Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Mhemiwa Rais fanya uwezavyo tupate katiba mpya,right aliokuwa anafanya hayati Molinge yangekuwa katika format leo ungefanya kuyaendeleza tuu,Mungu ibariki Tanzania.
 
Naomba nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoifanya ili kulikomboa taifa letu fukara. Najua nchi hii tukimuachia Rais peke yake hataiweza kamwe kwani kunachangamoto kubwa sana za kitaifa ambazo tumezilea kwa muda mrefu sana kama taifa na hivyo kuwa donda ndugu kwa maendeleo na mustakabali wa taifa letu. Mfano mafisadi na wala rushwa ambao wametamalaki katika taifa hili toka ngazi za juu hadi chini.
Rais kwa kumtazama jinsi anavoongea na kutenda inaonyesha ana nia ya dhati kabisa ya kulikomboa taifa hili. Ila katikati ya kulikomboa taifa anamaadui wengi waliokuwa wakinufaika na mfumo mbovu wa uongozi wa taifa hili. Maadui hao wapo ndani ya CCM na wengine wapo nje ya CCM hili ndugu zangu lazima tulijue bila ubishi, pia na Mheshimiwa Rais analijua hilo.
Kumjua adui ni jambo moja na kupambana naye ni jambo jingine.
Mheshimiwa Rais mimi binafsi namuomba Mungu akujalie hekima na busara zaidi ili wewe nasi wananchi kwa ujumla wetu tushirikiane tuipeleke nchi yetu mbele; Pia Watanzania tuweke itikadi zetu zote pembeni zikiwepo za kisiasa, kidini na kikabila. Najua katikati ya juhudi za kulikomboa taifa ADUI ni wengi sana hasa wanufaika wa mfumo uliotufikisha hapa, lakini kwa umoja wetu kama taifa tutashinda.
Mimi binafsi ni mwanachama wa CHADEMA lakini nachokiomba upinzani kwa ujumla tusiendeshe siasa kama ushabiki wa Simba na Yanga. Hili ni taifa hivyo vizazi vingi vyetu vitakuja na kustaajabu madudu tuliyokuwa tunayafanya kwa kutokua na mikakati yeyote ile zaidi ya ubishani tu. Kwa sasa si wakati wa kumvizia Rais na serikali yake wakosee ili kupata sehemu ya kuwakosoa, nacho kiomba tunapo ona mambo hayaendi ni wakati wa kumuona Rais na kutoa ushauri kabla janga halijatupata kama taifa vinginevyo Rais akatae huo ushauri. Naomba tuige siasa za watu wa Ulaya na Marekani. Ambapo wao baada ya chaguzi hurudi na kuwa kitu kimoja kujenga mataifa yao.
Pia CCM naomba muelewe kuwa sasa ni wakati wa kulijenga taifa imara kiuchumi na sio wakati wa kuchuma kupitia serikali. Tunacho mshukuru Mungu tumempata Rais anayesubutu kufanya anachokisema hivyo ni wakati wa kumwacha Rais awe huru na sio kumzonga Rais na kumpanda kichwani na kuliyumbisha taifa.
Rais tuliyempata sio Mungu hilo tulijue anamapungufu kama mwanadamu hivyo anahitaji washauri wazuri wenye nia njema wasio na hila , pia hawezi kugeuza hii nchi kwa siku moja hilo tulijue.
Mtanzania mwenzangu toa mawazo yako tumsaidie Rais kulijenga taifa letu.
Maoni yangu umeishayaongea kwenye hoja zako.

Ninakushukuru sana kwa thread yenye mawazo ya kujenga taifa na siyo unafiki uliojificha ndani ya ngozi za uzalendo.
 
Serikali ya viwanda ni Serikali yenye maamuzi. Nyie mtuache na maushauri yenu ambayo hayana kichwa wala miguu. Hapa kazi tuu. Huo ndo ushauri mkuu.

Swali la kizushi. Government Instruments zishatangazwa kwa awamu hii ya Tano?
 
Wakuu kwema,

Najiuliza je hili ni agizo la rais au ndo kusema kumuhujumu rais wetu?

Kama ilivyo ada mimi najiuliza magufuli kawaambia halimashauri walirudishe ushuru wa mazao (holela) mfano wilaya ya Sengerema watu wengi ni wakulima na wavuvi, lakini wakulima ndo wengi zaidi katika utafiti wangu mdogo nikiwa natokea nyamazugu nikaona barrier kuna mgambo nikaeenda weekend hii baratogwa maeneo ya njia panda ya Sengerema sekondari bBratogwa na Mwabaruhi kuna barrier nyingine.


