Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Bwana na akainyooshe fimbo ya nguvu zake kutoka mbinguni ili Rais Magufuli awe na enzi kati ya maadui zake wote. Amina
 
Mfalme Sulemani alimwomba mwenyezi mungu ampatie hekima katika utawala wake. Wapo wanaokushangilia kwa kazi iliyombele yako,"Kutumbua unaowaiita Majipu" bila sheria kufatwa.

Kuna msemo wetu unasema, Kufa-Kufaana.Ila, hakuna jambo lisilo na mwisho.Tumeona baadhi ya viongozi uliowachagua wanadiriki kuongea maneno yasio ya busara kabisa,mpaka kudiriki kuwaambia watu watajuta kuzaliwa kwao!.

Hivi Majuzi tumekusikia, unazungumzia Suala la Fixed Deposit Account( FDA), na kutaja TRA na taasisi nyingi za serikali ikiwemo TEA kuwa wameweka hela kwenye FDA ili wapate interest huku shule hazina vyoo,madarasa n.k.

Ukaenda mbali zaidi ukasema, ma chief executive wengi wanakubaliana na hawa wenye mabenki.Waziri upo hapa unanisikia,message sent and delivered.
Kesho yake, tukasikia Governor wa benki kuu(BOT),mchumi aliobobea akielezea Taasisi kuweka hela kwenye FDA si kosa.

Juzi tu hapa, tumemsikia tena Msajili wa hazina, kama kumkosoa raisi tena. kuweka hela kwenye FDA si kosa na taasisi za serikali nyingi zilikua zinaweka hela kwenye FDA miaka ya nyuma.

Kosa ni hizo interest kutumika tofauti.Na akasema ni ngumu kuiba hizo hela maana mwisho wa siku kuna ukaguzi huwafanywa.

Leo, nimesoma gazeti la mtanzania. Nimeona utumbuaji wa kimya kimya Mamlaka ya Elimu,naibu waziri wa elimu alipoulizwa kuhusina na hizo taarifa akasema hajui na hana hizo taarifa . Where are we headed? wa Tanzania wapi tulikosea?

Mwisho kabisa, Nakutakia maisha mema mh.raisi.
 
mkuu mbona nimesoma bandiko lako sijaona unamshauri Mh. Rais? au bado unaendelea kuandika?
 
Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa yenye mito isiyopungua 100 isiyokauka kipindi chote cha mwaka. Lakini cha ajabu mji wa Morogoro, chini ya MORUWASA, unakabiliwa na uhaba mkubwa sana wa maji. Kuna mitaa mingi sana, mathalani Bigwa, hukaa kwa muda wa miezi mpaka mitatu bila maji. MORUWASA, bila aibu, kila mwisho wa mwezi hupita na kusoma mita na kuwaletea bili za maji wenye mita .Miitaa kama Kihonda maji kwao ni almasi-hununua kwenye magari ya wauza maji, na uhaba huu wa maji yaelekea hauna jawabu. Ndoo MOJA ya maji, ya lita 20, huuzwa shilingi mia tano za kitanzania.

Huwezi kuwa nchi ya viwanda ikiwa maji yasiyohiyaji akili HAYAPATIKANI-just laying pipes na kusambaza kwa umma/watu!

Nionavyo mimi Shida kubwa kwa taasisi nyingi za umma, ikiwemo MORUWASA, ni: Kuwa na watumishi wengi wasio na uwezo,mizigo, wapiga dili na wanaofanya kazi kwa mazoea na pengine wenye maslahi na uhaba wa huduma za umma (mathalani wana magari ya kuuza maji, wana visima, au huduma ambazo zikiwemo kwenye idara za umma wanakosa dili). HAKUNA UBUNIFU, SOGA TU OFISINI NA kufanya kazi kwa mazoea-BUSINESS AS USUAL, ili mradi mwisho wa mwezi ufike waende kwenye ATM-kula kodi zetu.

Mkuu wa Mkoa wa Dsm, Paulo Makonda aliwahi kusema kuwa SERIKALI ina wafanyakazi wengi sana wasio na KAZI, MIZIGO. Nafikiri ni wakati muafaka kwa serikali kupitisha fagio la chuma, kubakisha watumishi wenye ueledi, tija na wabunifu, WENYE KUFANYA KAZI, SI KUPOKEA SALARI TU. Kuna mizigo mingi sana kwenye UTUMISHI wa umma. Magu pitia huku-watumishi waliopo, ambao si hewa, lakini hawana tija, mizigo, WAPOKEA SALARI TU BILA KUREJESHA HUDUMA ZENYE TIJA, WELEDI NA KWA WAKATI kwa jamii inayowalipa.
http://moruwasa.go.tz/home/index.php?option=com_content&task=view&id=47&Itemid=64
 
