Maswali na Majibu kuhusu gari aina ya Toyota Voltz

mkada

JF-Expert Member
Nov 14, 2011
1,200
903
Toyota Voltz.jpg


Wana JF,

Nataka kununua gari ya juu, isiyokula sana mafuta na ambayo matumizi yake ni ya mizunguzo ya biashara zangu mjini. Katika pitapita zangu kwenye mitandao nimeona gari ya Toyota Voltz. Hii gari nimeipenda kwa kweli. Nawaombeni msaada kwa waliowahi tumia hii gari au wanajua sifa, tabia na uwezo wake, ikijumuisha mapungufu yake kama yapo.

Thanx in advance.

WADAU WENGINE WANAHITAJI KUFAHAMU NINI?
Amani iwe kwenu wadau. Nimejichanga na nataka kununua gari aina ya Toyota Voltz kwa matumizi ya nyumbani. Itakuwa ikitumiwa zaidi na wife kwenda job na kurudi umbali wa takriban km 40 kwa siku (kwenda na kurudi)

Naomba ushauri juu ya uimara wa hiyo gari, upatikanaji wa spear parts na mambo mnayoona yanafaa kuyajua.

Natanguliza shukrani.
Wadau naombeni kunijuza juu ya ubora wa gari la aina yya TOYOTA VOLTZ imetokea kuipenda kwa ajili ya matumizi ya kawaida ofisini na binafsi. Ila nina wasiwasi juu ya either ubora na uimara wake. mie naishi mabonde kuinama zaidi ya 1,500km kutoka Dar.

Ushauri wenu utazingatiwa sana na mshukuriwe wote.
Wadau habari za hapa?

Ninataka kununua Voltz kwa sababu naipenda ilivyo hata mishe za mjini naona iko poa.

Je, hizi gari zina matatizo gani common na udhaifu wake ni upi?

Msaada


MICHANGO YA WADAU KUHUSU TOYOTA VOLTZ
NI GARI ZURI ILA KUNA WASIWASI WA SPEA KUPOTEA SOKONI
Hizi gari ukifuatilia historia yake si za toyota na zilitengenezwa na GMC Marekan ili ziuzwe Japan na wakaingia ubia na Toyota kuweka nembo yao tu ili waziuze kirahisi Japan. Ila hakuna mkono wala kifaa cha Toyota pale. Zilitengenezwa gari elfu kumi tu.

Unapoamua kuinunua have idea of that maana nina wasiwasi itafika muda spare zitakua hamna.

Ni gari nzuri kwa mwonekano na mafuta inatumia reasonable.
UZALISHAJI WAKE UMEKOMA, UKILIPATA LITAKUWA KUUKUU MNO
Kwa mtizamo ni gari zuri, cc zake haizidi 2000cc na engine nyingi zake ni vvt-i model 1 zz-fe maana ni kama za platz, vitz, Ist nk. nk

Down side ni kua magari haya yapo katika phase out huko Japan, hayakupendwa sana na soko lake lilidorora ni kuanzia mwaka 2000- mpk 2003 hivi au 2002 ndo ikawa mwisho wa kutengenezwa, hayazalishwi tena ndo maana lolote utakalo lipata litakua chakavu kwa sheria za Tz yaani more than 10 years since production.

Ninahis lina ubaya wake ila binafsi nililipenda nikajaribu kuangalia experience za watu katika mtanadao sikupata ubaya wake.

I hope this helps
HALINA UDHAIFU
Ni gari nzuri sana. Haina madhaifu. Ni gari ya Mmarekani imetengenezwa na NUMMI sema ikauzwa kwenye soko la Japan kati ya mwaka 2002 hadi 2004 kwa jina la Toyota Voltz. Awali ilikuwa inaitwa Pontiac huko North America ikiwa na baadhi ya features za Toyota Matrix.

Engine yake haina tofauti na engine ya Toyota Wish, Toyota Spacio ya 1.8 lt na ya Toyota Premio ya 1.8lt. Kuhusu uimara iko vizuri na spare parts zinapatikana coz watu kibao tu wanazimiliki.
NI GARI IMARA. UTUMIAJI WA MAFUTA NI MZURI. NI COMFORTABLE
Mkuu, Toyota Volz ni gari nzuri sana na imara pia ila uimara wake haufiki kwa Rav 4 old.

Utumiaji wake wa mafuta uko poa kwani ina cc1790 ambayo kawaida inakula 1lt/8-11km kutegemea na mwendo wa dereva.

Kwa upande Confitability iko poa sana ndani ina muundo kama Harrier.

Spear zilikuwa adimu kidogo ila kwa sasa naona zimeongezeka so usijali kuhusu hilo.

NB: Kama barabara unayopita haina shida kipindi cha masika chukua yenye 2 wheel bt kama ni njia zetu zile yenye 4 wheel itapendeza bt ulaji wa mafuta unaongezeka pia.

Ukiwa na swali uliza tu maana naijua vilivyo hii gari
UTUMIAJI WA MAFUTA UPO FAIR
Utumiaji wake wa mafuta mi naona uko fair, nikama wastani wa km 11 na 12 kwa lita. Upatikanaji wa taa zake na bampa kwa dar sijui sababu Dar mimi ni wa ubungo posta uwanja wa Taifa nikimaanisha sio mwenyeji, kwa Arusha huku wanasema ni kwa sababu hizo gari hazijawa nyingi ndio maana bampa na taa zake ni ghari. Ila ni gari nzuri na mimi yangu ni 4WD, kwa hiyo ni imara kwenye zile njia zetu.
 
Kusema ukweli, hata mimi muonekano wake wa nje naupenda, sijafahamu zaidi kuhusu engine yake ila kwa kuwa ni toyota, sidhani kama litakuwa na usumbufu kwa spea.
 
Kusema ukweli,hata mimi muonekano wake wa nje naupenda, sijafahamu zaidi kuhusu engine yake, ila kwa kuwa ni toyota,cdhani kama litakuwa na usumbufu kwa spea.
Hii gari muonekano wake wa nje na ndani halafu ina cc 1800, na pia iko juu inanifanya nisifikirie kabsa gari ingine, na kwa maeneo ya Dar naziona ona sana barabara. Ninachoogopa tu isije zikawa kama Toyota Noah.
 
Hii gari muonekano wake wa nje na ndani halafu ina cc 1800,,na pia iko juu inanifanya nisifikirie kabsa gari ingine,,na kwa maeneo ya dar naziona ona sana barabara,,,ninachoogopa tu isije zikawa kama toyota noah.

Noah zina matatizo gani? Unaongelea new au old model?
 
Hizi gari ukifuatilia historia yake si za toyota na zilitengenezwa na gmc marekan ili ziuzwe japan na wakaingia ubia na toyota kuweka nembo yao tu ili waziuze kirahisi japan. Ila hakuna mkono wala kifaa cha Toyota pale. Zilitengenezwa gari elfu kumi tu.

Unapoamua kuinunua have idea of that maana nina wasiwas itafika muda spare zitakua hamna.

Ni gari nzuri kwa mwonekano na mafuta inatumia reasonable.
 
Noah zina matatizo gani? Unaongelea new au old model?
Sina tatizo na Noah old model, ni nzuri sana, lakini Noah hizi za kuanzia miaka ya 2004 ni nyanya sana, bei rahisi lakini zinachoka mapema sana.
 
Hizi gari ukifuatilia historia yake si za toyota na zilitengenezwa na gmc marekan ili ziuzwe japan na wakaingia ubia na toyota kuweka nembo yao tu ili waziuze kirahisi japan. Ila hakuna mkono wala kifaa cha toyota pale. Zilitengenezwa gari elfu kumi tuu.

Unapoamua kuinunua have idea of that maana nina waswas itafika muda spare zitakua hamna.

Ni gar nzuri kwa mwonekano na mafuta inatumia reasonable
Mkuu unauhakika na ulichokiongea, hebu dadavua kidogo coz hawa jamaa wametoa Toyota Voltz za mwaka 2013 ambazo ni kali balaah, sasa unaposema zilitengenezwa elf kumi tu, zipi hizo kaka?
 
Mkuu everything with regards to what you have asked is here:

The Toyota Voltz was a tall station wagon sold from 2002 to 2004. It was assembled by NUMMI in Fremont, California and marketed by Toyota in its home market of Japan, but curtailed after a disappointing sales volume of just over 10,000 units. The Voltz was produced alongside the Pontiac Vibe in Fremont, California, in the United States by NUMMI (New United Motor Manufacturing, Inc), a joint venture between General Motors and Toyota.

This vehicle is known as the Pontiac Vibe (itself a version of the Toyota Matrix) in North America. The Vibe was exported to the Japanese market (with minor badging changes and right-hand drive configuration) as the Toyota Voltz. Whereas its exterior styling is identical to the Vibe, some interior details differ, matching the interior of the Matrix instead. Curiously, the North American Toyota-branded Matrix was not sold in Japan.(Toyota Voltz Pictures - Car Pictures Gallery)
 
Mkuu everything with regards to what you have asked is here:
The Toyota Voltz was a tall station wagon sold from 2002 to 2004. It was assembled by NUMMI in Fremont, California and marketed by Toyota in its home market of Japan, but curtailed after a disappointing sales volume of just over 10,000 units. The Voltz was produced alongside the Pontiac Vibe in Fremont, California, in the United States by NUMMI (New United Motor Manufacturing, Inc), a joint venture between General Motors and Toyota.