Sasa nini zinafanya barrier hizi..
Wanakamata gunia za mahindi za mpunga udaga na nafaka zingine unapigwa ushuru sasa swali langu najiuliza wakazi wengi wa mji wa Sengerema wamelima mazao ya chakula kwa subsistence sasa ushuru huu watu wana laani kweli.

Je hii ni sawa kwa kila mazao uliyo lima mwenyewe ulipie ushuru tena kwa matumizi yako binafsi au ni hujuma ya wilaya ya Sengerema kwa rais?
 
Sisi watanzania tuliowanyonge, tuliokuchagua tunakuunga mkono kwa 100% kwa hatua zote unazochukua zidi ya mafisadi na wahujumu uchumi. Wanao jaribu kukukatisha tamaa ni wachache sana, ila kundi kubwa tupo nyuma yako. Mungu wetu mkuu atawaangusha wote wale wanaonena maneno ya kejeli juu yako.

Kama walivyopata kunena juu ya udhaifu wa serikali iliyopita, basi watanena maneno ya kukukatisha tamaa kwa sababu tu wao wanaweza kupata muda kwenye vyombo vya habari, ila wananchi tunakuelewa zaidi wewe amri jeshi mkuu, maana ndiye tuliyekupatia dhamana ya kusimamia maslahi ya taifa na sisi wanyonge.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu Mbariki Dr. Magufuli!
 
Jipu lingne lipo Chuo cha usimamizi wa fedha IFM huyu acting rector aliyewekwa ni Bonge la jipu na yeye pamoja na wenzie wachache ndie aliyekwamisha maendeleo ya chuo kabla hajawa acting rector

Nadhani wewe una chuki naye, eleza tatizo lake ni nini siyo kutuletea majungu humu
 
Sisi watanzania tuliowanyonge, tuliokuchagua tunakuunga mkono kwa 100% kwa hatua zote unazochukua zidi ya mafisadi na wahujumu uchumi. Wanao jaribu kukukatisha tamaa ni wachache sana, ila kundi kubwa tupo nyuma yako. Mungu wetu mkuu atawaangusha wote wale wanaonena maneno ya kejeli juu yako.

Kama walivyopata kunena juu ya udhaifu wa serikali iliyopita, basi watanena maneno ya kukukatisha tamaa kwa sababu tu wao wanaweza kupata muda kwenye vyombo vya habari, ila wananchi tunakuelewa zaidi wewe amri jeshi mkuu, maana ndiye tuliyekupatia dhamana ya kusimamia maslahi ya taifa na sisi wanyonge.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu Mbariki Dr. Magufuli!
kundi kubwa lkn hamna nguvu ni wa kuburuzwa tu
 
Ndugu wana JamiiForums,

Nchi yetu imetafunwa mno na ni wakati sasa tuseme imetosha. Tumsaidie Rais Magufuli na Serikali yake kuweza kuzifahamu kero zetu za yanayotusumbua kama watanzania ambayo tungependa yafanyiwe kazi.

Karibuni sana.

MWONGOZO:
Elezea jipu/kero yako na kama ina ufafanuzi wa kutosha (nani, wapi, lini, kivipi n.k) ukiambatana na nyaraka itapendeza zaidi.

Kero hizi zitachapwa na kupelekwa kwa mamlaka husika ili zifanyiwe ufuatiliaji.

Hizi nyumba za serikali zilizouzwa kwa bei ya chini sana huu ni ufisadi kwa mtanzania pia ni vyema jipu hili likatumbuliwa haraka sana
 
Tangu awamu ya tano imeingia madarakani, kumezuka mtindo wa kuteka akili zetu kuhusu maamuzi yanayotolewa na viongozi wetu katika ngazi tofauti, ila swala la kujiuliza ni kati ya amri na sheria ni kipi kina nguvu ya kuamua jambo.!!?? ........ Nauliza tu
 
Tozo Daraja la Nyerere ni kero nyingine, Kwanini kupita darajani iwe gharama sawa au zaidi ya kivuko ambacho kinatumia mafuta,kinafanyiwa service ya mara kwa mara pamoja na kubadilisha spare chakavu? Mmepunguzia wananchi matatizo kwa kuwaongezea gharama za maisha!
 
Vyuo vya ualimu utaratibu wa kuwapata wakuu wa vyuo ni wa hovyo teuzi zinafanywa za hovyo na ndizo zinazofanya vyuo vya uwalimu vya serikali kushindwa kujiendesha na vinabaki kuwa duni tu kwa kuwa wakuu wa vyuo hawana mawazo ya kuviendeleza ni vyema utaratibu huu ukabadilishwa na wakuu wawe wanapatikana kwa kushindanishwa ili kumpata mtu Bora na makini
 
Jipu lingine ni wizara ya elimu nina maanisha Wizarani watumishi hawalipwi madeni yao miaka nenda rudi hata mishahara ya nyuma imekuwa tatizo kulipa
 
Ndugu wana JamiiForums,

Nchi yetu imetafunwa mno na ni wakati sasa tuseme imetosha. Tumsaidie Rais Magufuli na Serikali yake kuweza kuzifahamu kero zetu za yanayotusumbua kama watanzania ambayo tungependa yafanyiwe kazi.

Karibuni sana.

MWONGOZO:
Elezea jipu/kero yako na kama ina ufafanuzi wa kutosha (nani, wapi, lini, kivipi n.k) ukiambatana na nyaraka itapendeza zaidi.

Kero hizi zitachapwa na kupelekwa kwa mamlaka husika ili zifanyiwe ufuatiliaji.


Mirejesho jamani ilikuwa tia moyo wanajamii!
 
Heshima sana wanajamvi,

Serekali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dr John Pombe Makufuli yenye kutumia kauli mbiu "Hapa Kazi tu" inatimiza miezi saba tangu kuingia madarakani mwaka jana mwezi October 2015.

Dr Magufuli alianza na speed kubwa ya kutumbua MAJIPU BILA KUKAMUA" na kupongezwa na sehemu kubwa ya waTanzania.Tulishuhudia CEO wa TAKUKURU,TRA,NIDA,TIC........ wakitumbuliwa majipu mchana kweupe pasipo kukamuliwa.

Kwanini nasema Dr Magufuli anatumbua Majipu pasipo kukamua.Jipu likitumbuliwa ni lazima likamuliwe ili kuondoa tatizo moja kwa moja.Ukilitumbua jipu ukaliacha hivi hivi maana yake usaa utabaki ndani na pengine linaweza kutengeneza tatizo lingine kubwa sana kuliko hata jipu la mwanzo.

Kufukuza watumishi wa ngazi za juu kwa mbwembwe hakuondoi tatizo hata kidogo.Ikiwa mhusika ni mbadhirifu,fisadi...... unapomwondoa katika nafasi yake pasipo kutazama sababu / mfumo uliosababisha ubadhirifu / ufisadi ukatokea unakuwa haujaondoa tatizo.

Dr Magufuli na serekali yake watatakiwa kuutazama mfumo mzima unaotuzalishia viongozi/watendaji wabadhirifu.Sheria,kanuni na taratibu lazima zibadilishwe ili watendaji wote watakao jihusisha na ubadhirifu,rushwa mfumo uwashughulike.

Sheria ya maadili ya uongozi wa umma lazima iboreshwe sana tena sana pasipo kuchelewa hata kidogo.

Ziara za kushtukiza naziona kama aina nyingine ya usanii ya kutafuta au kujiongeza umaarufu hasa mbele ya jamii iliyokata tamaa,ambayo ipo tayari kushangilia usanii unaotendwa na wanasiasa wanaojua kucheza na akili ndogo.

Kutumbua majipu sawa lakini lazima yakamuliwe,yasafishwe,kufungwa na kuwekewa dawa sahihi.

Katiba ya Jaji Warioba ndio jibu sahihi.
 
Majipu DART mtandao unahujumiwa ili mradi wa mabasi usifanye kazi inayotakiwa fikiria mabasi yanaenda tupu kisamtandao hamna huku Abiria wamejaa kituon
 
Ndugu wana JamiiForums,

Nchi yetu imetafunwa mno na ni wakati sasa tuseme imetosha. Tumsaidie Rais Magufuli na Serikali yake kuweza kuzifahamu kero zetu za yanayotusumbua kama watanzania ambayo tungependa yafanyiwe kazi.

Karibuni sana.

MWONGOZO:
Elezea jipu/kero yako na kama ina ufafanuzi wa kutosha (nani, wapi, lini, kivipi n.k) ukiambatana na nyaraka itapendeza zaidi.