Polen Mkuu, vp na kwa Wakubwa kwao maji Hamna mfano RC kambi za jeshi n.k lakin mkuu hako nako kafursa cha kutokea, hata kama una corolla gx Unapiga nako kazi Ndo 1=500? hataliii
 
Polen Mkuu, vp na kwa Wakubwa kwao maji Hamna mfano RC kambi za jeshi n.k lakin mkuu hako nako kafursa cha kutokea, hata kama una corolla gx Unapiga nako kazi Ndo 1=500? hataliii
mkuu hii biashara nilipiga sana na ka gari ka dingi kakaja kufa ila hela nje nje yani kama mtu unakirikuu ndo umeulaa

kufa kufaana huku
 
Mbona mi nakaa kihonda bima hapa hamna shida ya maji
Inaongelewa kihonda kwa chambo ndugu. Fika kule uone. Infact ni kama hawa jamaa wanafanya makusudi kutengeneza uhaba ili wafaidike kupitia malori ya kuuza maji ambayo nadhani wanakuwa na maslahi nayo. Watu wa kihonda wakikomaa kidogo, huzugwa kwa kuletewa maji kama mara mbili hivi kisha hujisahaulisha kabisa. Kibaya zaidi kila mwisho wa mwezi wananchi hupelekewa bili za maji. Ni shida.
 
Nenda ofisini kawambie acha uwoga wakijibu ovyo panda kazi za juu. Maji ni uhai
 
Mindu na kibwe ni vyanzo vya zamani, wajitahidi kule juu kutunza mazingira ili iwe Moro yamaji yatiririka.
 
Hata kilakala hakuna maji wanafunzi wa kilakala sec kunakipindi walikuwa wanatoka nje ya uzio kwenda kuchota maji shule ya kiislamu ya darul arqam mimbamimba sidhani kama walikosa
 
Maji moro ni shida ila hata vyanzo vya maji vimepungua kwa uharibifu wa mazingira na ongezeko la idadi ya watu.miti mingi haina maji kwa sasa km huko bigwa ni mikavu kabisa. Uongozi ni kubuni njia za kutunza mazingira na kurejesha uoto wa asili wa milima ya uluguru ila mvua sinyeshe na maji yawe mengi huko milimani. Na ni kweli kuna maeneo maji yapo kila siku huko kwani hao wanaouza wanayatoa wapi?
 
Kwa hakika mheshimiwa Rais Magufuli anafanya vizuri sana. Tanzania ilipokuwa imefika, ilikuwa inahitaji kuwa na Rais kama Magufuli. Historia inaonesha kwamba, MUNGU HUMLETA MTU FULANI KATIKA ENEO HUSIKA KWA WAKATI NA MALENGO MAALUMU.
 
Naomba Rais Magufuli atoe tamko (amri ) ya kuingiza UMEME katika shule zote zilizopitiwa na line ya umeme. Ninathubutu kusema hivi kwa sababu utakuta nguzo za umeme zimepita uwanjani mwa shule lakini shule hiyo inakaa bila umeme kwa muda wa miaka mingi kana kwamba umeme hauna manufaa kabisa katika shule. Mfano mzuri wa shule ambazo zipo katikati ya mji lakini hazina umeme ni pamoja na SHULE ZA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO KATIKA MKOA WA NJOMBE. Pamoja na matumizi mengine ya umeme, umeme katika shule hizo ungeweza kutumika kwa ajili ya kuchapa mitihani nk. Kwa kuwa suala la MADAWATI limefanikiwa kwa asilimia nyingi, ninaamini hata hili likitiliwa mkazo linawezekana tena haraka sana. MUNGU MBARIKI RAIS JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, SERIKALI YAKE NA WATANZANIA WOTE. Amina.
 
kero yangu kubwa ni kuona kuwa wakuu wa wilaya wanakimbizana na wavuvi haramu wakati sisi wenye leseni ya uchimbaji madini tumepeleka taarifa kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya kuwa kuna wachimbaji haramu,wala hata hawashughulikiwi
 
Mimi kero yangu natamani kujua Lugumi ni Nani na kwa nini hili suala halishugulikiwi
 
BIMA YA AFYA NI JIPU LA KULIANGAZIA

Wanabodi, hongereni kwa constructive criticism.

Leo nimeona nije na hili suala la BIMA ya afya, to be specific, NHIF.

Kwanza niwapongeze waliokuja na wazo hili, ni msaada mkubwa hasa kwa watumishi wa umma ambao majority hawana uhakika wa kujiwekea akiba kwa ajili ya matibabu.

Lakini kwa upande mwingine BIMA hii imekuwa kama ni upigaji wa mishahara ya watumishi wa umma kutoka kwenye makato ya mishahara yao baada ya kukatwa kwa lazima kama sheria inavyoelekeza.

Nasema ni upigaji kwa sababu makato hayaendani na huduma zitolewazo pindi wanapozihitaji.