This vehicle is known as the Pontiac Vibe (itself a version of the Toyota Matrix) in North America. The Vibe was exported to the Japanese market (with minor badging changes and right-hand drive configuration) as the Toyota Voltz. Whereas its exterior styling is identical to the Vibe, some interior details differ, matching the interior of the Matrix instead. Curiously, the North American Toyota-branded Matrix was not sold in Japan.(Toyota Voltz Pictures - Car Pictures Gallery)
Sasa nishauri mkuu, hii gari ninunue au nisinunue? Umeniweka njia panda tayari mkuu.
 
Mkuu unauhakika na ulichokiongea, hebu dadavua kidogo coz hawa jamaa wametoa Toyota Voltz za mwaka 2013 ambazo ni kali balaah, sasa unaposema zilitengenezwa elf kumi tu, zipi hizo kaka?

Wewe ndio una uhakika? Hebu nioneshe picha ya hiyo voltz ya 2013? Voltz zimetoka 2002-2004 basi
 
Mkuu kama una misele ya kibiashara kwa nini usinunue Vitz?

Ushauri tu lakini mkuu kwa sababu nionavyo mimi hiyo Voltz ni 1800 cc which means more consumption when it comes to fuel. Why use 40,000 daily when you can use half of that money with Vitz kama ni misele ya kibiashara?

Mtazamo tu
 
mkuu kama una misele ya kibiashara kwa nini usinunue Vitz?

Ushauri tu lakini mkuu kwa sababu nionavyo mimi hiyo Voltz ni 1800 cc which means more consumption when it comes to fuel. Why use 40,000 daily when you can use half of that money with Vitz kama ni misele ya kibiashara?

Mtazamo tu
Mkuu hiyo ni option mojawapo niliyonayo, sema Vitz iko chini sana mkuu, anyway ikishindikana nitahamia huko mkuu, Vitz is my second option nikikosa gari la juu.
 
mkada Vitz ni kweli ikitoka kiwandani iko chini. Ila cha kufanya ni kuinyanyua kwa spacer na kubadili matairi kutoka yale ya kiwandani ya R13 weka sport rim za R14. Hapo Vitz inatulia barabarani na inaruka matuta na mashimo mpaka utaipenda. Binafsi nimeshangaa kama unajali mafuta unanunua injini ya 1800cc wakati Vitz zipo hadi za 970cc. Nimeshatumia Vitz ya engine ya 970cc kwa ruti ndefu za Mwanza, Arusha na Mbeya, iko fresh inakula km 15 kwa lita moja. Na spidi inagonga mpaka 140. Mpaka mashambani Vitz inakwenda, asikudanganye mtu.
 
Last edited by a moderator:
mkada Vitz ni kweli ikitoka kiwandani iko chini. Ila cha kufanya ni kuinyanyua kwa spacer na kubadili matairi kutoka yale ya kiwandani ya R13 weka sport rim za R14. Hapo Vitz inatulia barabarani na inaruka matuta na mashimo mpaka utaipenda. Binafsi nimeshangaa kama unajali mafuta unanunua injini ya 1800cc wakati Vitz zipo hadi za 970cc. Nimeshatumia Vitz ya engine ya 970cc kwa ruti ndefu za Mwanza, Arusha na Mbeya, iko fresh inakula km 15 kwa lita moja. Na spidi inagonga mpaka 140. Mpaka mashambani Vitz inakwenda, asikudanganye mtu.
Barikiwa sana kaka, I think now am decided. In fact uwezo wa kununua gari kubwa ninao lkn uwezo wa kujaza kila siku mafuta ya elf 30 nahisi nitaua familia, thanx bro, umekuwa msaada sana.
 
mkada Vitz ni kweli ikitoka kiwandani iko chini. Ila cha kufanya ni kuinyanyua kwa spacer na kubadili matairi kutoka yale ya kiwandani ya R13 weka sport rim za R14. Hapo Vitz inatulia barabarani na inaruka matuta na mashimo mpaka utaipenda. Binafsi nimeshangaa kama unajali mafuta unanunua injini ya 1800cc wakati Vitz zipo hadi za 970cc. Nimeshatumia Vitz ya engine ya 970cc kwa ruti ndefu za Mwanza, Arusha na Mbeya, iko fresh inakula km 15 kwa lita moja. Na spidi inagonga mpaka 140. Mpaka mashambani Vitz inakwenda, asikudanganye mtu.

Mkuu ni kweli kabisa vitz ni gari nzuri hasa kwny fuel cons mm ninayo sisumbuki kabisa ila tu ni muhimu uiwekee spacer ni 50,000 then unatembea uzuri tu
 
Kwa wale wenye experience wa haya magari naombeni mnisaidie.

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk
 
Back
Top Bottom