Kero hizi zitachapwa na kupelekwa kwa mamlaka husika ili zifanyiwe ufuatiliaji.
**USHAURI MDOGO KWA WAZIRI WA UTUMISHI**

UKIKATA MISHAHARA WATUMISHI WANAOCHELEWA KUFIKA KAZINI, KUNA UWEZEKANO WA KUTENGENEZA MADAWATI 10,000 KILA MWEZI KWA NCHI NZIMA:


mheshimiwa waziri, kama kuna kitu kinachokwamisha utendaji kazi kwa ufanisi na uwajibikaji miongozi mwa watumishi wa umma katika ofisi nyingi za serikali kuu,halmashauri na wilaya ni uchelewaji wa kufika kazini na suala zima la kutozingatia muda na maadili ya kazi na hii huchangiwa na ukosefu wa kamera za CCTV katika ofisi karibia zote za serikali, ambazo uwepo wake utakusaidia wewe na uongozi wako kuweza ku-monitor mienendo ya wafanyakazi kwenye kila ofisi ya serikali, halmashauri na wilaya. Kama inawezekana kwa supermarkets na maduka madogo madogo hata kwa huku mtaani kwetu kuwa na kamera za ulinzi, inashindikana vipi katika ofisi za serikali kama watu wapo serious??? bado nipo ninaandaa dodosi kamili la namna gani unaweza kutekeleza utaratibu wa namna hii kama ushauri wangu binafsi na kuweza kuzaa matunda ambayo watanzania wahatakaa kukusahau, and mark my words,
utarudisha nidhamu ya kazi kwa watumishi ofisi za serikalini for 80% na kupunguza idadi ya wanafunzi wanaosoma kwa kukaa chini for the same percentage countrywide!!!!!
 
Jipu uchungu nimeliona hospitali ya Mwananyamala kitengo cha maabara watu wanaanza kupewa huduma saa tano. Na wakati wafanyakazi wanafika ofisini saa moja wao ni stori tu na kuacha wagonjwa wanaendelea kuzidiwa....

Mtu amepima toka jana lakini kumpa tu majibu yake asubiri hadi saa tano ndo waanze kutoa majibu....wao na stori tu ofisini
Hao ndio watz wwanaofanya matamasha ya kuwapongeza wapiga viroba , ili kuwatongoza wazuie wageni wasipewe kazi, na wao waongezwe mishahara.
 
MAWAKALA WA MIZIGO WANAPOKUWA WASHAURI KWA WATEJA KUTOLIPA KODI

Nauliza tu jamani Watanzania wenzangu nimeiona sehemu anae clear mizigo agent yaani anaruhusiwa kumshawishi mteja apunguziwe kodi ama asilipe kabisaa msamaa yaani na akafanya mchakato mzima na hata kodi ikakwepwa kulipwa?

Kazi ya Agent kama ni mzawa anatakiwa afanye nini kulinufaisha Taifa lake? Nimeisoma sehemu moja Ofisi iko Ndani ya Uwanja wa saba saba Ukweli nimekereheka kama si kukwazika Samahani napita tu,Nikaenda mbali kuuliza kama alifanikiwa kumshawishi mteja wake nikaambiwa alifanikiwa, leo yule jamaa kanidokeza tena eti ameshawishi tena kusamehewa kodi halafu vitu vyenyewe ni malighafi ambayo Babu na Bibi walivilinda miaka mingiii ili sisi wajukuu wachimbaji wadogo wadogo wanufaike.

Mali inatoka nje Bondeni kwa hapa Bongo iko Makuyuni, Makanya hata Lindi mawe Matatu na Liganga na Mchuchuma????Wanapingana kabisa na JPM kuhusu Tozo la Thamani (18%) mmmmm
 
Kuna hili tatizo la mlundikano wa wafungwa magerezani, hasa wale wenye vifungo vidogo ( miaka mitatu kushuka chini) Serikali iwezeshe idara ya vifungo vya nje,...kwa kuongeza wafanyakazi na vitendea kazi.

Hakuna sababu ya kuendelea kuwa na miji michafu, wakati watu wakufanya usafi wamejazana Gerezani. Kila mwezi 1.7 billion zinatumika kwa mwezi kuhudumia magereza.

Wahalifu wakitumikia adhabu nje ya Gereza ni funzo kubwa kwao kuliko wakiwa Gerezani. Mtu kaiba kuku alafu anaishi na jambazi sugu, Mwisho wa siku Mwizi wa kuku tunamjengea mauzoefu maana anaweza kujifunza mengi akiwa huko...na siku akitoka anaweza kuwa hatari zaidi.

Tuwe wabunifu.
 
Upungufu wa sukari ushauri kwa serikali: Kwa kuwa mpaka Leo bado sukari inazidi kupanda being. Serikali ielekeze 'mkono' wake kwenye maduka ya rejareja yanayouza sukari kwa bei mbaya na kuwakamata hao waeleze wamepata wapi sukari wanayouza kwa 'mwendo wa kuruka'. Kwa njia hiyo itakuwa rahisi kwa Serikali kuwagungua wanaohodhi sukari na kuiuza kwa bei ya juu na kuwachukulia hatua kali!
 
Back
Top Bottom