Katika kuhusisha suala hili, HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA nitaichukulia kama CASE STUDY.

Juzi nilikuwa na uhitaji wa huduma ya afya kwa kutumia mpango wa BIMA ya afya ya NHIF. Nilifika mapokezi na kuandikisha kama kawaida. Nilipoingia ndani ili nihudumiwe, kero zifuatazo zilinikuta:-
1/ Upungufu wa wahudumu:
Matabibu ni wachache na waliopo wanaanza asubuhi mpaka jioni bila ya kuwepo kwa wengine waingie kwa shift. Hivyo kwa mtazamo wangu huwa wanachoka kwa masaa mengi ya kazi.

Pia mtu wa maabara alikuwa mmoja kwa siku hiyo kuhudumia msululu wa watu kwa siku nzima.

2/ Majibu na kauli mbaya kwa wateja:-
Ilipofika saa 11 alibaki Tabibu mmoja wa mlango wa Wazee ambaye alikuwa akitoa kauli chafu kwa wateja pale walipohoji uharaka wa huduma. Hii ikizingatia kuwa kuna kinamama, watoto, wazee na wajawazito waliokuwa hapo tangu asubuhi na hawapata huduma kwa wakati.

3/ Upungufu wa vifaa tiba:-
Kuna baadhi ya vipimo havipatikani kwenye jengo hilo mpaka uambiwe ukafuate upande wa HOSPITALI ya MKOA.
Pia baadhi ya dawa hazipatikani kwenye dirisha la dawa mpaka uende Pharmacy za nje.

HITIMISHO:-
Naomba kero za hapo juu zifanyiwe kazi ili huduma ziendane na makato ya lazima kwenye mishahara ya watumishi wa umma.

N.B:-
MALAIKA MZIMA JF USIIGUSE TENA HII KITU, NI YA MUHIMU KWETU.
 
BIMA YA AFYA NI JIPU LA KULIANGAZIA

Wanabodi, hongereni kwa constructive criticism.

Leo nimeona nije na hili suala la BIMA ya afya, to be specific, NHIF.

Kwanza niwapongeze waliokuja na wazo hili, ni msaada mkubwa hasa kwa watumishi wa umma ambao majority hawana uhakika wa kujiwekea akiba kwa ajili ya matibabu.

Lakini kwa upande mwingine BIMA hii imekuwa kama ni upigaji wa mishahara ya watumishi wa umma kutoka kwenye makato ya mishahara yao baada ya kukatwa kwa lazima kama sheria inavyoelekeza.

Nasema ni upigaji kwa sababu makato hayaendani na huduma zitolewazo pindi wanapozihitaji.

Katika kuhusisha suala hili, HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA DODOMA nitaichukulia kama CASE STUDY.

Juzi nilikuwa na uhitaji wa huduma ya afya kwa kutumia mpango wa BIMA ya afya ya NHIF. Nilifika mapokezi na kuandikisha kama kawaida. Nilipoingia ndani ili nihudumiwe, kero zifuatazo zilinikuta:-
1/ Upungufu wa wahudumu:
Matabibu ni wachache na waliopo wanaanza asubuhi mpaka jioni bila ya kuwepo kwa wengine waingie kwa shift. Hivyo kwa mtazamo wangu huwa wanachoka kwa masaa mengi ya kazi.

Pia mtu wa maabara alikuwa mmoja kwa siku hiyo kuhudumia msululu wa watu kwa siku nzima.

2/ Majibu na kauli mbaya kwa wateja:-
Ilipofika saa 11 alibaki Tabibu mmoja wa mlango wa Wazee ambaye alikuwa akitoa kauli chafu kwa wateja pale walipohoji uharaka wa huduma. Hii ikizingatia kuwa kuna kinamama, watoto, wazee na wajawazito waliokuwa hapo tangu asubuhi na hawapata huduma kwa wakati.

3/ Upungufu wa vifaa tiba:-
Kuna baadhi ya vipimo havipatikani kwenye jengo hilo mpaka uambiwe ukafuate upande wa HOSPITALI ya MKOA.
Pia baadhi ya dawa hazipatikani kwenye dirisha la dawa mpaka uende Pharmacy za nje.

HITIMISHO:-
Naomba kero za hapo juu zifanyiwe kazi ili huduma ziendane na makato ya lazima kwenye mishahara ya watumishi wa umma.

N.B:-
MALAIKA MZIMA JF USIIGUSE TENA HII KITU, NI YA MUHIMU KWETU.

Pole sana mkuu. Nadhani hayo mapungufu yanawahusu wamiliki wa hiyo hospitali na sio NHIF. Hupati hizo shida kwa sababu una kadi ya NHIF. Na hata kama usingekuwa na kadi ya NHIF bado ungepata shida hizo hizo.
 
Back
Top Bottom