shukuru mungu waulize wenzio huko mazimbu road na lukobe wakupe habari kamiliMbona mi nakaa kihonda bima hapa hamna shida ya maji
mkuu hii biashara nilipiga sana na ka gari ka dingi kakaja kufa ila hela nje nje yani kama mtu unakirikuu ndo umeulaaPolen Mkuu, vp na kwa Wakubwa kwao maji Hamna mfano RC kambi za jeshi n.k lakin mkuu hako nako kafursa cha kutokea, hata kama una corolla gx Unapiga nako kazi Ndo 1=500? hataliii
Inaongelewa kihonda kwa chambo ndugu. Fika kule uone. Infact ni kama hawa jamaa wanafanya makusudi kutengeneza uhaba ili wafaidike kupitia malori ya kuuza maji ambayo nadhani wanakuwa na maslahi nayo. Watu wa kihonda wakikomaa kidogo, huzugwa kwa kuletewa maji kama mara mbili hivi kisha hujisahaulisha kabisa. Kibaya zaidi kila mwisho wa mwezi wananchi hupelekewa bili za maji. Ni shida.Mbona mi nakaa kihonda bima hapa hamna shida ya maji
BIMA YA AFYA NI JIPU LA KULIANGAZIA
Wanabodi, hongereni kwa constructive criticism.
Leo nimeona nije na hili suala la BIMA ya afya, to be specific, NHIF.
Kwanza niwapongeze waliokuja na wazo hili, ni msaada mkubwa hasa kwa watumishi wa umma ambao majority hawana uhakika wa kujiwekea akiba kwa ajili ya matibabu.
Lakini kwa upande mwingine BIMA hii imekuwa kama ni upigaji wa mishahara ya watumishi wa umma kutoka kwenye makato ya mishahara yao baada ya kukatwa kwa lazima kama sheria inavyoelekeza.
Nasema ni upigaji kwa sababu makato hayaendani na huduma zitolewazo pindi wanapozihitaji.
Katika kuhusisha suala hili, HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA nitaichukulia kama CASE STUDY.
Juzi nilikuwa na uhitaji wa huduma ya afya kwa kutumia mpango wa BIMA ya afya ya NHIF. Nilifika mapokezi na kuandikisha kama kawaida. Nilipoingia ndani ili nihudumiwe, kero zifuatazo zilinikuta:-
1/ Upungufu wa wahudumu:
Matabibu ni wachache na waliopo wanaanza asubuhi mpaka jioni bila ya kuwepo kwa wengine waingie kwa shift. Hivyo kwa mtazamo wangu huwa wanachoka kwa masaa mengi ya kazi.
Pia mtu wa maabara alikuwa mmoja kwa siku hiyo kuhudumia msululu wa watu kwa siku nzima.
2/ Majibu na kauli mbaya kwa wateja:-
Ilipofika saa 11 alibaki Tabibu mmoja wa mlango wa Wazee ambaye alikuwa akitoa kauli chafu kwa wateja pale walipohoji uharaka wa huduma. Hii ikizingatia kuwa kuna kinamama, watoto, wazee na wajawazito waliokuwa hapo tangu asubuhi na hawapata huduma kwa wakati.
3/ Upungufu wa vifaa tiba:-
Kuna baadhi ya vipimo havipatikani kwenye jengo hilo mpaka uambiwe ukafuate upande wa HOSPITALI ya MKOA.
Pia baadhi ya dawa hazipatikani kwenye dirisha la dawa mpaka uende Pharmacy za nje.
HITIMISHO:-
Naomba kero za hapo juu zifanyiwe kazi ili huduma ziendane na makato ya lazima kwenye mishahara ya watumishi wa umma.
N.B:-
MALAIKA MZIMA JF USIIGUSE TENA HII KITU, NI YA MUHIMU KWETU.