Top 5 ya wakali wa chorus Tanzania 2010-2012

Kabota

Member
Aug 15, 2009
63
10
Muziki wa Hip hop hauwezi kuwa mtamu pasipo kuwa na chorus nzuri. Mwenye wimbo anaweza kuamua kuimba mwenyewe chorus ama kutafuta msaniii mwingine atakayemuimbia chorus ya kuvutia. Mchango wa msanii anayetoa melody nzuri ya chorus kamwe hauwezi kubezwa. Kuna wale ambao huvutiwa tu na chorus ya wimbo. Mara nyingi tumewahi kuzipenda nyimbo kwasababu tu ya chorus iliyoimbwa kwa ustadi mkubwa.


Tumeamua kuangalia kwa umakini kabisa pasipo upendeleo wowote kutafuta ni msanii gani aliyeshirikishwa zaidi na wasanii wa hip hop kuanzia mwishoni mwaka juzi (2010) hadi leo na kuwaweka kwenye Top five. Katika kupata list hii tumeangalia uzuri wa chorus yenyewe na namna wimbo ulivyohit. Kigezo cha wingi wa nyimbo alizoshirikishwa msanii hakikuwa na mchango mkubwa katika kupata wasanii bora wa chorus za hip hop mwaka 2010 – 2012.


Kuna wasanii wakubwa ambao ungehisi wanaweza kuwa kwenye list hii lakini ukweli ni kwamba nyimbo walizoshirikishwa aidha hazikuwa na impact yoyote, zilikuwa nyimbo za kawaida sana ama idadi yake haitoshi kumfanya aingie kwenye Top five. Wasanii hao ni pamoja na Ali Kiba na Diamond ambao licha ya kutokuwepo kwenye list hii wameendelea kufanya vizuri kwenye kazi walizofanya wenyewe.


Katika list hii hatukupenda kuwachanganya wasanii wa kiume na wa kike pamoja. Tutaangalia namna ya kuwaweka kwenye chart yao inayojitegemea.


Wafuatao ndio wasanii waliofanya vizuri zaidi kwa kushirikishwa kwenye chorus za wasanii wa Hip Hop nchini Tanzania mwaka 2010 –2012.

Click hapa kuwafahamu wakali hao:

DAILY ENTERTAINMENT TAKE AWAY: Top 5 ya wakali wa chorus Tanzania 2010-2012
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom