Judgement
JF-Expert Member
- Nov 13, 2011
- 10,327
- 4,779
Nimeshaona wazee wa kiume wakiwakataa, watoto walio wapata nje ya ndoa.
Aidha kuna wengine huwakubali, bt kw kificho ambapo inafanywa kua secret kati ya Mama aliemzaa mtoto huyo, Mtoto mwenyewe na Baba muhusika, ili mradi tu Mama aliepo madarakani aendelee kutokujua siri hiyo.
Mzee Ibrahim ni mmoja kati ya wahusika juu ya kadhia hii.
Akiwa ndani ya ndoa na mkewe Mama Pera, Mzee Ibra akawa amepata Mtoto wa kiume pembeni na mji aliokua anaishi.
Shughuli zake za minadani zilimkutanisha na Bi. Sara huko kijijini na kupata kijana aitwae Beka.
Mz Ibra hakutaka kabisa mkewe ajue , hata hivyo alijitahidi sana kua anapeleka kiasi cha matumizi.
Matumizi ambayo hayakua yakikidhi haja.
Kissa mkassa Beka alimlanda Mz Ibra kwa kila kitu, Sura, Umbo, Tambo, Pozi, wajihi wote jumla. Kiasi hata kuwazidi ya waliozaliwa ndoani ufanano na Baba yao.
Kidudu mtu mmoja akatokea na kwenda mueleza Mke wa Mz Ibra, kuhusu Beka.
Katika hali isiyozoeleka sana mkewe Mz Ibra alidodosa chini kwa chini na hatimae akafika kwa Mama wa Beka.
Alifika na kujitambulisha na kumwomba Mama Beka amruhusu aondoke na Beka (age 7) aendenae akalelewe na nduguze.
"Roho inaniuma kuona mtoto huyu upate nae shida kwa kumlea wewe peke yako kwa shida, wakati Babaake ni mwenye uwezo" aliongea Mkewe Mz Ibra maneno hayo.
Mama Beka hakua na pingamizi, alimridhia na akaondoka na Beka.
Mama Pera (mkewe mz Ibra) alifika na Beka nyumbani, hakika Mz. Ibra alifadhaika , kope zikimcheza kushoto kwenda kulia. Hata hivyo mkewe alimfariji kwa kumuondolea mfadhaiko.
Beka alilelewa pale kwa mapenzi yaliotakiwa mtoto apewe.
Hivi niandikavyo Beka ni mfanyabiashara akichukua bidhaa Thailand, China, Bangkok, kuleta Tanzania.
Mama mzazi wa Beka alikwishafariki zamani, Mama pekee anafaidi nguvu ya Beka ni Mama aliemlea.
Nduguze wote aliowakuta kwa Mz Ibra kawafungulia maduka.
Nyumba mpya kawajengea wazazi wake Mbezi beach, na kuwahamisha toka Kawe- ukwamani.
Aidha kuna wengine huwakubali, bt kw kificho ambapo inafanywa kua secret kati ya Mama aliemzaa mtoto huyo, Mtoto mwenyewe na Baba muhusika, ili mradi tu Mama aliepo madarakani aendelee kutokujua siri hiyo.
Mzee Ibrahim ni mmoja kati ya wahusika juu ya kadhia hii.
Akiwa ndani ya ndoa na mkewe Mama Pera, Mzee Ibra akawa amepata Mtoto wa kiume pembeni na mji aliokua anaishi.
Shughuli zake za minadani zilimkutanisha na Bi. Sara huko kijijini na kupata kijana aitwae Beka.
Mz Ibra hakutaka kabisa mkewe ajue , hata hivyo alijitahidi sana kua anapeleka kiasi cha matumizi.
Matumizi ambayo hayakua yakikidhi haja.
Kissa mkassa Beka alimlanda Mz Ibra kwa kila kitu, Sura, Umbo, Tambo, Pozi, wajihi wote jumla. Kiasi hata kuwazidi ya waliozaliwa ndoani ufanano na Baba yao.
Kidudu mtu mmoja akatokea na kwenda mueleza Mke wa Mz Ibra, kuhusu Beka.
Katika hali isiyozoeleka sana mkewe Mz Ibra alidodosa chini kwa chini na hatimae akafika kwa Mama wa Beka.
Alifika na kujitambulisha na kumwomba Mama Beka amruhusu aondoke na Beka (age 7) aendenae akalelewe na nduguze.
"Roho inaniuma kuona mtoto huyu upate nae shida kwa kumlea wewe peke yako kwa shida, wakati Babaake ni mwenye uwezo" aliongea Mkewe Mz Ibra maneno hayo.
Mama Beka hakua na pingamizi, alimridhia na akaondoka na Beka.
Mama Pera (mkewe mz Ibra) alifika na Beka nyumbani, hakika Mz. Ibra alifadhaika , kope zikimcheza kushoto kwenda kulia. Hata hivyo mkewe alimfariji kwa kumuondolea mfadhaiko.
Beka alilelewa pale kwa mapenzi yaliotakiwa mtoto apewe.
Hivi niandikavyo Beka ni mfanyabiashara akichukua bidhaa Thailand, China, Bangkok, kuleta Tanzania.
Mama mzazi wa Beka alikwishafariki zamani, Mama pekee anafaidi nguvu ya Beka ni Mama aliemlea.
Nduguze wote aliowakuta kwa Mz Ibra kawafungulia maduka.
Nyumba mpya kawajengea wazazi wake Mbezi beach, na kuwahamisha toka Kawe- ukwamani.