkuu wa Red Cross Bw. Peter Mlebusi

attachment.php

Katika Misaada hiyo SimbaNET Limited ilichangia kiasi cha TZS 1,500,000 ambazo zilitumika kununua misaada hiyo. Misaada hiyo kwa upande wa SimbaNET ilikabidhiwa na Sanctus Mtsimbe, Meneja Mauzo na Masoko wa SimbaNET.


attachment.php

Rais wa TPN Mzalendo Sanctus Mtsimbe, akimsomea orodha ya Misaada itakayokabidhiwa ambayo imekusanywa na TPN na Wadau wake (Jamiiforums.com na Michuzi.blogspot.com) Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Peter Mlebusi



Katibu Mkuu wa TPN Mzalendo Method Bakuza, leo alikabidhi misaada ambayo imekusanywa na TPN na Wadau wake (Jamiiforums.com na Michuzi.blogspot.com) kwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Bw. Peter Mlebusi. Misaada iliyotolewa ni pamoja na: Ndoo 40, Magodoro 40, Sabuni Cartoon 5, Vyandarua 40, Mablanketi 200 vyote vikiwa na thamani ya TZS 1,619,000 Pia kulikuwa na misaada ya vitu mbalimbali kama nguo nyingi sana, viatu, vyombo vya nyumbani vyote vikiwa mizigo kama 10 vikiwa na thamani ya TZS 4,600,000 ambavyo vilichangiwa na wadau mbalimbali.

Katika Misaada hiyo SimbaNET Limited ilichangia kiasi cha TZS 1,500,000 ambazo zilitumika kununua misaada hiyo. Misaada hiyo kwa upande wa SimbaNET ilikabidhiwa na Sanctus Mtsimbe, Meneja Mauzo na Masoko wa SimbaNET. Kampuni ya simu za Mkononi ya Tigo ilichangia kiasi cha mablanketi 200 yenye thamani ya TZS 1,600,000.

Kampeni ya Kuhamasisha uchangiaji imeshamalizika huku TPN na Wadau wake wakiwa wamechangia misaada yenye thamani ya karibia TZS 20 Million. Jumla ya watu 2000 Walichangia kwa SMS na kiasi cha Shilingi TZS 2,037,332 zimekusanywa.

Misaada yote ambayo imekabidhiwa ni kwa ajili ya wahanga wa mafuriko katika maeneo mbalimbali yaliyoathirika na mvua kubwa.

TPN inazindua Mfuko wake wa Uwezeshaji katika Mkutano Mkuu wa Mwaka utakaofanyika siku ya Jumapili Tarehe 14-03-2010 katika ukumbi wa Blue Pearl Hotel Ubungo Plaza.
 

Attachments

  • DSC05743.jpg
    DSC05743.jpg
    69.4 KB · Views: 243
  • DSC05753.jpg
    DSC05753.jpg
    80.9 KB · Views: 234
  • DSC05755.jpg
    DSC05755.jpg
    73.4 KB · Views: 242
  • DSC05752.jpg
    DSC05752.jpg
    75 KB · Views: 233
  • DSC05745.jpg
    DSC05745.jpg
    92 KB · Views: 236
Mtsimbe, hongera sana kwa kazi nzuri mnayoifanya.


Mzalendo Mwafrika asante sana,

Bila ya shaka hizi ni juhudi zetu wote kwa pamoja.

Walau JF, TPN and Michuzi tumeweza kutoa changamoto kuwa we can. TZS 20 Million si kazi ndogo, Wale wengine na ukubwa wao waliweza TZS 50 Million tu!!!
 
Mzalendo Mwafrika asante sana,

Bila ya shaka hizi ni juhudi zetu wote kwa pamoja.

Walau JF, TPN and Michuzi tumeweza kutoa changamoto kuwa we can. TZS 20 Million si kazi ndogo, Wale wengine na ukubwa wao waliweza TZS 50 Million tu!!!

Nimeona TPN wamerusha ujiko kwa TPN tu, tell mi waliambiwa lakini wao hawakurushwa kuwa michango hiyo ni kwa ushirikiano wa JF na Michuzi.
 
Hongera Sanctus.. kwa kuonesha uongozi katika hili..

Mzalendo na wewe pia Maxe; Michuzi na Wadau wote hongera sana kwa team work.

Ninao uhakika wote tumetoa changamoto na kuonyesha njia kwa vitendo!

Asante wote mliotoa support kwa hali na mali.

Shukrani kwa wote pia waliotoa kejeli na kutokuwa na imani na kampeni hii kwani wametumia uhuru wao.

Asanteni pia tuliowashirikisha katika mawazo na mkakati wetu wa kuchangia lakini wakageuka, "kutupiga bao" na kutumia mbinu yetu. Imesaidia pia kupata michango ya kuwasaidia waathirika, maana hilo ndilo lilikuwa lengo letu. Huenda bila sisi wasingetoa misaada wala kufanya kampeni.

Asante sana Wana JF.

Nawaalika pia TPN ili kuendeleza mapambano!
 
Hongera sana mzalendo Sanctus sasa nafikiri tuwakumbuke hata ndugu zetu wa Mwanza nako kuna mafuriko.
 
Hongera sana mzalendo Sanctus sasa nafikiri tuwakumbuke hata ndugu zetu wa Mwanza nako kuna mafuriko.

Asante sana Mkuu.

Tuko pamoja. Tunajaribu kuangalia Strategy ambayo itatupa misaada ya kutosha. Bado iko katika mchakato kuona kama itafaa.
 
..........Walau JF, TPN and Michuzi tumeweza kutoa changamoto kuwa we can. TZS 20 Million si kazi ndogo, Wale wengine na ukubwa wao waliweza TZS 50 Million tu!!!

...................Asanteni pia tuliowashirikisha katika mawazo na mkakati wetu wa kuchangia lakini wakageuka, "kutupiga bao" na kutumia mbinu yetu. Imesaidia pia kupata michango ya kuwasaidia waathirika, maana hilo ndilo lilikuwa lengo letu. Huenda bila sisi wasingetoa misaada wala kufanya kampeni.

Asante sana Wana JF.

Nawaalika pia TPN ili kuendeleza mapambano!

Well done my brother
 
As a matter of fact.. the whole campaign ya kusaidia Red Cross has raised over 100Million Tanzanian Shillings.. !
 
......Hongera Mtsimbe kuwa mzalendo wa kweli,kusimamia hii kazi sio kazi ndogo.
God bless you all abundantly.
 
Mzalendo Mtsimbe,

Shukurani sana kwa kuonyesha ujasiri katika uongozi kwa vitendo na kuwasaidia ndugu zetu. Mungu akubariki.
 
Back
Top Bottom