Uwezo Tunao
JF-Expert Member
- Nov 14, 2010
- 6,942
- 1,190
Waziri Mkuu wa Zamani nhini Uingereza (1997 -2007), Tony Blair, leo hii alasiri amekiri majuto mazito moyoni kwa maafa nchini Iraq wakati wa vita.
Kiongozi huyu mstaafu alielezea jinsi anavyoendelea kukumbwa na MISONONEKO MIZITO SANA MOYONI kufuatia maafa yaliotokea katika vita hivyo.
Alifafanua kwamba anasikitikia sana maisha ya ama wanajeshi wake, Wamarekani, Wairaki, Watumishi wa Mashirika ya kimataifa na raia wa kawaida pale Iraq.
Ndugu Blair alikiri hayo leo hii saa 10:53 alielezea hisia zake hizo wakati akiwa kikaangoni mbele ya Tume ya Uchunguzi juu ya ushiriki wa Uingereza katika vita nchini Iraq (the British Commission of Inquiry into Iraq War - BCIIC) ikiongozwa na Mwenyekiti wake John Chilot.
Pamoja na yote, Waziri Mkuu mstaafu huyo alisisita kwa uzito wake kwamba vita dhidi ya Iraq ilikua haikwepeki kwa vyovyote vile kutokana na vikundi haramia na hatari vikifadhiliwa na mikono mibaya huku vikiwa vimepandikizwa chuki za kidini na kuhatarisha maisha kwa ulimwengu mzima.
Kikao cha tume kitaendelea siku ya jumanne wiki ijayo kwa kuleta viongozi wengine wazito zaidi kikaangoni.
Kwa habari zaidi, fuatilia katika mikondo hii: Iraq Inquiry na C-SPAN | Capitol Hill, The White House and National Politics
HOJA YANGU:
Tunajifunza nini kama nchi na vile vita vya Iraq na misingi ya kuchochewa au kufadhiliwa migawanyiko kwa misingi ya kidini ndani ya taifa letu?
Na kitendo cha kiongozi wa ngazi ya juu duniani kama Waziri Mkuu mstaafu wa Uingereza anapowekwa kikaangoni vikali kiasi hiki panapoonekana kuna MASWALI MAZITO YANAYOHITA MAJIBU KITAIFA, sisi hapa kwetu somo ni nini hadi hapo kwa viongozi wetu ama walioko madarakani au wanaopumzika nyumbani?
SOURCE: C-Span2 TV.
Kiongozi huyu mstaafu alielezea jinsi anavyoendelea kukumbwa na MISONONEKO MIZITO SANA MOYONI kufuatia maafa yaliotokea katika vita hivyo.
Alifafanua kwamba anasikitikia sana maisha ya ama wanajeshi wake, Wamarekani, Wairaki, Watumishi wa Mashirika ya kimataifa na raia wa kawaida pale Iraq.
Ndugu Blair alikiri hayo leo hii saa 10:53 alielezea hisia zake hizo wakati akiwa kikaangoni mbele ya Tume ya Uchunguzi juu ya ushiriki wa Uingereza katika vita nchini Iraq (the British Commission of Inquiry into Iraq War - BCIIC) ikiongozwa na Mwenyekiti wake John Chilot.
Pamoja na yote, Waziri Mkuu mstaafu huyo alisisita kwa uzito wake kwamba vita dhidi ya Iraq ilikua haikwepeki kwa vyovyote vile kutokana na vikundi haramia na hatari vikifadhiliwa na mikono mibaya huku vikiwa vimepandikizwa chuki za kidini na kuhatarisha maisha kwa ulimwengu mzima.
Kikao cha tume kitaendelea siku ya jumanne wiki ijayo kwa kuleta viongozi wengine wazito zaidi kikaangoni.
Kwa habari zaidi, fuatilia katika mikondo hii: Iraq Inquiry na C-SPAN | Capitol Hill, The White House and National Politics
HOJA YANGU:
Tunajifunza nini kama nchi na vile vita vya Iraq na misingi ya kuchochewa au kufadhiliwa migawanyiko kwa misingi ya kidini ndani ya taifa letu?
Na kitendo cha kiongozi wa ngazi ya juu duniani kama Waziri Mkuu mstaafu wa Uingereza anapowekwa kikaangoni vikali kiasi hiki panapoonekana kuna MASWALI MAZITO YANAYOHITA MAJIBU KITAIFA, sisi hapa kwetu somo ni nini hadi hapo kwa viongozi wetu ama walioko madarakani au wanaopumzika nyumbani?
SOURCE: C-Span2 TV.