Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,172
Tokea nimemwona akiwa mahakama ya hakimu mkazi hapa Singida majuma mawili yaliyopita nimekuwa nikijiuliza sana nini hasa kilichomfanya Dr huyu na maarifa makubwa aliyonayo hadi kuingizwa katika siasa za kimabavu na matusi za CDM na CCM?. Dr huyu nakumbuka wakati akinifundisha nikiwa pale Udsm miaka miwili iliyopita niliamni kabisa ana sifa ya uchambuzi wa siasa na sio kuhusika moja kwa moja katika siasa kama alivyojikuta anafanya. CDM wameamua kumtumia ili kukuza profile yao Iramba - CCM nao kwa kuwa ustaarabu wake Dr wakaamua kumchezesha kwata la kumchomekea katika kuhusika na fujo kule Ndago. Tokea sakata hili litokee, Dr wa watu hajatamka neno, yamkini inawezekana anajuta kimoyo kwamba "yamkini ningejua...... nisingefanya hivi". Kwa sasa hata majukumu yake ya Udean aliyoyapata juzi juzi UDSM hawezi kuyatekeleza ipasavyo kwa sababu ya kesi uchwara inayomkabili huku Singida. Leo tena nitafika mahakamani ili nikaone atakavyokuwa mpole, mnyonge, msikivu, mtulivu na mwenye kila hali ya kuonewa huruma mbele ya hakimu ambaye ana shahada moja tu ya sheria ilihali yeye akiwa ni Daktari wa Falsafa. Hakika Dr wangu umeingia mkenge, tena mkenge kama anaouingia mwenzako Zitto Kabwe katika kashfa ya kupokea rushwa katika kupitia Kamati ya Nishati Madini.
hata nelson mandela alipokuwa akiwapinga makaburu aliambiwa maneno ya kuvunja moyo, kwamba atajutia.
siasa za majitaka.