Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Leo asubuhi wakati wa kipindi cha udondozi wa magazeti, Tom Chilala alijitokeza ghafla na kukatiza habari aliyokuwa akisoma mfanyakazi mwenzake, kutoka kwenye gazeti la Mzalendo. Habari hiyo aliyoikatiza,ilihusu namna kesi kati ya Tanesco na Dowans ya hivi majuzi, iliyopelekea kampuni hiyo ya umma kuhukumiwa kulipa Dowans mabilioni ya fedha, ilivyoendeshwa. Kwa yeyote aliyekuwa akifuatilia kipindi hicho, atakubaliana na mimi ya kwamba, kwa namna mtangazaji huyo alivyolazimisha kusitishwa kwa habari husika, bila shaka kuna jambo lililopo kwenye habari hiyo ambalo hakutaka litoke hewani. Swali la kujiuliza ni kwanini? Na je, yeye anahusikaje katika sakata la Dowans,au kawekwa mfukoni na wahusika wenyewe! Naomba yeyote anayeweza kutoa mwanga katika maswali hayo anisaidie.