Mpendanchi-2
JF-Expert Member
- Apr 4, 2009
- 304
- 37
WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, amesema kuwa kuanzia Septemba mwaka huu, kwa mara ya kwanza magari na taasisi za serikali zitaanza kutumia gesi asilia.
Aliweka hilo wazi jana Dar es Salaam wakati alipokuwa akizindua mradi wa kuzalisha gesi iliyosindikwa wenye thamani ya sh bilioni tatu wa kuzalisha gesi iliyoshindiliwa (compressed gas), wa Kampuni ya Pan African Energy (T) Ltd katika eneo la Ubungo.
Ngeleja alisema mara baada ya kumpata mtaalamu mwelekezi na kukamilisha kazi ya kutoa upembuzi yakinifu Julai 2007, jumla ya vituo 12 vitajengwa huku nyumba 38,000 zikiunganishwa na jumla ya magari 8,200 yanatarajiwa kurekebishwa mifumo yake ya nishati, ili yaweze kutumia gesi asilia.
Alisema kuwa mradi huo ni wa awamu mbili - awamu ya kwanza utakuwa katika hatua ya kuhamasisha kwa kuyafanyia marekebisho magari 200 huku hoteli za Southern Sun, Kilimanjaro Kempinski, New Africa, Sea Cliff na Movenpick zitakuwa katika awamu hiyo.
Vilevile taasisi za serikali kama Magereza ya Ukonga na Keko, Jeshi Mgulani na Hospitali ya Muhimbili vitakuwamo katika awamu hiyo, alisema na kuongeza kuwa nyumba 70 katika eneo la Mikocheni, Dar es Salaam, nazo zitajumuishwa katika hatua hiyo.
Katika mradi huo unaosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa kushirikiana na Pan African Energy, unatarajiwa kugharimu kiasi cha dola za Kimarekani milioni tatu.
Kwa mujibu wa Ngeleja, mradi huo unaotekelezwa kwa kushirikiana na makampuni ya ECO Motors kwa pamoja na BICO ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Taasisi ya Teknolojia (DIT), katika hatua za mwanzo, serikali imefanikiwa kukusanya kiasi cha dola za Kimarekani milioni 74.3, huku ukiokoa kiasi cha dola bilioni 1.9 kiasi ambacho kingetumika kuagiza nishati ya mafuta nje.
Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC, Jenerali mstaafu Robert Mboma, alimweleza waziri kuwa shirika hilo lingekuwa na ufanisi zaidi katika kubuni miradi endelevu ya nishati, ila tatizo ni ukosefu wa fedha.
Jenerali Mboma alisema shirika hilo limeshindwa kuchangia miradi kadhaa inayohusu uendelezaji wa nishati kikiwamo kisima namba kumi cha Songosongo.
Kutokana na kutoonesha uwezo wa kuchangia miradi hiyo, mwenyekiti huyo wa bodi alisema serikali imekuwa ikipoteza mapato huku ikidumaza kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Mkurungezi wa Pan African Energy, Peter Clutterbuck, aliipongeza serikali na TPDC kwa kuonesha nia ya kuinua sekta hiyo, kwani itasaidia ukuaji wa uchumi.
Source: Tanzania Daima
------------
Ni move ya TPDC ni nzuri kwa maendeleo ya Watanzania, lakini inashangaza Serikali inatamba kukusanya pesa nyingi za mauzo ya Gas ila haitaki kuwekeza kwenye hiyo miradi ziweze kujizalisha zaidi, na ili iwe na control ya uchumi na energy sector kwa ujumla.
Kwa mfano huu mradi ulikuwa ufanywe na serikali kupitia TPDC pekee ambapo miundombinu yote yaaani Pipeline networking za jiji lote zingemilikiwa na serikali, na hivyo kuwa na control kuanzia bei ya gas kwa wananchi na itakuwa ya kudumu kwa kizazi kijacho. Lakini wameshindwa kutoa pesa hizo zinazokusanywa hadi imebidi TPDC aingie ubia na Panafrican Energy kampuni binafsi ili itoe pesa !!!. wameshindwa kutoa Bil. 3 wakati wamekusanya Bil.70 !!!!!
