Tosamaganga Investment Group

SolarPower

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
223
27
Wakuu,

Habari za siku nyingi wale wote mliosoma katika shule yetu ya TOSAMAGANGA mkoani Iringa.

Kama wadau wakuu wa Tosamaganga, naomba tuanzishe TOSAMAGANGA INVESTMENT GROUP ambapo lengo kuu la taasisi yetu hii litakuwa ni KUIBORESHA KITAALUMA KWA KIWANGO CHA JUU SANA SHULE YETU HIYO YA TOSAMAGANGA.

Naomba pia mniruhusu nipendekeze yafuatayo:-

1. Taasisi yetu hii ya Uwekezaji Katika Taaluma itaendeshwa kama SOCIAL BUSINESS ENTERPRISE--Naomba tujifunze zaidi kuhusu SOCIAL BUSINESS ENTERPRISES toka www.muhammadyunus.org.

2. Kila mmoja wetu anunue angalau Hisa zenye thamani ya shilingi milioni moja. Bei ya Hisa Moja inapendekezwa iwe shilingi za kitanzania elfu 10 tu.

Wakuu, Kama WAZO HILI litakubalika binafsi pamoja na familia yangu tutanunua Hisa za angalau shilingi milioni 5 ifikapo mwisho wa Mwezi wa Tisa Mwaka Huu wa 2012.

Naomba kuwasilisha.

Namba yangu ya simu ni 0654-467758 na nilisoma Tosamaganga mwaka 1984 mpaka 1986 EGM. Enzi za Marehemu Mpogole (MWENYEZI MUNGU amrehemu.)
 
SolarPower,

Sorry to share that Tanzanian Youth, especially those you meet through digital social forums, self Economic Emancipation is not their priority rather gossiping is. They are here for complaining, condemning and criticizing not looking to derive nor share solutions.

I second this initiative but very unfortunate I'm naturally disqualified. May be I'll copy your move and invite my ZOO colleagues if they're available here.
 
SolarPower,

Sorry to share that Tanzanian Youth, especially those you meet through digital social forums, self Economic Emancipation is not their priority rather gossiping is. They are here for complaining, condemning and criticizing not looking to derive nor share solutions.

I second this initiative but very unfortunate I'm naturally disqualified. May be I'll copy your move and invite my ZOO colleagues if they're available here.

Asante kwa post yako na kwa kuunga mkono wazo. Naamini tutafika.
 
Wakuu,

Tuliosoma Tosamaganga, mbali na kutoa mawazo yetu hapa, napendekeza tutafutane, tukutane na kisha kuanzisha mawasiliano rasmi kati yetu. Tunaweza kukutana kimakundi katika kila mkoa tukianza na mikoa kama ya Dar es Salaam, Iringa na Mbeya na kuona matokeo yake. Mimi napatikana kupitia namba 0654 467758.
 
Back
Top Bottom