only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa anatarajia kuiuzia Serikali ya Wilaya ya Ukerewe nyumba yake iliyo katika eneo la Bomani mjini Nansio ambayo imekuwa ikitumiwa na viongozi wa ngazi ya kitaifa wanaokwenda wilayani humo kwa ziara za kikazi. Uamuzi huu umetangazwa leo na mkuu wa wilaya hiyo ndugu Mary Tesha wakati wa kuwakilisha taarifa ya maendeleo ya wilaya hiyo mbele ya waziri mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda anayeendelea na ziara ya siku saba mkoani Mwanza. Mkuu wa wilaya aliendelea kusema kuwa wamepata nyumba mbili ambazo wanadhani zitafaa kuwa makazi ya viongozi wa kiserikali hasa wa ngazi za juu wanapofika Ukerewe..Moja ni ya Mzee Msekwa na nyingine ni ya Masumbuko Mtani.
Mkuu huyo wa wilaya aliendelea kusema kuwa mwaka 2010 wakati JK akiwa ziarani huko Ukerewe aliagiza kujengwa kwa nyumba mpya ya mkuu wa wilaya, lakini bahati mbaya fedha ya mgao haikutosha.
My take:
Hivi ni kweli Serikali imeshindwa kujenga nyumba mpaka inunue toka kwa wananchi wake? Hii serikali ni dhaifu kiasi gani? Yani imezidiwa umaskini na wananchi wake. Tanzania ndio nchi ya kwanza ambayo raia wake wana pesa kuliko nchi yenyewe. Aibu kwa hii serikali.
Mkuu huyo wa wilaya aliendelea kusema kuwa mwaka 2010 wakati JK akiwa ziarani huko Ukerewe aliagiza kujengwa kwa nyumba mpya ya mkuu wa wilaya, lakini bahati mbaya fedha ya mgao haikutosha.
My take:
Hivi ni kweli Serikali imeshindwa kujenga nyumba mpaka inunue toka kwa wananchi wake? Hii serikali ni dhaifu kiasi gani? Yani imezidiwa umaskini na wananchi wake. Tanzania ndio nchi ya kwanza ambayo raia wake wana pesa kuliko nchi yenyewe. Aibu kwa hii serikali.