Je, serikali inaliona hili??? nchi zote zilizoendelea kama UK, Urusi, China, USA, Canada, n.k gas inasambazwa na kampuni za serikali.
Aliweka hilo wazi jana Dar es Salaam wakati alipokuwa akizindua mradi wa kuzalisha gesi iliyosindikwa wenye thamani ya sh bilioni tatu wa kuzalisha gesi iliyoshindiliwa (compressed gas), wa Kampuni ya Pan African Energy (T) Ltd katika eneo la Ubungo.
Ngeleja alisema mara baada ya kumpata mtaalamu mwelekezi na kukamilisha kazi ya kutoa upembuzi yakinifu Julai 2007, jumla ya vituo 12 vitajengwa huku nyumba 38,000 zikiunganishwa na jumla ya magari 8,200 yanatarajiwa kurekebishwa mifumo yake ya nishati, ili yaweze kutumia gesi asilia.
Alisema kuwa mradi huo ni wa awamu mbili - awamu ya kwanza utakuwa katika hatua ya kuhamasisha kwa kuyafanyia marekebisho magari 200 huku hoteli za Southern Sun, Kilimanjaro Kempinski, New Africa, Sea Cliff na Movenpick zitakuwa katika awamu hiyo.
Vilevile taasisi za serikali kama Magereza ya Ukonga na Keko, Jeshi Mgulani na Hospitali ya Muhimbili vitakuwamo katika awamu hiyo, alisema na kuongeza kuwa nyumba 70 katika eneo la Mikocheni, Dar es Salaam, nazo zitajumuishwa katika hatua hiyo.
Katika mradi huo unaosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa kushirikiana na Pan African Energy, unatarajiwa kugharimu kiasi cha dola za Kimarekani milioni tatu.
Kwa mujibu wa Ngeleja, mradi huo unaotekelezwa kwa kushirikiana na makampuni ya ECO Motors kwa pamoja na BICO ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Taasisi ya Teknolojia (DIT), katika hatua za mwanzo, serikali imefanikiwa kukusanya kiasi cha dola za Kimarekani milioni 74.3, huku ukiokoa kiasi cha dola bilioni 1.9 kiasi ambacho kingetumika kuagiza nishati ya mafuta nje.
Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC, Jenerali mstaafu Robert Mboma, alimweleza waziri kuwa shirika hilo lingekuwa na ufanisi zaidi katika kubuni miradi endelevu ya nishati, ila tatizo ni ukosefu wa fedha.
Jenerali Mboma alisema shirika hilo limeshindwa kuchangia miradi kadhaa inayohusu uendelezaji wa nishati kikiwamo kisima namba kumi cha Songosongo.
Kutokana na kutoonesha uwezo wa kuchangia miradi hiyo, mwenyekiti huyo wa bodi alisema serikali imekuwa ikipoteza mapato huku ikidumaza kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Mkurungezi wa Pan African Energy, Peter Clutterbuck, aliipongeza serikali na TPDC kwa kuonesha nia ya kuinua sekta hiyo, kwani itasaidia ukuaji wa uchumi.
Source: Tanzania Daima
------------
Ni move ya TPDC ni nzuri kwa maendeleo ya Watanzania, lakini inashangaza Serikali inatamba kukusanya pesa nyingi za mauzo ya Gas ila haitaki kuwekeza kwenye hiyo miradi ziweze kujizalisha zaidi, na ili iwe na control ya uchumi na energy sector kwa ujumla.
Kwa mfano huu mradi ulikuwa ufanywe na serikali kupitia TPDC pekee ambapo miundombinu yote yaaani Pipeline networking za jiji lote zingemilikiwa na serikali, na hivyo kuwa na control kuanzia bei ya gas kwa wananchi na itakuwa ya kudumu kwa kizazi kijacho. Lakini wameshindwa kutoa pesa hizo zinazokusanywa hadi imebidi TPDC aingie ubia na Panafrican Energy kampuni binafsi ili itoe pesa !!!. wameshindwa kutoa Bil. 3 wakati wamekusanya Bil.70 !!!!!
Je, serikali inaliona hili??? nchi zote zilizoendelea kama UK, Urusi, China, USA, Canada, n.k gas inasambazwa na kampuni za serikali.